< 1 Wakorintho 11 >
1 Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
Be ye then imitators of me, as I also am of Christ.
2 Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
Now I commend you, brethren, that ye remember me in all things, and keep the ordinances, as I delivered them to you.
3 Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
But I would have you know that Christ is the head of every man; and the head of the woman is the man; and the head of Christ is God.
4 Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
Every man praying or prophesying, having a veil on his head, dishonoureth Him who is his head.
5 Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
But every woman praying or prophesying with her head unveiled dishonoureth man her head; for it is even all one as if she were shaved.
6 Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
For if a woman be not covered, she may as well be shorn: but if it be shameful to a woman to be shorn or shaved, let her be covered.
7 Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
For a man indeed ought not to have his head covered, he being the image and glory of God: but the woman is the glory of the man.
8 Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
For the man was not of the woman; but the woman was taken out of the man:
9 Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
nor was the man created for the sake of the woman, but the woman for the man.
10 Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
For this reason ought the woman to have power on her head, because of the angels.
11 Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
Nevertheless, neither is the man without the woman, nor the woman without the man, in the Lord.
12 Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
For as the woman was originally from the man, so also is the man by the woman: but all things are from God.
13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
Judge in yourselves, Is it decent for a woman to pray to God uncovered?
14 Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
Doth not even nature itself teach you, that if a man have long hair, it is a disgrace to him?
15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
but if a woman have long hair it is a glory to her; because the hair was given her as for a veil.
16 Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
But if any one is pleased to contend for the contrary, I answer, We have no such custom, nor any of the churches of God.
17 Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
But whilst I am declaring this, I do not commend you, that ye assemble together not for the better, but for the worse.
18 Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
For first when ye come together in the church, I hear there are divisions among you, and I partly believe it.
19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
For there must be even heresies among you, that they who are approved may be made manifest among you.
20 Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
When therefore ye thus assemble together, this is not eating the Lord's supper:
21 kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
for in eating every one takes his own supper first; and one is hungry, and another is glutted.
22 Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
What! have ye not houses to eat and to drink in? or do ye despise the church of God, and shame those that have not? What shall I say to you? shall I praise you in this? I praise you not.
23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
For I received from the Lord, that which I also delivered unto you, that the Lord Jesus the same night in which He was betrayed took bread:
24 naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
and gave thanks, and brake it, and said, "Take and eat; this is my body, which is going to be broken for you: this do in remembrance of me."
25 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
And in the same manner He took the cup, after supper, saying, "This cup is the new covenant ratified in my blood: this do, as often as ye drink of it, in remembrance of me."
26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
As often then as ye eat of this bread, and drink of this cup, ye commemorate the Lord's death till he come.
27 Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
So that whosoever eateth this bread, or drinketh of the cup of the Lord unworthily, shall be guilty of profaning the body and blood of the Lord.
28 Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
But let a man examine himself, and so let him eat of this bread and drink of this cup:
29 Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
for he that eateth and drinketh unworthily, eateth and drinketh judgement against himself, not distinguishing the Lord's body.
30 Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
For this many among you are weak and infirm, and several are fallen asleep.
31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
If then we would judge ourselves, we should not be judged:
32 Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
but when judged, we are chastened by the Lord, that we may not be condemned with the world.
33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
Wherefore, my brethren, when ye come together to eat, wait for one another:
34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.
and if any one be hungry, let him eat at home, that ye may not come together to your condemnation. And as to other things, I will set them in order when I come.