< 1 Wakorintho 15 >

1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
Now I declare to you, brothers, the Good News which I preached to you, which also you received, in which you also stand,
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
by which also you are saved, if you hold firmly the word which I preached to you—unless you believed in vain.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
For I delivered to you first of all that which I also received: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
that he was buried, that he was raised on the third day according to the Scriptures,
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
and that he appeared to Cephas, then to the twelve.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
Then he appeared to over five hundred brothers at once, most of whom remain until now, but some have also fallen asleep.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
Then he appeared to James, then to all the apostles,
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
and last of all, as to the child born at the wrong time, he appeared to me also.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, who is not worthy to be called an apostle, because I persecuted the assembly of God.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am. His grace which was given to me was not futile, but I worked more than all of them; yet not I, but the grace of God which was with me.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
Whether then it is I or they, so we preach, and so you believed.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
Now if Christ is preached, that he has been raised from the dead, how do some among you say that there is no resurrection of the dead?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
But if there is no resurrection of the dead, neither has Christ been raised.
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
If Christ has not been raised, then our preaching is in vain and your faith also is in vain.
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
Yes, we are also found false witnesses of God, because we testified about God that he raised up Christ, whom he didn’t raise up if it is true that the dead are not raised.
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
For if the dead aren’t raised, neither has Christ been raised.
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
If Christ has not been raised, your faith is vain; you are still in your sins.
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
Then they also who are fallen asleep in Christ have perished.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
If we have only hoped in Christ in this life, we are of all men most pitiable.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
But now Christ has been raised from the dead. He became the first fruit of those who are asleep.
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
For since death came by man, the resurrection of the dead also came by man.
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
For as in Adam all die, so also in Christ all will be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
But each in his own order: Christ the first fruits, then those who are Christ’s at his coming.
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
Then the end comes, when he will deliver up the Kingdom to God the Father, when he will have abolished all rule and all authority and power.
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
For he must reign until he has put all his enemies under his feet.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
The last enemy that will be abolished is death.
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
For, “He put all things in subjection under his feet.” But when he says, “All things are put in subjection”, it is evident that he is excepted who subjected all things to him.
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
When all things have been subjected to him, then the Son will also himself be subjected to him who subjected all things to him, that God may be all in all.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
Or else what will they do who are baptized for the dead? If the dead aren’t raised at all, why then are they baptized for the dead?
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
Why do we also stand in jeopardy every hour?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
I affirm, by the boasting in you which I have in Christ Jesus our Lord, I die daily.
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
If I fought with animals at Ephesus for human purposes, what does it profit me? If the dead are not raised, then “let’s eat and drink, for tomorrow we die.”
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Don’t be deceived! “Evil companionships corrupt good morals.”
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
Wake up righteously and don’t sin, for some have no knowledge of God. I say this to your shame.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
But someone will say, “How are the dead raised?” and, “With what kind of body do they come?”
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
You foolish one, that which you yourself sow is not made alive unless it dies.
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
That which you sow, you don’t sow the body that will be, but a bare grain, maybe of wheat, or of some other kind.
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
But God gives it a body even as it pleased him, and to each seed a body of its own.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
All flesh is not the same flesh, but there is one flesh of men, another flesh of animals, another of fish, and another of birds.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
There are also celestial bodies and terrestrial bodies; but the glory of the celestial differs from that of the terrestrial.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
There is one glory of the sun, another glory of the moon, and another glory of the stars; for one star differs from another star in glory.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
So also is the resurrection of the dead. The body is sown perishable; it is raised imperishable.
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
It is sown in dishonor; it is raised in glory. It is sown in weakness; it is raised in power.
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
It is sown a natural body; it is raised a spiritual body. There is a natural body and there is also a spiritual body.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
So also it is written, “The first man Adam became a living soul.” The last Adam became a life-giving spirit.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
However, that which is spiritual isn’t first, but that which is natural, then that which is spiritual.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man is of the earth, made of dust. The second man is the Lord from heaven.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
As is the one made of dust, such are those who are also made of dust; and as is the heavenly, such are they also that are heavenly.
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
As we have borne the image of those made of dust, let’s also bear the image of the heavenly.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
Now I say this, brothers, that flesh and blood can’t inherit God’s Kingdom; neither does the perishable inherit imperishable.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
Behold, I tell you a mystery. We will not all sleep, but we will all be changed,
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
in a moment, in the twinkling of an eye, at the last trumpet. For the trumpet will sound and the dead will be raised incorruptible, and we will be changed.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
For this perishable body must become imperishable, and this mortal must put on immortality.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
But when this perishable body will have become imperishable, and this mortal will have put on immortality, then what is written will happen: “Death is swallowed up in victory.”
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs g86)
“Death, where is your sting? Hades, where is your victory?” (Hadēs g86)
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
The sting of death is sin, and the power of sin is the law.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
But thanks be to God, who gives us the victory through our Lord Jesus Christ.
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
Therefore, my beloved brothers, be steadfast, immovable, always abounding in the Lord’s work, because you know that your labor is not in vain in the Lord.

< 1 Wakorintho 15 >