< 1 Wakorintho 14 >
1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
Recherchez la charité. Aspirez néanmoins aux dons spirituels, mais surtout à celui de prophétie.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
En effet, celui qui parle en langue ne parle pas aux hommes, mais à Dieu, car personne ne le comprend, et c’est en esprit qu’il dit des mystères.
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
Celui qui prophétise au contraire, parle aux hommes, les édifie, les exhorte, les console.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
Celui qui parle en langue s’édifie lui-même; celui qui prophétise édifie l’Église [de Dieu].
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Je désire que vous parliez tous en langues, mais encore plus que vous prophétisiez; car celui qui prophétise est plus grand que celui qui parle en langues, à moins que ce dernier n’interprète ce qu’il dit, pour que l’Église en reçoive de l’édification.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
Voyons, frères, de quelle utilité vous serais-je, si je venais à vous parlant en langues, et si je ne vous parle pas par révélation, ou par science, ou par prophétie, ou par doctrine?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Si les objets inanimés qui rendent un son, comme une flûte ou une harpe, ne rendent pas des sons distincts, comment connaîtra-t-on ce qui est joué sur la flûte ou sur la harpe?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
Et si la trompette rend un son confus, qui se préparera au combat?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
De même vous, si vous ne faites pas entendre avec la langue une parole distincte, comment saura-t-on ce que vous dites? Vous parlerez en l’air.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
Quelque nombreuses que puissent être dans le monde les diverses langues, il n’en est aucune qui consiste en sons inintelligibles.
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
Si donc j’ignore la valeur du son, je serai un barbare pour celui qui parle, et celui qui parle sera un barbare pour moi.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
De même vous aussi, puisque vous aspirez aux dons spirituels, que ce soit pour l’édification de l’Église que vous cherchiez à en avoir abondamment.
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
C’est pourquoi, que celui qui parle en langue prie pour obtenir le don d’interpréter.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
Car si je prie en langue, mon esprit est en prière, mais mon intelligence demeure sans fruit.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
Que faire donc? Je prierai avec l’esprit, mais je prierai aussi avec l’intelligence; je chanterai avec l’esprit, mais je chanterai aussi avec l’intelligence.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Autrement, si tu rends grâces avec l’esprit, comment celui qui est dans les rangs de l’homme du peuple répondra-t-il « Amen! » à ton action de grâces, puisqu’il ne sait pas ce que tu dis?
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
Ton hymne d’action de grâces est sans doute fort beau; mais lui n’en est pas édifié.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
Je rends grâces à [mon] Dieu de ce que je parle en langues plus que vous tous;
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
mais, dans l’Église, j’aime mieux dire cinq paroles avec mon intelligence, afin d’instruire aussi les autres, que dix mille paroles en langue.
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Frères, ne soyez pas des enfants sous le rapport du jugement; mais faites-vous enfants sous le rapport de la malice, et, pour le jugement, soyez des hommes faits.
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
Il est écrit dans la Loi: « C’est par des hommes d’une autre langue et par des lèvres étrangères que je parlerai à ce peuple, et même ainsi ils ne m’écouteront pas, dit le Seigneur. »
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
C’est donc que les langues sont un signe, non pour les croyants, mais pour les infidèles; la prophétie, au contraire, est un signe, non pour les infidèles, mais pour les croyants.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
Si donc, l’Église entière se trouvant réunie en assemblée, tous parlent en langues, et qu’il survienne des hommes non initiés ou des infidèles, ne diront-ils pas que vous êtes des fous?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
Mais si tous prophétisent, et qu’il survienne un infidèle ou un homme non initié, il est convaincu par tous, il est jugé par tous,
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
les secrets de son cœur sont dévoilés, de telle sorte que, tombant sur sa face, il adorera Dieu, et publiera que Dieu est vraiment au milieu de vous.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Que faire donc, mes frères? Lorsque vous vous assemblez, tel d’entre vous a un cantique, tel une instruction, tel une révélation, tel un discours en langue, tel une interprétation, que tout se passe de manière à édifier.
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
Si l’on parle en langue, que ce soient chaque fois deux ou trois au plus, chacun à son tour, et qu’il y ait un interprète;
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
s’il n’y a point d’interprète, qu’on se taise dans l’assemblée et qu’on se parle à soi-même et à Dieu.
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
Pour les prophètes, qu’il y en ait deux ou trois à parler, et que les autres jugent;
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
et si un autre, qui est assis, a une révélation, que le premier se taise.
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
Car vous pouvez tous prophétiser l’un après l’autre, afin que tous soient instruits et que tous soient exhortés.
32 Roho za manabii huwatii manabii.
Or les esprits des prophètes sont soumis aux prophètes,
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
car Dieu n’est pas un Dieu de désordre, mais de paix. Comme cela a eu lieu dans toutes les Églises des saints,
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
que vos femmes se taisent dans les assemblées, car elles n’ont pas mission de parler; mais qu’elles soient soumises, comme le dit aussi la Loi.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
Si elles veulent s’instruire sur quelque point, qu’elles interrogent leurs maris à la maison; car il est malséant à une femme de parler dans une assemblée.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
Est-ce de chez vous que la parole de Dieu est sortie? ou est-ce à vous seuls qu’elle est parvenue?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
Si quelqu’un croit être prophète ou riche en dons spirituels, qu’il reconnaisse que ces choses que je vous ai écrites sont des commandements du Seigneur.
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
Et s’il veut l’ignorer, qu’il l’ignore.
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
Ainsi donc, mes frères, aspirez au don de prophétie, et n’empêchez pas de parler en langue.
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
Mais que tout se fasse avec bienséance et avec ordre.