< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
Now concerning spiritual gifts, brethren, I would not have you ignorant.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
Ye know that ye were Gentiles, carried away unto these dumb idols, even as ye were led.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
Wherefore I give you to understand, that no man speaking by the Spirit of God calleth Jesus accursed: and that no man can say that Jesus is the Lord, but by the Holy Ghost.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
Now there are diversities of gifts, but the same Spirit.
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
And there are differences of ministries, but the same Lord.
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
And there are diversities of operations, but it is the same God which worketh all in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
But the manifestation of the Spirit is given to every man to profit withal.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
For to one is given by the Spirit the word of wisdom; to another the word of knowledge by the same Spirit;
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
To another faith by the same Spirit; to another the gifts of healing by the same Spirit;
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
To another the working of miracles; to another prophecy; to another discerning of spirits; to another divers kinds of tongues; to another the interpretation of tongues:
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
But all these worketh that one and the selfsame Spirit, dividing to every man severally as he will.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
For as the body is one, and hath many members, and all the members of that one body, being many, are one body: so also is Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
For by one Spirit are we all baptized into one body, whether we be Jews or Gentiles, whether we be bond or free; and have been all made to drink into one Spirit.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
For the body is not one member, but many.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
If the foot shall say, Because I am not the hand, I am not of the body; is it therefore not of the body?
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
And if the ear shall say, Because I am not the eye, I am not of the body; is it therefore not of the body?
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
If the whole body were an eye, where were the hearing? If the whole were hearing, where were the smelling?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
But now hath God set the members every one of them in the body, as it hath pleased him.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
And if they were all one member, where were the body?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
But now are they many members, yet but one body.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
And the eye cannot say unto the hand, I have no need of thee: nor again the head to the feet, I have no need of you.
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
Nay, much more those members of the body, which seem to be more feeble, are necessary:
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
And those members of the body, which we think to be less honourable, upon these we bestow more abundant honour; and our uncomely parts have more abundant comeliness.
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
For our comely parts have no need: but God hath tempered the body together, having given more abundant honour to that part which lacked:
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
That there should be no schism in the body; but that the members should have the same care one for another.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
And whether one member suffer, all the members suffer with it; or one member be honoured, all the members rejoice with it.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
Now ye are the body of Christ, and members in particular.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
And God hath set some in the Assembly, first apostles, secondarily prophets, thirdly teachers, after that miracles, then gifts of healings, helps, governments, diversities of tongues.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
Are all apostles? are all prophets? are all teachers? are all workers of miracles?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
Have all the gifts of healing? do all speak with tongues? do all interpret?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
But covet earnestly the best gifts: and yet shew I unto you a more excellent way.