< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
But concerning spiritual [manifestations], brethren, I do not wish you to be ignorant.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
Ye know that when ye were [of the] nations [ye were] led away to dumb idols, in whatever way ye might be led.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
I give you therefore to know, that no one, speaking in [the power of the] Spirit of God, says, Curse [on] Jesus; and no one can say, Lord Jesus, unless in [the power of the] Holy Spirit.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
But there are distinctions of gifts, but the same Spirit;
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
and there are distinctions of services, and the same Lord;
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
and there are distinctions of operations, but the same God who operates all things in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
But to each the manifestation of the Spirit is given for profit.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
For to one, by the Spirit, is given [the] word of wisdom; and to another [the] word of knowledge, according to the same Spirit;
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
and to a different one faith, in [the power of] the same Spirit; and to another gifts of healing in [the power of] the same Spirit;
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
and to another operations of miracles; and to another prophecy; and to another discerning of spirits; and to a different one kinds of tongues; and to another interpretation of tongues.
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
But all these things operates the one and the same Spirit, dividing to each in particular according as he pleases.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
For even as the body is one and has many members, but all the members of the body, being many, are one body, so also [is] the Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
For also in [the power of] one Spirit we have all been baptised into one body, whether Jews or Greeks, whether bondmen or free, and have all been given to drink of one Spirit.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
For also the body is not one member but many.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
If the foot say, Because I am not a hand I am not of the body, is it on account of this not indeed of the body?
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
And if the ear say, Because I am not an eye I am not of the body, is it on account of this not indeed of the body?
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
If the whole body [were] an eye, where the hearing? if all hearing, where the smelling?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
But now God has set the members, each one of them in the body, according as it has pleased [him].
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
But if all were one member, where the body?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
But now the members [are] many, and the body one.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
The eye cannot say to the hand, I have not need of thee; or again, the head to the feet, I have not need of you.
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
But much rather, the members of the body which seem to be weaker are necessary;
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
and those [parts] of the body which we esteem to be the more void of honour, these we clothe with more abundant honour; and our uncomely [parts] have more abundant comeliness;
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
but our comely [parts] have not need. But God has tempered the body together, having given more abundant honour to [the part] that lacked;
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
that there might be no division in the body, but that the members might have the same concern one for another.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
And if one member suffer, all the members suffer with [it]; and if one member be glorified, all the members rejoice with [it].
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
Now ye are Christ's body, and members in particular.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
And God has set certain in the assembly: first, apostles; secondly, prophets; thirdly, teachers; then miraculous powers; then gifts of healings; helps; governments; kinds of tongues.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
[Are] all apostles? [are] all prophets? [are] all teachers? [are] all [in possession of] miraculous powers?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
have all gifts of healings? do all speak with tongues? do all interpret?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
But desire earnestly the greater gifts, and yet shew I unto you a way of more surpassing excellence.