< 1 Wakorintho 11 >

1 Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
Be ye followers of me, even as I also [am] of Christ.
2 Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
Now I praise you, brethren, that ye remember me in all things, and keep the ordinances, as I delivered [them] to you.
3 Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
But I would have you know, that the head of every man is Christ; and the head of the woman [is] the man; and the head of Christ [is] God.
4 Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
Every man praying or prophesying, having [his] head covered, dishonoreth his head.
5 Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
But every woman that prayeth or prophesieth with [her] head uncovered, dishonoreth her head: for that is even all one as if she were shaved.
6 Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
For if the woman is not covered, let her also be shorn: but if it is a shame for a woman to be shorn or shaved, let her be covered.
7 Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
For a man indeed ought not to cover [his] head, forasmuch as he is the image and glory of God: but the woman is the glory of the man.
8 Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
For the man is not from the woman, but the woman from the man.
9 Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
Neither was the man created for the woman, but the woman for the man.
10 Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
For this cause ought the woman to have power on [her] head, because of the angels.
11 Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
Nevertheless, neither is the man without the woman, neither the woman without the man in the Lord.
12 Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
For as the woman [is] from the man, even so [is] the man also by the woman; but all things from God.
13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
Judge in yourselves: Is it comely that a woman should pray to God uncovered?
14 Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
Doth not even nature itself teach you, that if a man hath long hair, it is a shame to him?
15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
But if a woman hath long hair, it is a glory to her: for [her] hair is given her for a covering.
16 Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
But if any man seemeth to be contentious, we have no such custom, neither the churches of God.
17 Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
Now in this that I declare [to you], I praise [you] not, that ye come together not for the better, but for the worse.
18 Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
For first of all, when ye come together in the church, I hear that there are divisions among you; and I partly believe it.
19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
For there must be also heresies among you, that they who are approved may be made manifest among you.
20 Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
When therefore ye come together in one place, [this] is not to eat the Lord's supper.
21 kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
For in eating every one taketh before [another] his own supper: and one is hungry, and another is drunken.
22 Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
What? have ye not houses to eat and to drink in? or despise ye the church of God, and shame them that have not? What shall I say to you? shall I praise you in this? I praise [you] not.
23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
For I have received from the Lord, that which also I delivered to you, That the Lord Jesus, the [same] night in which he was betrayed, took bread:
24 naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
And when he had given thanks, he broke [it], and said, Take, eat: this is my body, which is broken for you: this do in remembrance of me.
25 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
After the same manner also [he took] the cup, when he had supped, saying, This cup is the new testament in my blood: this do ye, as often as ye drink [it], in remembrance of me.
26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
For as often as ye eat this bread, and drink this cup, ye do show the Lord's death till he shall come.
27 Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
Wherefore, whoever shall eat this bread, and drink [this] cup of the Lord unworthily, shall be guilty of the body and blood of the Lord.
28 Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
But let a man examine himself, and so let him eat of [that] bread, and drink of [that] cup.
29 Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
For he that eateth and drinketh unworthily, eateth and drinketh condemnation to himself, not discerning the Lord's body.
30 Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
For this cause many [are] weak and sickly among you, and many sleep.
31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
For if we would judge ourselves, we should not be judged.
32 Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
But when we are judged, we are chastened by the Lord, that we should not be condemned with the world.
33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
Wherefore, my brethren, when ye come together to eat, tarry one for another.
34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.
And if any man hungereth, let him eat at home; that ye come not together to condemnation. And the rest will I set in order when I come.

< 1 Wakorintho 11 >