< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
E quanto aos [dons] espirituais, irmãos, não quero que sejais ignorantes.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
Vós sabeis que éreis gentios, vós vos desviáveis para os ídolos mudos, conforme éreis guiados.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
Por isso eu vos deixo claro que ninguém que fala pelo Espírito de Deus chama a Jesus de maldito; e ninguém pode dizer [que] Jesus [é] o Senhor, a não ser pelo Espírito Santo.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
E há variedade de dons, mas o Espírito é o mesmo.
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
E há variedade de trabalhos [na Igreja], mas o Senhor é o mesmo.
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
E há variedade de operações, mas é o mesmo Deus que opera tudo em todos.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
Mas a cada um é dada a manifestação do Espírito, para o que for conveniente.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
Porque a um é dada, pelo Espírito, palavra de sabedoria; e a outro palavra de conhecimento, pelo mesmo Espírito.
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
e a outro fé pelo mesmo Espírito; e a outro dons de curas, pelo mesmo Espírito.
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
E a outro operações de milagres; e a outro profecia; e a outro o [dom de] discernir aos espíritos; e a outro variedade de línguas; e a outro interpretação de línguas.
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
Mas todas estas coisas [quem] opera [é] um e o mesmo Espírito, repartindo particularmente a cada um como quer.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
Porque assim como o corpo é um, e tem muitos membros, e todos os membros deste único corpo, sendo muitos, compõem um só corpo; assim também é Cristo.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
Porque também todos nós somos batizados em um [só] Espírito, para um [só] corpo, quer judeus, quer gregos, quer servos, quer livres; e para todos nós foi dado de beber um [só] Espírito.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
Porque também o corpo não é um [só] membro, mas muitos.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
Se o pé disser: Por eu não ser mão, não sou do corpo; Por isso, ele não é do corpo?
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
E se a orelha disser: Por eu não ser olho, não sou do corpo; Por isso, ela não é do corpo?
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
Se todo o corpo fosse olho, onde [estaria] o ouvido? Se [fosse] todo ouvido, onde [estaria] o olfato?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
Mas agora Deus pôs os membros no corpo, a cada qual deles como ele quis.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Porque se todos fossem um [só] membro, onde [estaria] o corpo?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
Mas há agora muitos membros, porém um [só] corpo.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
E o olho não pode dizer à mão: Não tenho necessidade de ti; Nem a cabeça aos pés: Não tenho necessidade de vós;
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
Antes até os membros do corpo que [nos] parecem ser os mais fracos, são muito mais necessários.
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
E os que pensamos serem os menos honrados do corpo, a esses muito mais honramos; e os nossos mais desprezíveis têm muito mais respeito.
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
Porém os nosso mais respeitáveis não têm [tanta] necessidade; mas [assim] Deus juntou o corpo, dando muito mais honra ao que tinha falta [dela].
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
Para que não haja divisão no corpo, mas que os membros tenham igual cuidado uns com os outros.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
E seja que, [caso] um membro sofra, [também] os membros sofrem juntos; e [caso] um membro seja honrado, todos os membros se alegram juntos.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
E vós sois o corpo de Cristo, e membros em particular.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
E Deus pôs a uns na Igreja: em primeiro lugar apóstolos, em segundo profetas, em terceiro mestres; depois milagres, dons de curas, socorros, lideranças, variedades de línguas.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
Por acaso são todos apóstolos? São todos profetas? São todos mestres? São todos com dons de milagres?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
Tem todos dons de curas? Falam todos [várias] línguas? Interpretam todos?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
Porém desejai com zelo pelos melhores dons; e eu vos mostro um caminho ainda mais excelente.