< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
But about the things of the spirit, my brothers, it is not right for you to be without teaching.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
You are conscious that when you were Gentiles, in whatever way you were guided, you went after images without voice or power.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
So it is my desire for you to be clear about this; that no one is able to say by the Spirit of God that Jesus is cursed; and no one is able to say that Jesus is Lord, but by the Holy Spirit.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
Now there are different qualities given to men, but the same Spirit.
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
And there are different sorts of servants, but the same Lord.
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
And there are different operations, but the same God, who is working all things in all.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
But to every man some form of the Spirit's working is given for the common good.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
For to one are given words of wisdom through the Spirit; and to another words of knowledge through the same Spirit:
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
To another faith in the same Spirit; and to another the power of taking away disease, by the one Spirit;
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
And to another the power of working wonders; and to another the prophet's word; and to another the power of testing spirits; to another different sorts of tongues; and to another the power of making clear the sense of the tongues:
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
But all these are the operations of the one and the same Spirit, giving to every man separately as his pleasure is.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
For as the body is one, and has a number of parts, and all the parts make one body, so is Christ.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
For through the baptism of the one Spirit we were all formed into one body, Jews or Greeks, servants or free men, and were all made full of the same Spirit.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
For the body is not one part, but a number of parts.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
If the foot says, Because I am not the hand, I am not a part of the body; it is no less a part of the body.
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
And if the ear says, Because I am not the eye, I am not a part of the body; it is a part of the body all the same.
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
If all the body was an eye, where would be the hearing? if all was hearing, where would be the smelling?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
But now God has put every one of the parts in the body as it was pleasing to him.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
And if they were all one part, where would the body be?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
But now they are all different parts, but one body.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
And the eye may not say to the hand, I have no need of you: or again the head to the feet, I have no need of you.
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
No, those parts which seem to be feeble are the more necessary;
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
And to those parts of the body which seem to have less honour we give all the more honour; and to those parts of the body which are a cause of shame to us we give the greater respect;
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
But those parts of the body which are beautiful have no need of such care: and so the body has been joined together by God in such a way as to give more honour to those parts which had need of it;
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
So that there might be no division in the body; but all the parts might have the same care for one another.
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
And if there is pain in one part of the body, all the parts will be feeling it; or if one part is honoured, all the parts will be glad.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
Now you are the body of Christ, and every one of you the separate parts of it.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
And God has put some in the church, first, Apostles; second, prophets; third, teachers; then those with wonder-working powers, then those with the power of taking away disease, helpers, wise guides, users of strange tongues.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
Are all Apostles? are all prophets? are all teachers? have all the power of working wonders?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
Are all able to take away disease? have all the power of tongues? are all able to give their sense?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
But let your desires be turned to the more important things given by the Spirit. And now I am pointing out to you an even better way.