< 1 Wakorintho 15 >
1 Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
Now, brothers, I want to add information to the Gospel that I proclaimed to you, that you also received, and in which you stand;
2 Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
through which also you are saved, if you hold fast that word that I proclaimed to you—unless you believed in vain.
3 Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
Because I transmitted to you at first that which I also received: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
4 ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
and that He was buried, and that He was raised on the third day according to the Scriptures,
5 na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
and that He was seen by Cephas, then by the Twelve.
6 Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
After that He was seen by over five hundred brothers at once, most of whom are still living, while some have fallen asleep.
7 Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
After that He was seen by James, then by all the apostles.
8 Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
And last of all He was seen by me also, like one born out of season.
9 Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
For I am the least of the apostles, who am not worthy to be called an apostle, because I persecuted the Church of God.
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
But by the grace of God I am what I am, and His grace toward me has not been in vain; in fact, I have worked harder than all of them—well, not I, but the grace of God that was with me.
11 Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
So whether it was I or they, thus we preached and thus you believed.
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
Now if Christ is being proclaimed as having been raised from among the dead, how can some among you say that there is no resurrection of the dead?
13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
If there is no resurrection of the dead, not even Christ has been raised.
14 Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
And if Christ has not been raised, then our preaching is empty, and so is your faith!
15 Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
Further, we are even discovered to be false witnesses of God, because we have testified about God that He raised the Christ, whom He did not raise, if in fact the dead are not raised.
16 Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
For if no dead are raised, neither has Christ been raised.
17 Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
And if Christ has not been raised, your faith is useless; you are still in your sins.
18 Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
Then those also who have fallen asleep in Christ are lost.
19 Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
If it is only for this life that we have hoped in Christ, we are of all men most pitiable.
20 Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
But indeed, Christ has been raised from the dead; He became the firstfruits of those who have fallen asleep.
21 Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
For since death came through a man, resurrection of the dead also came through a man.
22 Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
For as all in Adam are dying, so also all in the Christ will be made alive.
23 Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
But each one in his own order: Christ the firstfruits, then those who belong to Christ at His coming;
24 Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
then the end, when He hands over the Kingdom to the God and Father, whenever He puts an end to every ruler and all authority and power.
25 Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
Because it is necessary that He reign until He has put all the enemies under His feet.
26 Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
The last enemy that will be destroyed is death.
27 Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
For “He has put all things under His feet.” But when it says that all things have been subordinated, it is obvious that He who put all things under Him is excepted.
28 Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
Now whenever all things have been subjected to Him, then the Son Himself will also be subjected to Him who subjected all things to Him, so that God may be all in all.
29 Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
Otherwise, what will they do who are being baptized in place of the dead? If the dead are not raised at all, just why are they being baptized in the place of the dead?
30 Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
And why do we face danger every hour?
31 Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
I die every day—so I affirm by the boasting about you that I have in Christ Jesus our Lord.
32 Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
If I fought human ‘animals’ in Ephesus, what did I gain? If the dead are not raised, “Let us eat and drink, for tomorrow we die!”
33 Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
Stop kidding yourselves: evil associations corrupt good habits.
34 Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
Sober up righteously, and stop sinning, for some have no knowledge of God. I say this to your shame.
35 Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
But someone will say, “How are the dead raised? With what kind of body do they come?”
36 Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
Ignorant, what you plant is not brought to life unless it dies.
37 Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
And what you plant is a bare seed (perhaps of wheat or some one of the others); you do not plant the body that it will become.
38 Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
But God gives it a body just as He determined, to each of the seeds its own body.
39 Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
All flesh is not the same flesh: that of humans is one kind, and the flesh of animals is another, that of fish is another, that of birds is yet another.
40 Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
There are also celestial bodies and terrestrial bodies; but the glory of the heavenly is one, while that of the earthly is another.
41 Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
There is one splendor of the sun, another splendor of the moon, and another splendor of the stars; and star differs from star in brightness.
42 Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
The resurrection of the dead is like that: the body is ‘planted’ in deterioration and it is raised in incorruptibility;
43 unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
it is ‘planted’ in dishonor and it is raised in glory; it is ‘planted’ in weakness and it is raised in power;
44 unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
it is ‘planted’ a natural body and it is raised a spiritual body. There is a natural body and there is a spiritual body.
45 Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
So also it is written: “The first man, Adam, became a living being”; the last Adam became a life-giving spirit.
46 Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
However, the spiritual is not first, but the natural, and then the spiritual.
47 Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
The first man was of the earth, of soil; the second man was the Lord from heaven.
48 Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
As was the earth-man, just so are the earth-people; and as was the heaven-man, just so are the heaven-people.
49 Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
And just as we have borne the image of the earth-man, we should also bear the image of the heaven-man.
50 Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
Now this I say, brothers, that flesh and blood cannot inherit the Kingdom of God; neither will deterioration inherit incorruptibility.
51 Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
And now, I tell you a mystery: we will not all sleep, but we will all be changed
52 ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
—in a split second, in an eye twinkle, at the last trumpet—the trumpet will blast and the dead will be raised incorruptible, and we will be changed.
53 Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
Because this corruptible must put on incorruption, and this mortal put on immortality.
54 Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
So whenever this corruptible puts on incorruption and this mortal puts on immortality, then this written word will happen: “Death has been swallowed down into victory.”
55 “Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs )
“Where, O Death, is your sting? Where, O Hades, is your victory?” (Hadēs )
56 Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
The stinger of death is sin, and the adjunct of sin is the law.
57 Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Now thanks be to God who gives us the victory through our Lord Jesus Christ!
58 Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.
So then, my dear brothers, be steadfast, immovable, always abounding in the work of the Lord, knowing that your labor is not in vain in the Lord.