< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
Now I do not want you to be ignorant, brothers, that our fathers were all under the cloud and all passed through the sea
2 Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
—all were baptized into Moses by the cloud and by the sea—
3 Wote walikula chakula kile kile cha roho,
and all ate the same spiritual food
4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
and drank the same spiritual drink; because they kept drinking from a spiritual rock that accompanied them, and that Rock was the Christ.
5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
For all that, God was not pleased with most of them—their carcasses were scattered around the desert!
6 Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
Now these things became examples for us, to the intent that we should not lust after evil things as they also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
And do not become idolaters, just like some of them; as it is written: “The people sat down to eat and drink, and got up to amuse themselves.”
8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
And let us not fornicate, just as some of them did—and in one day twenty-three thousand died!
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
Neither let us test the Christ, just as also some of them did—and were destroyed by the snakes!
10 Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
And do not grumble, just as also some of them did—and were executed by the destroyer!
11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn g165)
Now all these things happened to them as examples and were written for our admonition, upon whom the ends of the ages have come. (aiōn g165)
12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
So then, let him who thinks he stands be careful that he does not fall!
13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
No testing has overtaken you except what is common to man, and God is competent, who will not allow you to be tested beyond what you can stand, but with the testing will also provide the way out, that you may be able to endure it.
14 Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
Therefore, my beloved, flee from idolatry!
15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
I speak as to wise men; judge for yourselves what I say.
16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
The cup of blessing that we bless, is it not a sharing of the blood of Christ? The bread that we break, is it not a sharing of the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
Since the loaf is one, we, the many, are one body, because we all partake of that single loaf.
18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
Consider the physical Israel: are not those who eat the sacrifices partakers of the altar?
19 Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
So what am I getting at? That an idol is anything, or what is offered to idols is anything?
20 La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
Rather, that the things pagans sacrifice they sacrifice to demons and not to God. I do not want you to become participants with the demons.
21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
You cannot drink the cup of the Lord and the cup of demons; you cannot partake of the Lord's table and of the table of demons.
22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
Are we going to provoke the Lord's jealousy? Are we stronger than He?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
All things are ‘permissible’ for me, but not all things are expedient. All things are ‘permissible’ for me, but not all things edify.
24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
Let no one seek his own, but each one the other's well-being.
25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
Eat whatever is being sold in the meat market, asking no question for the sake of conscience;
26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
since “the earth is the Lord's, and all its fullness.”
27 Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
If some unbeliever invites you and you decide to go, eat whatever is set before you, asking no questions for the sake of conscience.
28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
But if anyone says, “This was offered to idols,” do not eat it for the sake of the speaker and of the conscience; since “the earth is the Lord's, and all its fullness.”
29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
‘Conscience’ I say, not your own but that of the other. Now just why should my freedom be judged by another's conscience?
30 Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
If I partake with thanks, why be slandered over something I give thanks for?
31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
Therefore, whether you eat or you drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
Give no offense, either to Jews or to Greeks or to the Church of God
33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.
—even as I try to please everyone in every way, not seeking my own profit but that of the many, that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >