< 1 Wakorintho 14 >

1 Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.
Pursue charity. Be zealous for spiritual things, but only so that you may prophesy.
2 Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.
For whoever speaks in tongues, speaks not to men, but to God. For no one understands. Yet by the Spirit, he speaks mysteries.
3 Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.
But whoever prophesies speaks to men for edification and exhortation and consolation.
4 Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.
Whoever speaks in tongues edifies himself. But whoever prophesies edifies the Church.
5 Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.
Now I want you all to speak in tongues, but more so to prophesy. For he who prophesies is greater than he who speaks in tongues, unless perhaps he interprets, so that the Church may receive edification.
6 Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?
But now, brothers, if I were to come to you speaking in tongues, how would it benefit you, unless instead I speak to you in revelation, or in knowledge, or in prophecy, or in doctrine?
7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?
Even those things that are without a soul can make sounds, whether it is a wind or a stringed instrument. But unless they present a distinction within the sounds, how will it be known which is from the pipe and which is from the string?
8 Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?
For example, if the trumpet made an uncertain sound, who would prepare himself for battle?
9 Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.
So it is with you also, for unless you utter with the tongue in plain speech, how will it be known what is said? For then you would be speaking into the air.
10 Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.
Consider that there are so many different kinds of languages in this world, and yet none is without a voice.
11 Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.
Therefore, if I do not understand the nature of the voice, then I shall be like a foreigner to the one with whom I am speaking; and he who is speaking will be like a foreigner to me.
12 Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.
So it is with you also. And since you are zealous for what is spiritual, seek the edification of the Church, so that you may abound.
13 Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.
For this reason, too, whoever speaks in tongues, let him pray for the interpretation.
14 Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.
So, if I pray in tongues, my spirit prays, but my mind is without fruit.
15 Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.
What is next? I should pray with the spirit, and also pray with the mind. I should sing psalms with the spirit, and also recite psalms with the mind.
16 Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?
Otherwise, if you have blessed only with the spirit, how can someone, in a state of ignorance, add an “Amen” to your blessing? For he does not know what you are saying.
17 Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.
In this case, certainly, you give thanks well, but the other person is not edified.
18 Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.
I thank my God that I speak in tongues for all of you.
19 Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.
But in the Church, I prefer to speak five words from my mind, so that I may instruct others also, rather than ten thousand words in tongues.
20 Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.
Brothers, do not choose to have the minds of children. Instead, be free of malice like infants, but be mature in your minds.
21 Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.
It is written in the law: “I will speak to this people with other tongues and other lips, and even so, they will not heed me, says the Lord.”
22 Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.
And so, tongues are a sign, not for believers, but for unbelievers; and prophecies are not for unbelievers, but for believers.
23 Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?
If then, the entire Church were to gather together as one, and if all were to speak in tongues, and then ignorant or unbelieving persons were to enter, would they not say that you were insane?
24 Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,
But if everyone prophesies, and one who is ignorant or unbelieving enters, he may be convinced by it all, because he understands it all.
25 nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”
The secrets of his heart are then made manifest. And so, falling to his face, he would adore God, proclaiming that God is truly among you.
26 Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.
What is next, brothers? When you gather together, each one of you may have a psalm, or a doctrine, or a revelation, or a language, or an interpretation, but let everything be done for edification.
27 Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.
If anyone is speaking in tongues, let there be only two, or at most three, and then in turn, and let someone interpret.
28 Lakini kama hakuna mtu wa kutafsiri, hao watu na wanyamaze kimya kanisani na wanene na nafsi zao wenyewe na Mungu.
But if there is no one to interpret, he should remain silent in the church, then he may speak when he is alone with God.
29 Manabii wawili au watatu wanene na wengine wapime yale yasemwayo.
And let the prophets speak, two or three, and let the others discern.
30 Kama mtu yeyote aliyeketi karibu, akipata ufunuo, basi yule wa kwanza na anyamaze.
But then, if something is revealed to another who is sitting, let the first one become silent.
31 Kwa maana wote mnaweza kutoa unabii, mmoja baada ya mwingine, ili kila mtu apate kufundishwa na kutiwa moyo.
For you are all able to prophesy one at a time, so that all may learn and all may be encouraged.
32 Roho za manabii huwatii manabii.
For the spirits of the prophets are subject to the prophets.
33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko bali ni Mungu wa amani. Kama ilivyo katika makusanyiko yote ya watakatifu,
And God is not of dissension, but of peace, just as I also teach in all the churches of the saints.
34 wanawake wanapaswa kuwa kimya kanisani. Hawaruhusiwi kusema, bali wanyenyekee kama sheria isemavyo.
Women should be silent in the churches. For it is not permitted for them to speak; but instead, they should be subordinate, as the law also says.
35 Kama wakitaka kuuliza kuhusu jambo lolote, wawaulize waume zao nyumbani. Kwa maana ni aibu kwa mwanamke kuzungumza kanisani.
And if they want to learn anything, let them ask their husbands at home. For it is disgraceful for a woman to speak in church.
36 Je, neno la Mungu lilianzia kwenu? Au ni ninyi tu ambao neno la Mungu limewafikia?
So now, did the Word of God proceed from you? Or was it sent to you alone?
37 Kama mtu yeyote akidhani kwamba yeye ni nabii, au ana karama za rohoni, basi na akubali kwamba haya ninayoandika ni maagizo kutoka kwa Bwana.
If anyone seems to be a prophet or a spiritual person, he should understand these things which I am writing to you, that these things are the commandments of the Lord.
38 Kama mtu akipuuza jambo hili yeye mwenyewe atapuuzwa.
If anyone does not recognize these things, he should not be recognized.
39 Kwa hiyo ndugu zangu, takeni sana kutoa unabii na msikataze watu kusema kwa lugha.
And so, brothers, be zealous to prophesy, and do not prohibit speaking in tongues.
40 Lakini kila kitu kitendeke kwa heshima na kwa utaratibu.
But let everything be done respectfully and according to proper order.

< 1 Wakorintho 14 >