< 1 Wakorintho 10 >
1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
Now I would not have you ignorant, brothers, that our fathers were all under the cloud, and all passed through the sea;
2 Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
and were all baptized into Moses in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kile kile cha roho,
and all ate the same spiritual food;
4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
and all drank the same spiritual drink. For they drank of a spiritual rock that followed them, and the rock was Christ.
5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
However with most of them, God was not well pleased, for they were overthrown in the wilderness.
6 Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things as they also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
Don’t be idolaters, as some of them were. As it is written, “The people sat down to eat and drink, and rose up to play.”
8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
Let’s not commit sexual immorality, as some of them committed, and in one day twenty-three thousand fell.
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
Let’s not test Christ, as some of them tested, and perished by the serpents.
10 Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
Don’t grumble, as some of them also grumbled, and perished by the destroyer.
11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
Now all these things happened to them by way of example, and they were written for our admonition, on whom the ends of the ages have come. (aiōn )
12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
Therefore let him who thinks he stands be careful that he doesn’t fall.
13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
No temptation has taken you except what is common to man. God is faithful, who will not allow you to be tempted above what you are able, but will with the temptation also make the way of escape, that you may be able to endure it.
14 Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
Therefore, my beloved, flee from idolatry.
15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
I speak as to wise men. Judge what I say.
16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, isn’t it a sharing of the blood of Christ? The bread which we break, isn’t it a sharing of the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
Because there is one loaf of bread, we, who are many, are one body; for we all partake of the one loaf of bread.
18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
Consider Israel according to the flesh. Don’t those who eat the sacrifices participate in the altar?
19 Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
What am I saying then? That a thing sacrificed to idols is anything, or that an idol is anything?
20 La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
But I say that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons and not to God, and I don’t desire that you would have fellowship with demons.
21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
You can’t both drink the cup of the Lord and the cup of demons. You can’t both partake of the table of the Lord and of the table of demons.
22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
Or do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
“All things are lawful for me,” but not all things are profitable. “All things are lawful for me,” but not all things build up.
24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
Let no one seek his own, but each one his neighbor’s good.
25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
Whatever is sold in the butcher shop, eat, asking no question for the sake of conscience,
26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
for “the earth is the Lord’s, and its fullness.”
27 Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
But if one of those who don’t believe invites you to a meal, and you are inclined to go, eat whatever is set before you, asking no questions for the sake of conscience.
28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
But if anyone says to you, “This was offered to idols,” don’t eat it for the sake of the one who told you, and for the sake of conscience. For “the earth is the Lord’s, with all its fullness.”
29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
Conscience, I say, not your own, but the other’s conscience. For why is my liberty judged by another conscience?
30 Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
If I partake with thankfulness, why am I denounced for something I give thanks for?
31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
Whether therefore you eat or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
Give no occasion for stumbling, whether to Jews, to Greeks, or to the assembly of God;
33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.
even as I also please all men in all things, not seeking my own profit, but the profit of the many, that they may be saved.