< 1 Wakorintho 15 >
1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
notum autem vobis facio fratres evangelium quod praedicavi vobis quod et accepistis in quo et statis
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
per quod et salvamini qua ratione praedicaverim vobis si tenetis nisi si frustra credidistis
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
tradidi enim vobis in primis quod et accepi quoniam Christus mortuus est pro peccatis nostris secundum scripturas
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
et quia sepultus est et quia resurrexit tertia die secundum scripturas
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
et quia visus est Cephae et post haec undecim
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
deinde visus est plus quam quingentis fratribus simul ex quibus multi manent usque adhuc quidam autem dormierunt
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
deinde visus est Iacobo deinde apostolis omnibus
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
novissime autem omnium tamquam abortivo visus est et mihi
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
ego enim sum minimus apostolorum qui non sum dignus vocari apostolus quoniam persecutus sum ecclesiam Dei
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
gratia autem Dei sum id quod sum et gratia eius in me vacua non fuit sed abundantius illis omnibus laboravi non ego autem sed gratia Dei mecum
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
sive enim ego sive illi sic praedicamus et sic credidistis
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
si autem Christus praedicatur quod resurrexit a mortuis quomodo quidam dicunt in vobis quoniam resurrectio mortuorum non est
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
si autem resurrectio mortuorum non est neque Christus resurrexit
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
si autem Christus non resurrexit inanis est ergo praedicatio nostra inanis est et fides vestra
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
invenimur autem et falsi testes Dei quoniam testimonium diximus adversus Deum quod suscitaverit Christum quem non suscitavit si mortui non resurgunt
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
nam si mortui non resurgunt neque Christus resurrexit
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
quod si Christus non resurrexit vana est fides vestra adhuc enim estis in peccatis vestris
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
ergo et qui dormierunt in Christo perierunt
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
si in hac vita tantum in Christo sperantes sumus miserabiliores sumus omnibus hominibus
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
nunc autem Christus resurrexit a mortuis primitiae dormientium
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
quoniam enim per hominem mors et per hominem resurrectio mortuorum
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
et sicut in Adam omnes moriuntur ita et in Christo omnes vivificabuntur
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
unusquisque autem in suo ordine primitiae Christus deinde hii qui sunt Christi in adventu eius
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
deinde finis cum tradiderit regnum Deo et Patri cum evacuaverit omnem principatum et potestatem et virtutem
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
oportet autem illum regnare donec ponat omnes inimicos sub pedibus eius
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
novissima autem inimica destruetur mors omnia enim subiecit sub pedibus eius cum autem dicat
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
omnia subiecta sunt sine dubio praeter eum qui subiecit ei omnia
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
cum autem subiecta fuerint illi omnia tunc ipse Filius subiectus erit illi qui sibi subiecit omnia ut sit Deus omnia in omnibus
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
alioquin quid facient qui baptizantur pro mortuis si omnino mortui non resurgunt ut quid et baptizantur pro illis
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
ut quid et nos periclitamur omni hora
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
cotidie morior per vestram gloriam fratres quam habeo in Christo Iesu Domino nostro
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
si secundum hominem ad bestias pugnavi Ephesi quid mihi prodest si mortui non resurgunt manducemus et bibamus cras enim moriemur
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
nolite seduci corrumpunt mores bonos conloquia mala
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
evigilate iuste et nolite peccare ignorantiam enim Dei quidam habent ad reverentiam vobis loquor
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
sed dicet aliquis quomodo resurgunt mortui quali autem corpore veniunt
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
insipiens tu quod seminas non vivificatur nisi prius moriatur
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
et quod seminas non corpus quod futurum est seminas sed nudum granum ut puta tritici aut alicuius ceterorum
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
Deus autem dat illi corpus sicut voluit et unicuique seminum proprium corpus
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
non omnis caro eadem caro sed alia hominum alia pecorum alia caro volucrum alia autem piscium
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
et corpora caelestia et corpora terrestria sed alia quidem caelestium gloria alia autem terrestrium
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
alia claritas solis alia claritas lunae et alia claritas stellarum stella enim ab stella differt in claritate
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
sic et resurrectio mortuorum seminatur in corruptione surgit in incorruptione
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
seminatur in ignobilitate surgit in gloria seminatur in infirmitate surgit in virtute
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
seminatur corpus animale surgit corpus spiritale si est corpus animale est et spiritale sic et scriptum est
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
factus est primus homo Adam in animam viventem novissimus Adam in spiritum vivificantem
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
sed non prius quod spiritale est sed quod animale est deinde quod spiritale
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
primus homo de terra terrenus secundus homo de caelo caelestis
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
qualis terrenus tales et terreni et qualis caelestis tales et caelestes
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
igitur sicut portavimus imaginem terreni portemus et imaginem caelestis
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
hoc autem dico fratres quoniam caro et sanguis regnum Dei possidere non possunt neque corruptio incorruptelam possidebit
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
ecce mysterium vobis dico omnes quidem resurgemus sed non omnes inmutabimur
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
in momento in ictu oculi in novissima tuba canet enim et mortui resurgent incorrupti et nos inmutabimur
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
oportet enim corruptibile hoc induere incorruptelam et mortale hoc induere inmortalitatem
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
cum autem mortale hoc induerit inmortalitatem tunc fiet sermo qui scriptus est absorta est mors in victoria
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs )
ubi est mors victoria tua ubi est mors stimulus tuus (Hadēs )
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
stimulus autem mortis peccatum est virtus vero peccati lex
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Deo autem gratias qui dedit nobis victoriam per Dominum nostrum Iesum Christum
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
itaque fratres mei dilecti stabiles estote et inmobiles abundantes in opere Domini semper scientes quod labor vester non est inanis in Domino