< 1 Wakorintho 1 >

1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
Paul a called apostle of Christ Jesus through [the] will of God and Sosthenes the brother
2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
To the church of God which is being in Corinth, sanctified in Christ Jesus called holy, together with all those calling on the name of the Lord of us Jesus Christ in every place, both theirs (then *k*) and ours:
3 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God Father of us and [the] Lord Jesus Christ.
4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
I thank the God of mine always concerning you for the grace of God which having been given you in Christ Jesus
5 Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
for in everything you have been enriched in Him in all speech and in all knowledge,
6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
even as the testimony about Christ was confirmed in you,
7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
so as for you not to be lacking in not one gift eagerly awaiting the revelation of the Lord of us Jesus Christ;
8 Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who also will sustain you to [the] end blameless in the day of the Lord of us Jesus Christ.
9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
Faithful [is] God, through whom you were called into fellowship with the Son of Him Jesus Christ the Lord of us.
10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
I exhort now you, brothers, through the name of the Lord of us Jesus Christ that the same thing you may speak all and not there may be among you divisions, you may be however knit together in the same mind and in the same judgment.
11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
It was shown for to me concerning you, brothers of mine, by those of Chloe that quarrels among you there are.
12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
I mean now this, that each of you says; I myself indeed am of Paul, I myself however of Apollos, I myself however of Cephas, I myself however of Christ.
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Has been divided Christ? Surely not Paul was crucified for you? Or into the name of Paul were you baptized?
14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
I thank God that no [one] of you I baptized only except Crispus and Gaius,
15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
so that not anyone may say that into my name (you were baptized. *N(K)O*)
16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
I baptized now also the of Stephanas household; as to the rest not I know whether any other I baptized.
17 Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
Not for sent me Christ to baptize but to evangelise; not in wisdom of discourse, that not may be emptied of power the cross of the Christ.
18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
The message for of the cross to those indeed perishing foolishness is, to those however being saved to us power of God it is.
19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
It has been written for: I will destroy the wisdom of the wise, and the intelligence of the intelligent I will frustrate.
20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn g165)
Where [is the] wise? Where [the] scribe? Where [the] debater of the age this? Surely has made foolish God the wisdom of the world (this? *k*) (aiōn g165)
21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
Since for in the wisdom of God not knew the world through the wisdom God, was pleased God through the foolishness of the proclamation to save those believing;
22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
Seeing that both Jews (signs *N(K)O*) ask for and Greeks wisdom seek,
23 Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
we ourselves however preach Christ crucified, to [the] Jews indeed a stumbling block (to Gentiles *N(K)O*) however foolishness
24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
to them however to those called, Jews both and to Greeks, Christ of God [the] power and of God [the] wisdom.
25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
For the foolishness of God wiser than men is and the weakness of God stronger than men (is. *k*)
26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
Consider for the calling of you, brothers, that not many wise according to flesh [were], not many powerful, not many of noble birth,
27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
But the foolish things of the world has chosen God that He may shame the wise and the weak things of the world chose God that He may shame the strong,
28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
and the low-born of the world and the [things] despised chose God, (and *ko*) the [things] not being, that the [things] being He may annul,
29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
so that not may boast all flesh before (God. *N(K)O*)
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
Out of Him however you yourselves are in Christ Jesus, who has been made wisdom unto us from God, righteousness and also sanctification and redemption,
31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
in order that even as it has been written: The [one] boasting in [the] Lord he should boast.

< 1 Wakorintho 1 >