< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
And concerning the spiritual things, brothers, I do not wish you to be ignorant;
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
you have known that you were nations, being carried away as you were led to the mute idols;
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
for this reason, I give you to understand that no one, speaking in the Spirit of God, says Jesus [is] accursed, and no one is able to say Jesus [is] LORD, except in the Holy Spirit.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
And there are diversities of gifts, and the same Spirit;
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
and there are diversities of ministries, and the same Lord;
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
and there are diversities of workings, and it is the same God—who is working all in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
And to each has been given the manifestation of the Spirit for profit;
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
for to one through the Spirit has been given a word of wisdom, and to another a word of knowledge, according to the same Spirit;
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
and to another faith in the same Spirit, and to another gifts of healings in the same Spirit;
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
and to another in-workings of mighty deeds; and to another prophecy; and to another discernings of spirits; and to another [various] kinds of tongues; and to another interpretation of tongues:
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
and the one and the same Spirit works all these, dividing to each individually as He intends.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
For even as the body is one, and has many members, and all the members of the one body, being many, are one body, so also [is] the Christ,
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
for also in one Spirit we were all immersed into one body, whether Jews or Greeks, whether servants or freemen, and all were made to drink one Spirit,
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
for also the body is not one member, but many.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
If the foot may say, “Because I am not a hand, I am not of the body,” is it not, because of this, not of the body?
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
And if the ear may say, “Because I am not an eye, I am not of the body,” is it not, because of this, not of the body?
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
If the whole body [were] an eye, where the hearing? If the whole hearing, where the smelling?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
And now, God set the members, each one of them in the body, according as He willed,
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
and if all were one member, where [is] the body?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
And now, indeed, [are] many members, but one body;
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
and an eye is not able to say to the hand, “I have no need of you”; nor again the head to the feet, “I have no need of you.”
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
But much more the members of the body seeming to be weaker are necessary,
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
and those that we think to be less honorable of the body, around these we put more abundant honor, and our unseemly things have more abundant seemliness,
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
and our seemly things have no need; but God tempered the body together, having given more abundant honor to the lacking part,
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
that there may be no division in the body, but that the members may have the same anxiety for one another,
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
and whether one member suffers, all the members suffer with [it], or one member is glorified, all the members rejoice with [it];
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
and you are the body of Christ, and members in particular.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
And some, indeed, God set in the Assembly: first apostles, secondly prophets, thirdly teachers, afterward powers, afterward gifts of healings, helpings, governings, various kinds of tongues.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
[Are] all apostles? [Are] all prophets? [Are] all teachers? [Are] all powers?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
[Do] all have gifts of healings? Do all speak with tongues? Do all interpret?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
And earnestly desire the better gifts; and yet I show to you a far [more] excelling way: