< 1 Wakorintho 15 >

1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
I make known now to you, brothers, the gospel that I evangelised to you, which also you received, in which also you have stood
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
through which also you are being saved, to the word I evangelised to you if you hold fast, unless only except in vain you have believed.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
I delivered for to you in [the] foremost what also I received that Christ died for the sins of us according to the Scriptures
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
and that He was buried and that He has been raised on the day the third according to the Scriptures
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
and that He appeared to Cephas, then to the Twelve.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
Thereafter He appeared to above five hundred brothers at once of whom the greater part remain until now, some however (and *k*) were fallen asleep.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
Then He appeared to James, then to the apostles all.
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
Last then of all as an untimely birth He appeared also to me. also to me.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
I myself for am the least of the apostles who not am fit to be called an apostle, because I persecuted the church of God;
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
By [the] grace however of God I am what I am, and the grace of Him toward me myself not void has been, Rather more excessive than them all I toiled, not I myself however, but the grace of God that [was] with me myself.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
Whether therefore I myself or they, thus we preach and thus you believed.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
If now Christ is preached that out from [the] dead He has been raised, how say among you some that a resurrection of [the] dead not there is?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
If however a resurrection of [the] dead not there is, neither Christ has been raised;
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
if then Christ not has been raised, [is] void then (also *no*) the preaching of us, void (now *k*) also the faith (of you. *NK(O)*)
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
We are found then also false witnesses of God, because we have witnessed concerning God that He raised up Christ whom not He has raised if indeed if indeed then [the] dead not are raised;
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
If for [the] dead not are raised, neither Christ has been raised;
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
if then Christ not has been raised, [is] futile the faith of you (is; *o*) still you are in the sins of you;
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
Then also those having fallen asleep in Christ have perished.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
If in life this in Christ already hoping we are only, more to be pitied than all men we are.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
Now however Christ has been raised out from [the] dead, firstfruit of those having fallen asleep (he became. *K*)
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
Since for through a man [came] (*k*) death also through a man resurrection of [the] dead.
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
For as indeed in Adam all die, so also in Christ all will be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
each however in the own order: [the] firstfruit Christ, then those of Christ at the coming of Him;
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
then the end, when (He may hand over *N(k)(o)*) the kingdom to the God and Father, when He may have annulled all dominion and all authority and power;
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
It behooves for Him to reign until that (when *k*) He may have put all the enemies under the feet of Him.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
[The] last enemy to be abolished [is] death.
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
All things for He has put in subjection under the feet of Him; When however it may be said that all things have been put in subjection, [it is] evident that [is] excepted the [One who] having put in subjection to Him all things;
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
When now shall have been subjected to Him all things, then also Himself the Son will be put in subjection to the [One] having put in subjection to Him all things, so that may be God all in all.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
Otherwise what will they do who are baptized for the dead? If at all [the] dead not are raised; why also are they baptized for (*k*) (them? *N(K)O*)
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
Why also we ourselves are in danger every hour?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
Every day I die, as surely as (in you *NK(O)*) boasting, (brothers *NO*) which I have in Christ Jesus the Lord of us.
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
If according to man I fought wild beasts in Ephesus, what to me the profit? If [the] dead not are raised, Let us eat and let us drink, tomorrow for we die.
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Not do be misled: Do corrupt morals good companionships bad.
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
do sober up righteously and not do sin; ignorance for of God some have; to [the] shame of you (I speak. *N(k)O*)
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
But will say someone; How are raised the dead? With what then body do they come?
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
Fool you yourself What you sow not does come to life only unless it may die;
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
And what you sow, not the body that will be you sow but a bare grain, if it would be of wheat or of some of the rest;
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
But God gives to it a body even as He has willed and to each of the seeds (*k*) [its] own body.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
Not all flesh [is] the same flesh but one indeed (flesh *k*) of men, another however flesh of beasts, another however (flesh *no*) of birds another however of fish.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
And bodies [there are] heavenly and bodies earthly; But one indeed [is] the of the heavenly glory, another however that of the earthly.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
One [is] [the] glory of [the] sun, and another [the] glory of [the] moon, and another [the] glory of [the] stars; star for from star differs in glory.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
So also [is] the resurrection of the dead. It is sown in decay, it is raised in immortality;
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
It is sown in dishonor, it is raised in glory; It is sown in weakness, it is raised in power;
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
It is sown a body natural, it is raised a body spiritual. (If *NO*) there is a body natural, there is also (body *k*) spiritual.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
So also it has been written: Became the first man Adam into a soul living; the last Adam into a spirit life-giving.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
However not first [was] the spiritual but the natural, then the spiritual.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man [was] from [the] earth made of dust, the second man ([is] the Lord *K*) from heaven.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
As the [one] made of dust, so also [are] those of the earth, and as the heavenly [one], so also those of heaven;
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
And even as we have born the image of the earthly, (we will bear *NK(o)*) also the image of the heavenly.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
This now I say, brothers, that flesh and blood [the] kingdom of God to inherit not (is able, *N(k)O*) nor the decay the immortality does inherit.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
Behold a mystery to you I tell; All (indeed *k*) not we will sleep, all however we will be changed —
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
in an instant in [the] twinkling of an eye at the last trumpet; [The] trumpet will sound for, and the dead will be raised imperishable, and we ourselves will be changed.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
It behooves for perishable this to put on imperishable and mortal this to put on immortality.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
When now perishable this may have put on [the] imperishable and mortal this may have put on (*o*) immortality, then will come to pass the word which written: Has been swallowed up death in victory.
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs g86)
Where of you, O death, the victory Where of you, (O Hades, *N(K)O*) the sting (Hadēs g86)
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
And the sting of death [is] sin, and the power of sin the law.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
however to God [be] thanks who is giving us the victory through the Lord of us Jesus Christ.
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
Therefore, brothers of mine beloved, steadfast do be, immovable, abounding in the work of the Lord always, knowing that the toil of you not is in vain in [the] Lord.

< 1 Wakorintho 15 >