< 1 Wakorintho 14 >
1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
Hrepenite za ljubeznijo, a trudite se za duhovne stvari, bolje pa, da prerokujete.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
Kajti kdor govori v jeziku, ne govori ljudém, nego Bogu, ker nikdor ne sluša; z duhom pa govori skrivnosti;
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
A kdor prerokuje ljudém, govori na zbujanje pobožnosti in na opominjanje in na tolažbo.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
Kajti kdor v jeziku govori, sam sebe zbuja na pobožnost, kdor pa prerokuje, cerkev zbuja na pobožnost.
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Hočem pa, da vsi govorite jezike, bolje pa, da prerokujete, kajti veči je, kdor prerokuje, nego kdor govori jezike, razen če razklada, da bi se cerkev zbudila na pobožnost.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
Sedaj pa, bratje, če pridem k vam jezike govoreč, kaj vam bom koristil, če vam ne bom govoril ali v razodetji, ali v znanji, ali v preroštvu, ali v nauku?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Kakor brezdušne stvari, ktere glas dajo, bodi si piščal, ali gosli, če razločka v glasovih ne dajo, kako se bo umelo, kaj se piska ali gode?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
Ker če nerazločen glas trobenta dá, kdo se bo pripravil za boj?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
Tako tudi vi, če z jezikom razumljive besede ne daste, kako se bo umelo, kaj pravite? kajti v zrak boste govorili.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
Toliko vrst glasov, postavim, je na svetu, in nobeden izmed njih ni brez znamenovanja.
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
Če torej ne vem moči glasa, mutec bom govorečemu in govoreči bo meni mutec.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Tako tudi vi, ko se trudite za duhovne darí, glejte, da boste za pobožno zbujevanje cerkve bogati.
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
Za to, kdor govori v jeziku, naj moli, da bi razkladal.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
Kajti če molim v jeziku, duh moj moli, a um moj je brez sada.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
Kaj torej? molil bom z duhom, a molil bom tudi z umom; prepeval bom z duhom, a prepeval bom tudi z umom.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Ker če blagosloviš z duhom, ta, kteri je nepodučen, kako poreče amen na tvoj blagoslov, ko ne ve, kaj govoriš?
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
Ti se, res da, dobro zahvaljuješ, ali drugi se ne zbuja na pobožnost.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
Zahvaljujem se svojemu Bogu, da bolje od vseh vas jezike govorim.
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
Toda v cerkvi rajši pet besed s svojim umom rečem, da tudi druge podučim, nego pa tisoč besed v jeziku.
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Bratje, ne bodite deca, nego v zlobi bodite deca, a v umu bodite popolni.
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
V postavi je pisano: "Z drugimi jeziki in z drugimi ustnicami bom govoril temu ljudstvu, in tudi tako me ne bodo poslušali, govori Gospod."
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
Tako so jeziki za znamenje ne tem, kteri verujejo, nego nevernim, in preroštvo ne nevernim, nego tem, kteri verujejo.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
Ko bi se torej sešla cerkev vsa na eno mesto, in bi vsi jezike govorili in vnišli bi tudi nepodučeni ali neverniki, je li ne porekó, da norite?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
Ko bi pa vsi prerokovali a vnišel bi kak nevernik ali nepodučen, ozmerjajo ga vsi, sodijo ga vsi.
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
In tako se skrivnosti njegovega srca razodevajo, in tako padši na obraz molil bo Boga oznanjujoč, da je Bog za res v vas.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Kaj je torej, bratje? Kedar se shajate, vsak vas ima psalm, ima nauk, jezik ima, razodetje ima, razkladanje ima: vse naj se zgodi na zbujevanje pobožnosti.
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
Če v jeziku kdo govori, naj govorita po dva ali k večemu po trije in eden za drugim, in eden naj razklada.
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
Ko bi pa ne bilo razkladalca, molči naj v cerkvi, a sebi naj govori in Bogu.
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
Preroka naj pa govorita dva ali trije, drugi naj pa razsojajo.
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
Če se pa drugemu, kteri sedí, kaj razodene, prvi naj molči.
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
Kajti morete eden po eden vsi prerokovati, da se vsi učé in vsi opominjajo.
32 Roho za manabii huwatii manabii.
In duhovi preroški podlagajo se prerokom.
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
Ker Bog ni Bog punta, nego in mira, kakor po vseh cerkvah svetniških.
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
Žene vaše naj v cerkvah molčé, kajti ni jim dopuščeno govoriti, nego podlagati se, kakor tudi postava pravi.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
A če se hočejo česa naučiti, doma naj svoje može prašajo; kajti grdo je ženam v cerkvi govoriti.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
Je li od vas beseda Božja izšla? je li k vam samim prišla?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
Če kdo misli, da je prerok ali duhoven, spozna naj, kar vam pišem, da so Gospodove zapovedi.
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
Če pa kdo ne vé, naj ne vé.
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
Tako, bratje, trudite se, da prerokujete in govoriti v jezikih nikar ne branite.
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
Vse naj se spodobno in po redu godi.