< 1 Wakorintho 16 >
1 Basi kuhusu changizo kwa ajili ya watakatifu: Kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia, fanyeni vivyo hivyo.
Now concerning the collection for the saints, according to the directions which I gave to the churches of Galatia, so also do ye.
2 Siku ya kwanza ya kila juma, kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha, kulingana na mapato yake na fedha hizo aziweke akiba, ili nitakapokuja pasiwe na lazima ya kufanya mchango.
Every first day of the week let each of you lay by him something in store, according as he hath prospered; that the collections may not have to be made when I come.
3 Kwa hiyo nitakapowasili, nitawapa wale mtakaowachagua barua za kuwatambulisha, ili kuwatuma wapeleke zawadi zenu huko Yerusalemu.
And when I am with you, I will send with letters whomever you may approve to carry your bounty to Jerusalem;
4 Kama ikionekana ni vyema na mimi niende, basi hao watu watafuatana nami.
and if it be worth while for me to go also, they shall go with me.
5 Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia.
Now I will come to you, when I have passed through Macedonia; for I am about to pass through Macedonia;
6 Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo.
and perhaps I may remain, or even spend the winter with you, that ye may set me forward on my journey whithersoever I may be going.
7 Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda.
For I am unwilling to see you now in passing; for I hope to stay some time with you if the Lord permit.
8 Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste,
But I shall remain at Ephesus until the Pentecost;
9 kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.
for a door hath been opened to me great and effective, and there are many adversaries.
10 Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo.
Now if Timothy come, see that he be with you without fear; for he is laboring in the work of the Lord, as I am;
11 Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.
let no one therefore despise him. But conduct him on in peace, that he may come to me; for I am waiting for him with the brethren.
12 Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.
As regards Apollos, the brother, I urged him much to come to you with the brethren; and it was not at all his will to come at this time; but he will come when he hath a convenient opportunity.
13 Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari.
Watch, stand fast in the faith, quit you like men, be strong;
14 Fanyeni kila kitu katika upendo.
let all your doings be in love.
15 Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi,
And I exhort you, brethren, —ye know the family of Stephanas, that they are the first-fruits of Achaia, and that they have devoted themselves to the service of the holy, —
16 mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii.
that ye submit yourselves to such as they are, and to every one that worketh with us, and laboreth.
17 Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu.
I am glad of the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus; for what was lacking on your part, they supplied;
18 Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.
for they refreshed my spirit and yours. Pay regard then to those that are such.
19 Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana.
The churches of Asia salute you. Aquila and Prisca, with the church that is in their house, send you many salutations in the Lord.
20 Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
All the brethren salute you. Salute one another with a holy kiss.
21 Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.
The salutation of me, Paul, with my own hand.
22 Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.
If any one loveth not the Lord, let him be accursed! The Lord is at hand.
23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
The grace of the Lord Jesus be with you.
24 Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.
My love is with you all in Christ Jesus.