< 1 Wakorintho 10 >
1 Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.
Now, brethren, I do not wish you to be ignorant, that all our fathers were under the cloud, and that all passed through the sea,
2 Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.
and were all immersed into Moses, in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kile kile cha roho,
and did all eat the same spiritual food,
4 na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.
and did all drink the same spiritual drink: for they drank of that spiritual Rock that followed them, and that Rock was the Christ.
5 Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.
But with the most of them God was not well pleased, for they were overthrown in the wilderness.
6 Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.
Now these things took place as examples for us, that we should not desire evil things, as they, also, desired.
7 Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”
Neither be you idolaters, as some of them were, as it is written: Tho people sat down to eat and to drink, and rose up to engage in idolatrous sport.
8 Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.
Nor let us be guilty of lewdness, as some of them were guilty, and fell, in one day, twenty-three thousand.
9 Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.
Nor let us tempt the Christ, as some of them also tempted, and were destroyed by serpents.
10 Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.
Nor do you murmur, as some of them also murmured, and were destroyed by the destroyer.
11 Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia. (aiōn )
Now all these things happened to them as examples, and they are written for the instruction of us, upon whom the ends of the ages have come. (aiōn )
12 Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
Wherefore, let him that thinks he stands, take heed lest he foil.
13 Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.
No trial has come upon you but such as is common to man: but God is faithful, who will not suffer you to be tried more than you are able to bear; but he will, with the trial, make a way to escape, so that you be able to bear up under it.
14 Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.
Wherefore, my beloved, flee from idolatry.
15 Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.
I speak as to wise men; judge you what I say.
16 Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not the participation of the blood of the Christ? The bread which we break, is it not the participation of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.
Because the loaf is one, we, the many, are one body, for we are all partakers of the one loaf.
18 Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?
Look at Israel according to the flesh: are not those who eat the sacrifices partakers with the altar?
19 Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?
What, then, do I say? That an idol is any thing? or, that what is sacrificed to an idol is any thing?
20 La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.
But I say, that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God. I do not wish you to be partakers with demons.
21 Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.
You can not drink the cup of the Lord, and the cup of demons: you can not be partakers of the table of the Lord, and of the table of demons.
22 Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?
Do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
23 “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.
All meats are lawful for me; but all are not profitable; all are lawful, but all do not edify.
24 Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.
Let no one seek his own, but each the welfare of the other.
25 Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.
Any thing that is sold in the market, eat, asking no questions on account of conscience:
26 Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
for the earth and its fullness are the Lord’s.
27 Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.
If any one of the unbelievers invites you to a feast, and you are disposed to go, eat any thing that is set before you, asking no questions for conscience sake.
28 Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.
But if any one say to you: This is sacrificed to idols; eat not, for the sake of him that pointed it out, and for conscience sake:
29 Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
conscience, I say, not your own, but that of the other. Why, then, is my liberty judged by the conscience of another?
30 Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?
If I partake with thanksgiving, why am I evil spoken of on account of that for which I give thanks?
31 Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
Whether, therefore, you eat or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,
Give no occasion for stumbling, either to the Jews, or to the Greeks, or to the church of God;
33 kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.
even as I please all men in all things, not seeking my own good, but that of the many, in order that they may be saved.