< 1 Wakorintho 12 >
1 Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
Men hvad de aandelige Gaver angaar, Brødre! vil jeg ikke, at I skulle være uvidende.
2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
I vide, at da I vare Hedninger, droges I hen til de stumme Afguder, som man drog eder.
3 Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
Derfor kundgør jeg eder, at ingen, som taler ved Guds Aand, siger: „Jesus er en Forbandelse,” og ingen kan sige: „Jesus er Herre” uden ved den Helligaand.
4 Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
Der er Forskel paa Naadegaver, men det er den samme Aand;
5 Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
og der er Forskel paa Tjenester, og det er den samme Herre;
6 Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
og der er Forskel paa kraftige Gerninger, men det er den samme Gud, som virker alt i alle.
7 Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
Men til enhver gives Aandens Aabenbarelse til det, som er gavnligt.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
En gives der nemlig ved Aanden Visdoms Tale; en anden Kundskabs Tale ifølge den samme Aand;
9 Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
en anden Tro i den samme Aand; en anden Gaver til at helbrede i den ene Aand;
10 Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
en anden at udføre kraftige Gerninger; en anden profetisk Gave; en anden at bedømme Aander; en anden forskellige Slags Tungetale; en anden Udlægning af Tungetale.
11 Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
Men alt dette virker den ene og samme Aand, som uddeler til enhver især, efter som han vil.
12 Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
Thi ligesom Legemet er eet og har mange Lemmer, men alle Legemets Lemmer, skønt de ere mange, dog ere eet Legeme, saaledes ogsaa Kristus.
13 Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
Thi med een Aand bleve vi jo alle døbte til at være eet Legeme, hvad enten vi ere Jøder eller Grækere, Trælle eller frie; og alle fik vi een Aand at drikke.
14 Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
Legemet er jo heller ikke eet Lem, men mange.
15 Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
Dersom Foden vilde sige: „Fordi jeg ikke er Haand, hører jeg ikke til Legemet,” saa ophører den dog ikke derfor at høre til Legemet.
16 Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
Og dersom Øret vilde sige: „Fordi jeg ikke er Øje, hører jeg ikke til Legemet,” saa ophører det dog ikke derfor at høre til Legemet.
17 Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
Dersom hele Legemet var Øje, hvor blev da Hørelsen? Dersom det helt var Hørelse, hvor blev da Lugten?
18 Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
Men nu har Gud sat Lemmerne, ethvert af dem, paa Legemet, efter som han vilde.
19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
Men dersom de alle vare eet Lem, hvor blev da Legemet?
20 Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
Nu er der derimod mange Lemmer og dog kun eet Legeme.
21 Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
Øjet kan ikke sige til Haanden: „Jeg har dig ikke nødig,” eller atter Hovedet til Fødderne: „Jeg har eder ikke nødig.”
22 Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
Nej, langt snarere ere de Lemmer paa Legemet nødvendige, som synes at være de svageste,
23 Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
og de, som synes os mindre ærefulde paa Legemet, dem klæde vi med des mere Ære; og de Lemmer, vi blues ved, omgives med desto større Blufærdighed;
24 wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
de derimod, som vi ikke blues ved, have det ikke nødig. Men Gud har sammenføjet Legemet saaledes, at han tillagde det ringere mere Ære;
25 ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
for at der ikke skal være Splid i Legemet, men for at Lemmerne skulle have samme Omsorg for hverandre;
26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
og hvad enten eet Lem lider, lide alle Lemmerne med, eller eet Lem bliver hædret, glæde alle Lemmerne sig med.
27 Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
Men I ere Kristi Legeme, og Lemmer enhver især.
28 Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
Og nogle satte Gud i Menigheden for det første til Apostle, for det andet til Profeter, for det tredje til Lærere, dernæst kraftige Gerninger, dernæst Gaver til at helbrede, til at hjælpe, til at styre, og forskellige Slags Tungetale.
29 Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
Mon alle ere Apostle? mon alle ere Profeter? mon alle ere Lærere? mon alle gøre kraftige Gerninger?
30 Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
mon alle have Gaver til at helbrede? mon alle tale i Tunger? mon alle udlægge?
31 Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.
Men tragter efter de største Naadegaver! Og ydermere viser jeg eder en ypperlig Vej.