< 1 Wakorintho 12 >

1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
Now, concerning spiritual gifts, brethren, I would not have you ignorant.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
You know that you were Gentiles, led away to dumb idols, even as you happened to be led.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
Wherefore, I inform you, that no one, speaking by the Spirit of God, pronounces Jesus accursed; and, that no one can declare Jesus Lord, except by the Holy Spirit.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
Now, there are diversities of gifts, but the same spirit.
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
And there are diversities of ministries, but the same Lord.
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
And there are diversities of operations, but the same God, who works all in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
And to each is given this manifestation of the Spirit, for the advantage of all.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
For to one, indeed, is given, by the Spirit, the word of wisdom: and to another, the word of knowledge, according to the same Spirit.
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
And to another, faith, by the same Spirit: and to another, healing, by the same Spirit:
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
and to another, the operations of powers: and to another, prophecy: and to another, diverse kinds of foreign tongues: and to another, the interpretation of foreign tongues.
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
Now, all these does the one and the same Spirit effectively work; distributing to each, respectively, as he pleases.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
For, as the body is one, although it have many members; and all the members of that one body, being many, are one body, so also is Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
For, indeed, by one Spirit, we all have been immersed into one body; whether Jews or Greeks, whether slaves or freemen; and all have been made to drink of one Spirit.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
Since, then, the body is not one member, but many;
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
if the foot shall say, Because I am not the hand, I am not of the body; is it, for this, not of the body?
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
And if the ear shall say, Because I am not the eye, I am not of the body; is it, for this, not of the body?
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
If the whole body were an eye, where were the hearing? If the whole were hearing, where were the smelling?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
But, now, God has placed the members, every one of them, in the body, as he has pleased.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Besides, if all were one member, where were the body?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
But now, indeed, there are many members, but one body.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
Therefore, the eye can not say to the hand, I have no need of you: nor, again, the head to the feet, I have no need of you.
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
Nay, those members of the body which seem to be more feeble, are necessary.
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
And those which we think are less honorable members of the body, around them we throw more abundant honor; and so our uncomely members have more abundant comeliness.
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
But, our comely members have no need. However, God has tempered the body together; having given to the member which wants it, more abundant honor.
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
That there may be no schism in the body; but, that the members may have the very same anxious care, one for another.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
So, whether one member suffer, all the members sympathize; or, one member be honored, all the members rejoice together.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
Now, you are Christ's body, and members in particular.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
And these, indeed, God has placed in the congregation: first, Apostles; secondly, prophets; thirdly, teachers; next, powers; then, gifts of healing; helpers, directors, kinds of foreign languages.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
Are all Apostles? are all prophets? are all teachers? have all powers?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
have all the gift of healing? do all speak in foreign languages? do all interpret?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
Now, ardently desire the best gifts; and yet I show you a more excellent way.

< 1 Wakorintho 12 >