< 1 Wakorintho 14 >

1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
SEGUID la caridad; y procurad los [dones] espirituales: mas sobre todo que profeticeis.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
Porque el que habla en lenguas, no habla á los hombres, sino á Dios; porque nadie le entiende, aunque en espíritu hable misterios.
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
Mas el que profetiza, habla á los hombres, [para] edificacion, y exhortacion, y consolacion.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
El que habla lengua [extraña, ] á sí mismo se edifica; mas el que profetiza, edifica á la iglesia.
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Así que quisiera que todos vosotros hablaseis lenguas; empero más [quisiera] que profetizaseis; porque mayor es el que profetiza que el que habla lenguas, si tambien no interpretare, para que la iglesia tome edificacion.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
Ahora pues, hermanos, si yo fuere á vosotros hablando lenguas, qué os aprovecharé, si no os hablare ó con revelacion, ó con ciencia, ó con profecía, ó con doctrina?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Ciertamente si las cosas inanimadas que hacen sonidos, como la flauta ó la vihuela, si no dieren distincion de voces, ¿cómo se sabrá lo que se tañe con la flauta, ó con la vihuela?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
Y si la trompeta diere sonido incierto, ¿quién se apercibirá á la batalla?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
Así tambien vosotros, si por la lengua no diereis palabra bien significante, ¿cómo se entenderá lo que se dice? porque hablaréis al aire.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
Tantos géneros de voces, (por ejemplo, ) hay en el mundo; y nada hay mudo;
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
Mas si [yo] ignorare el valor de la voz, seré bárbaro al que habla, y el que habla [será] bárbaro para mí.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Así tambien vosotros; pues que anhelais espirituales [dones, ] procurad ser excelentes para la edificacion de la iglesia.
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
Por lo cual el que habla lengua [extraña, ] pida que [la] interprete.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
Porque si yo orare en lengua [desconocida, ] mi espíritu ora; mas mi entendimiento es sin fruto.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
¿Qué pues? Oraré con el espíritu, mas oraré tambien con entendimiento: cantaré con el espíritu, mas cantaré tambien con entendimiento.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Porque si bendijeres con el espíritu, el que ocupa lugar de un mero particular, ¿cómo dirá Amen á tu accion de gracias? pues no sabe lo que has dicho.
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
Porque tú, á la verdad, bien haces gracias; mas el otro no es edificado.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
Doy gracias á Dios que hablo lenguas más que todos vosotros:
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
Pero en la iglesia [más] quiero hablar cinco palabras con mi sentido, para que enseñe tambien á los otros, que diez mil palabras en lengua [desconocida.]
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Hermanos, no seais niños en el sentido, sino sed niños en la malicia; empero perfectos en el sentido.
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
En la ley está escrito: En otras lenguas y en otros labios hablaré á este pueblo; y ni aun así me oirán, dice el Señor.
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
Así que las lenguas por señal son no á los fieles, sino á los infieles: mas la profecía no [se da] á los infieles, sino á los fieles.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
De manera que si toda la iglesia se juntare en uno y todos hablan lenguas, y entran indoctos, ó infieles, ¿no dirán que estais locos?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
Mas si todos profetizan, y entra algun infiel ó indocto, de todos es convencido, de todos es juzgado;
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
Lo oculto de su corazon se hace manifiesto: y así postrándose sobre el rostro, adorará á Dios, declarando que verdaderamente Dios está en vosotros.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
¿Qué hay, pues, hermanos? Cuando os juntais, cada uno de vosotros tiene salmo, tiene doctrina, tiene lengua, tiene revelacion, tiene interpretacion: hágase todo para edificacion.
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
Si hablare alguno en lengua [extraña, sea esto] por dos, ó á lo más tres, y por turno; mas uno interprete.
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
Y si no hubiere intérprete, calle en la iglesia; y hable á sí mismo, y á Dios.
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
Asimismo los profetas hablen dos ó tres, y los demás juzguen.
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
Y si á otro que estuviere sentado, fuere revelado, calle el primero.
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
Porque podeis todos profetizar uno por uno, para que todos aprendan, y todos sean exhortados.
32 Roho za manabii huwatii manabii.
Y los espíritus de los que profetizaren, sujétense á los profetas:
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
Porque Dios no es [Dios] de disension, sino de paz; como en todas las iglesias de los santos.
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
Vuestras mujeres callen en las congregaciones: porque no les es permitido hablar, sino que estén sujetas, como tambien la ley dice.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
Y si quieren aprender alguna cosa, pregunten en casa á sus maridos; porque deshonesta cosa es hablar una mujer en la congregacion.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
Qué ¿ha salido de vosotros la palabra de Dios? ó ¿á vosotros solos ha llegado?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
Si alguno, á su parecer, es profeta, o espiritual, reconozca lo que os escribo, porque son mandamientos del Señor.
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
Mas el que ignora, ignore.
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
Así que, hermanos procurad profetizar; y no impidais el hablar lenguas.
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
Empero hágase todo decentemente y con orden.

< 1 Wakorintho 14 >