< 1 Wakorintho 11 >

1 Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
Be imitators of me, as I am an imitator of Christ.
2 Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
Indeed I praise you for remembering me in everything, and because you are holding fast to the traditions just as you received them.
3 Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
But I wish you to understand that the head of every man is Christ, and of a wife her husband is head; and that God is head of Christ.
4 Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
Every man who prays or prophesies with head veiled dishonors his Head;
5 Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
but every woman who prays or prophesies with her head unveiled dishonors her head (her husband). for it is one and the same thing as if she were shaven.
6 Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
If a woman does not wear a veil, let her also cut off her hair; now if it is a disgrace for a woman to have her hair cut off or her head shaved, let her be veiled.
7 Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
A man, indeed, ought not to have his head veiled, for he is an image and glory of God; but woman is a glory of man.
8 Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
For it is not man who was made from woman, but woman was made from man.
9 Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
And man was not created for woman, but woman for man.
10 Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
For this reason the woman ought to have authority over her head, because of her guardian angels.
11 Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
However, in the Lord neither is woman independent of man, nor is man independent of woman;
12 Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
for just as the woman was made from the man, so also is the man born of the woman, while they both come from God.
13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
Judge of this for your own selves. It is fitting that a woman should pray to God with her head unveiled.
14 Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
Nor does nature itself teach you that it is a disgrace to a man to have long hair,
15 Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
but it is woman’s glory, because her hair has been given her instead of a veil.
16 Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
If, however, any one is inclined to be disputatious regarding such a custom, let him know that neither I nor the churches of God hold to such a custom.
17 Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
But in giving you the following instructions, I cannot praise you; your solemn assemblies do more harm than good.
18 Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
To begin with, I am told - and I believe there is some truth in it - that when you meet at a church there are divisions among you.
19 Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
For there must needs be also parties among you, in order that the good may be tested and made known.
20 Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
Again, when you meet together, there is no true eating of the Lord’s Supper;
21 kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
for each one of you begins to eat his own supper; one goes hungry, while another gets drunk.
22 Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
What! Have you no houses in which to eat or drink? or do you wish to show your contempt for the church of God, and to shame those who have no homes to eat in? What shall I say to you? Shall I praise you? In this I certainly do not praise you.
23 Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
For I passed on to you the account, which I myself received from the Lord; how the Lord Jesus, on the very night he was betrayed, took bread,
24 naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
and when he had given thanks, he broke it, saying, "This is my body, broken for you; this do in memory of me."
25 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
In the same way also, he took the cup after supper, saying. "This cup is the new covenant in my blood; do this, whenever you drink it, in memory of me."
26 Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
For as often as you eat this bread and drink this cup, you are proclaiming your Lord’s death until he come.
27 Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
So he that eats the bread or drinks the cup of the Lord unworthy must answer for a sin against the body and blood of the Lord.
28 Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
Let each man scrutinize himself, and thus let him eat of the bread and drink of the cup.
29 Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
For whoever eats and drinks without discerning the body, eats and drinks condemnation to himself.
30 Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
This is why many among you are feeble and sickly, and many sleep.
31 Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
If however, we were judging ourselves aright, we should not now be condemned;
32 Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
but through our condemnation by the Lord, we are trained so that we may not be condemned;
33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
So, my brothers, whenever you come together for this meal, wait for one another.
34 Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.
If any one is hungry, let him eat at home, so that your meetings do not bring condemnation upon you. The other matters I will adjust when I come.

< 1 Wakorintho 11 >