< 1 Wakorintho 14 >
1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
Follow after divine love; and seek the spiritual gifts, but rather that you may prophesy.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
For the one speaking with a tongue speaks not to men, but to God; for no one hears him; but he speaks mysteries in the spirit:
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
but the one prophesying speaks to men edification, exhortation, and comfort.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
The one speaking with a tongue edifies himself; but the one prophesying edifies the church.
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
But I wish you all to speak with tongues, but rather that you may prophesy: but greater is the one prophesying, than the one speaking with tongues, unless he may interpret, in order that the church may receive edification.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
But now, brethren, if I may come unto you speaking with tongues, what shall I profit you, unless I shall speak to you either in revelation, or knowledge, or prophecy, or in instruction?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Nevertheless things without life, giving forth a voice, whether pipe or harp, if it may not give a distinction to the sounds, how shall it be known what is piped, or what is harped?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
For if indeed the trumpet may give an uncertain sound, who will prepare himself for the war?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
Thus also if you through the tongue may give an indistinct word, how will that which is spoken be known? for you will be speaking into the air.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
If it so happens that there are so many kinds of voices in the world, and nothing without a voice;
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
if then I do not understand the power of the voice, I will be a barbarian to the one speaking, and the one speaking will be a barbarian to me.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
So also you, since you are zealots of spirits, seek that you may abound unto the edification of the church.
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
Therefore let the one speaking with a tongue, pray that one may interpret.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
For if I pray with a tongue, my spirit is praying, but my mind is not fruitful.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
Then what is it? I will pray with my spirit, and I will pray with my mind also: I will sing with my spirit, and I will sing with my mind also.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Since if you may bless with the spirit, how will one occupying the place of the unlearned say Amen to your blessing? since he does not know what you are saying.
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
For you indeed bless beautifully, but the other is not edified.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
I thank God, I speak with tongue more than you all:
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
but I would rather speak five words in the church with my understanding, so that I may indeed teach others, than ten thousand words in a tongue.
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Brethren, be not children in intellect: but be infants in evil, but be perfect in intellect.
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
It has been written in the law; I will speak to this people with other tongues and with the lips of others; and thus they will not hearken unto me, says the Lord.
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
So tongues are for a sign, not to those who believe, but to the unbelievers: and prophecy is not for the unbelievers, but for the believers.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
Then if the whole church may come together, and all may speak with tongues, and the unlearned or unbelievers may come in, will they not say that you are gone mad?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
But if all may prophesy, and some unbeliever or unlearned person may come in, he is convicted by all, he is discerned by all;
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
the secrets of his heart are made manifest; and thus falling upon his face he will worship God, proclaiming that God is truly in you.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
Then what is it, brethren? When you may come together, each one has a psalm, has a lesson, has a revelation, has a tongue, has an interpretation. Let all things be done to edification.
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
If one speaks with a tongue, let it he by twos, or at most by threes, and separately; and let one interpret;
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
but if there may be no interpreter, let him keep silent in the church; but let him speak to himself, and to God.
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
But let two or three prophets speak, and let the others give audience;
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
but if something may be revealed to another sitting down, let the first be silent.
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
For you are all able to prophesy one by one, in order that all may learn, and all may be comforted.
32 Roho za manabii huwatii manabii.
Truly the spirits of the prophets are subject to the prophets;
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
for he is not a God of confusion, but of peace. So in all the churches of the saints,
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
let the women be silent in the churches: for it is not permitted to them to talk; but let them be subordinate, as the law also says.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
But if they wish to learn something, let them ask their own husbands at home: for it is disgraceful for a woman to talk in church.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
Whether did the word of God come out from you? or has it reached unto you alone?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
If any one seems to be a prophet, or spiritual, let him understand the things which I write to you, that they are of the Lord;
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
but if any one ignores, he is ignored.
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
So, my brethren, be zealous to prophesy, and do not forbid to speak with tongues;
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
but let all things be done decently and in order.