< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
Car je ne veux pas que vous ignoriez, frères, que nos pères ont tous été sous la nuée, et que tous ils ont passé à travers la mer,
2 Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
et que tous ils ont été baptisés pour Moïse dans la nuée et dans la mer,
3 Wote walikula chakula kile kile cha roho,
et que tous ils ont mangé la même viande spirituelle,
4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
et que tous ils ont bu le même breuvage spirituel, car ils buvaient d’un rocher spirituel qui les suivait: et le rocher était le Christ.
5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
Mais Dieu n’a point pris plaisir en la plupart d’entre eux, car ils tombèrent dans le désert.
6 Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
Or ces choses arrivèrent comme types de ce qui nous concerne, afin que nous ne convoitions pas des choses mauvaises, comme ceux-là aussi ont convoité.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
Ne soyez pas non plus idolâtres, comme quelques-uns d’eux, ainsi qu’il est écrit: « Le peuple s’assit pour manger et pour boire, et ils se levèrent pour jouer ».
8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
Ne commettons pas non plus la fornication, comme quelques-uns d’eux ont commis la fornication, et il en est tombé en un seul jour 23 000.
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
Ne tentons pas non plus le Christ, comme quelques-uns d’eux l’ont tenté et ont péri par les serpents.
10 Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
Ne murmurez pas non plus, comme quelques-uns d’eux ont murmuré et ont péri par le destructeur.
11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn g165)
Or toutes ces choses leur arrivèrent comme types, et elles ont été écrites pour nous servir d’avertissement, à nous que les fins des siècles ont atteints. (aiōn g165)
12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
Ainsi, que celui qui croit être debout prenne garde qu’il ne tombe.
13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
Aucune tentation ne vous est survenue qui n’ait été une tentation humaine; et Dieu est fidèle, qui ne permettra pas que vous soyez tentés au-delà de ce que vous pouvez [supporter], mais avec la tentation il fera aussi l’issue, afin que vous puissiez la supporter.
14 Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
C’est pourquoi, mes bien-aimés, fuyez l’idolâtrie.
15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
Je parle comme à des personnes intelligentes: jugez vous-mêmes de ce que je dis.
16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
La coupe de bénédiction que nous bénissons, n’est-elle pas la communion du sang du Christ? Le pain que nous rompons, n’est-il pas la communion du corps du Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
Car nous qui sommes plusieurs, sommes un seul pain, un seul corps, car nous participons tous à un seul et même pain.
18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
Considérez l’Israël selon la chair: ceux qui mangent les sacrifices n’ont-ils pas communion avec l’autel?
19 Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
Que dis-je donc? que ce qui est sacrifié à une idole soit quelque chose? ou qu’une idole soit quelque chose?
20 La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
[Non], mais que les choses que les nations sacrifient, elles les sacrifient à des démons et non pas à Dieu: or je ne veux pas que vous ayez communion avec les démons.
21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
Vous ne pouvez boire la coupe du Seigneur et la coupe des démons; vous ne pouvez participer à la table du Seigneur et à la table des démons.
22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
Provoquons-nous le Seigneur à la jalousie? Sommes-nous plus forts que lui?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
Toutes choses sont permises, mais toutes choses ne sont pas avantageuses; toutes choses sont permises, mais toutes choses n’édifient pas.
24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
Que personne ne cherche son propre intérêt, mais celui d’autrui.
25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
Mangez de tout ce qui se vend à la boucherie, sans vous enquérir de rien à cause de la conscience:
26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
« car la terre est au Seigneur, et tout ce qu’elle contient ».
27 Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
Or si quelqu’un des incrédules vous convie, et que vous vouliez aller, mangez de tout ce qui est mis devant vous, sans vous enquérir de rien à cause de la conscience.
28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
Mais si quelqu’un vous dit: Ceci a été offert en sacrifice, – n’en mangez pas, à cause de celui qui vous a avertis, et à cause de la conscience.
29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
Or je dis: la conscience, non la tienne, mais celle de l’autre; car pourquoi ma liberté est-elle jugée par la conscience d’autrui?
30 Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
Si moi, je participe avec action de grâces, pourquoi suis-je blâmé pour une chose dont moi je rends grâces?
31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
Soit donc que vous mangiez, soit que vous buviez, ou quoi que vous fassiez, faites tout pour la gloire de Dieu.
32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
Ne devenez une cause d’achoppement ni aux Juifs, ni aux Grecs, ni à l’assemblée de Dieu;
33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.
comme moi aussi je complais à tous en toutes choses, ne cherchant pas mon avantage propre, mais celui du grand nombre, afin qu’ils soient sauvés.

< 1 Wakorintho 10 >