< 1 Wakorintho 15 >
1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
Moreover, brethren, I declare anew to you the gospel which I preached to you, which also ye received, and wherein ye stand,
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
by which also ye are saved, if ye hold fast the same word which I preached to you, unless ye believed in vain.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
For I delivered to you first of all what I also received, that Christ died for our sins, according to the Scriptures;
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
and that he was buried, and that he hath risen on the third day, according to the Scriptures;
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
and that he appeared to Cephas, then to the twelve.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
After that, he appeared to more than five hundred brethren at once, of whom the greater part remain until now, but some have fallen asleep.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
After that, he appeared to James; then to all the apostles.
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
And last of all, as to one born out of due time, he appeared also to me.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, one not worthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am; and his grace which was bestowed upon me was not in vain, but I labored more abundantly than they all; yet not I, but the grace of God which was with me.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
Whether, then, it were I or they, thus we preach, and thus ye believed.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
But if Christ be preached that he hath risen from the dead, how is it that some among you say, that there is no resurrection of the dead?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
But if there be no resurrection of the dead, then Christ hath not risen;
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
and if Christ hath not risen, then is our preaching vain, and vain also is your faith.
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
And we are also found false witnesses concerning God; because we testified concerning God that he raised up Christ, whom he did not raise up, if so be that the dead rise not.
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
For if the dead rise not, then Christ hath not risen;
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
and if Christ hath not risen, your faith is vain; ye are yet in your sins;
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
then also they that have fallen asleep in Christ have perished.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
If in this life only we have hope in Christ, we are of all men most miserable.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
But now hath Christ risen from the dead, the first-fruits of them that have fallen asleep.
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
For since through man came death, through man came also the resurrection of the dead.
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
For as in Adam all die, so also in Christ will all be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
But every one in his own order; Christ the first-fruits, afterward they that are Christ's, at his coming.
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
Then will be the end, when he delivereth up the kingdom to God, the Father, when he shall have destroyed all dominion, and all authority, and power.
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
For he must reign, “till he hath put all enemies under his feet.”
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
The last enemy, death, will be destroyed;
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
for “he put all things under his feet.” But when it is said that all things have been put under him, it is manifest that he who put all things under him is excepted.
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
And when all things have been put under him, then will also the Son himself become subject to him that put all things under him, that God may be all in all.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
If it be not so, what are they doing, who are baptized for the dead? If the dead rise not at all, why are they then baptized for them?
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
Why also do we stand in peril every hour?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
I protest, brethren, by my glorying in you which I have in Christ Jesus our Lord, that I die daily.
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
If with the views of men I fought with wild beasts at Ephesus, what advantage is it to me? If the dead rise not, “let us eat and drink, for to-morrow we die.”
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Be not deceived; “evil communications corrupt good manners.”
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
Awake, as is your duty, and sin not; for some have not the knowledge of God; I say it to your shame.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
But some one will say, How are the dead to rise? and with what body do they come?
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
Fool! that which thou sowest is not brought to life unless it die;
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
and what thou sowest, not the body that shall be dost thou sow, but a bare grain, of wheat perhaps, or of some of the other grains;
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
but God giveth it a body, as he willed, and to every seed its own body.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
All flesh is not the same flesh; but there is one flesh of men, another of beasts, another of birds, another of fishes.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
There are also heavenly bodies, and earthly bodies; but the glory of the heavenly is one, and the glory of the earthly is another.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
There is one glory of the sun, and another glory of the moon, and another glory of the stars; for one star differeth from another star in glory.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
So also is the resurrection of the dead. It is sown in corruption, it is raised in incorruption;
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
it is sown in dishonor, it is raised in glory; it is sown in weakness, it is raised in power;
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
it is sown an animal body, it is raised a spiritual body. If there is an animal body, there is also a spiritual body.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
Thus is it also written: “The first man Adam became a living soul;” the last Adam a life-giving spirit.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
But the spiritual is not first, but the animal; and afterward the spiritual.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man is from the earth, earthy; the second man is from heaven.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
As was the earthy, such are they also that are earthy; and as is the heavenly, such are they also that are heavenly;
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
and as we bore the image of the earthy, we shall also bear the image of the heavenly.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
And this I say, brethren, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God, nor doth corruption inherit incorruption.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
Behold, I tell you a mystery. We shall not all sleep; but we shall all be changed,
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
in a moment, in the twinkling of an eye, at the last trump. For the trumpet will sound, and the dead will be raised incorruptible, and we shall be changed.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
For this corruptible must put on incorruption, and this mortal must put on immortality.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
So when this corruptible shall have put on incorruption, and this mortal shall have put on immortality, then will be brought to pass that which is written: “Death is swallowed up in victory.”
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs )
“Where, O death, is thy sting? Where, O death, is thy victory?” (Hadēs )
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
The sting of death is sin; and the strength of sin is the Law.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
But thanks be to God, who giveth us the victory, through our Lord Jesus Christ.
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
Therefore, my beloved brethren, be steadfast, immovable, always abounding in the work of the Lord, since ye know that your labor is not in vain in the Lord.