< 1 Wakorintho 1 >
1 Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.
Paul, a called apostle of Jesus Christ, through the will of God, and Sosthenes the brother,
2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:
to the Assembly of God that is in Corinth, to those sanctified in Christ Jesus, called holy ones, with all those calling on the Name of our Lord Jesus Christ in every place—both theirs and ours:
3 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ!
4 Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.
I give thanks to my God always concerning you for the grace of God that was given to you in Christ Jesus,
5 Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,
that in everything you were enriched in Him, in all discourse and all knowledge,
6 kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.
according as the testimony of the Christ was confirmed in you,
7 Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
so that you are not behind in any gift, waiting for the revelation of our Lord Jesus Christ,
8 Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
who also will confirm you to the end—unblamable in the day of our Lord Jesus Christ;
9 Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.
faithful [is] God, through whom you were called into the fellowship of His Son Jesus Christ our Lord.
10 Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.
And I call on you, brothers, through the Name of our Lord Jesus Christ, that the same thing you may all say, and there may not be divisions among you, and you may be perfected in the same mind, and in the same judgment,
11 Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.
for it was signified to me concerning you, my brothers, by those of Chloe, that contentions are among you;
12 Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”
and I say this, that each one of you says, “I, indeed, am of Paul,” and “I of Apollos,” and “I of Cephas,” and “I of Christ.”
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
Has the Christ been divided? Was Paul crucified for you? Or were you immersed into the name of Paul?
14 Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.
I give thanks to God that I immersed no one of you, except Crispus and Gaius—
15 Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.
that no one may say that to my own name I immersed;
16 (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
and I also immersed Stephanas’ household—further, I have not known if I immersed any other.
17 Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.
For Christ did not send me to immerse, but to proclaim good news, not in wisdom of discourse, that the Cross of the Christ may not be made of no effect;
18 Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
for the word of the Cross to those indeed perishing is foolishness, and to us—those being saved—it is the power of God,
19 Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”
for it has been written: “I will destroy the wisdom of the wise, and the intelligence of the intelligent I will bring to nothing”;
20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu? (aiōn )
where [is] the wise? Where the scribe? Where a disputer of this age? Did God not make foolish the wisdom of this world? (aiōn )
21 Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.
For seeing in the wisdom of God the world through the wisdom did not know God, it pleased God through the foolishness of the preaching to save those believing.
22 Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.
Since also Jews ask a sign, and Greeks seek wisdom,
23 Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.
also we preach Christ crucified, to Jews, indeed, a stumbling-block, and to Greeks foolishness,
24 Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.
and to those called—both Jews and Greeks—Christ the power of God, and the wisdom of God,
25 Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.
because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men;
26 Ndugu zangu, kumbukeni mlivyokuwa mlipoitwa. Kwa kipimo cha kibinadamu, si wengi wenu mliokuwa na hekima. Si wengi mliokuwa na ushawishi, si wengi mliozaliwa katika jamaa zenye vyeo.
for see your calling, brothers, that not many [are] wise according to the flesh, not many mighty, not many noble;
27 Lakini Mungu alivichagua vitu vipumbavu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye hekima, Mungu alivichagua vitu dhaifu vya ulimwengu ili awaaibishe wenye nguvu.
but God chose the foolish things of the world that He may put the wise to shame; and God chose the weak things of the world that He may put the strong to shame;
28 Alivichagua vitu vya chini na vinavyodharauliwa vya dunia hii, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko,
and God chose the base things of the world, and the things despised, and the things that are not, that He may make useless the things that are—
29 ili mtu yeyote asijisifu mbele zake.
that no flesh may glory before Him;
30 Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanyika kwetu hekima itokayo kwa Mungu, yaani haki, na utakatifu na ukombozi.
but out of Him you are in Christ Jesus, who became to us from God wisdom, righteousness also, and sanctification, and redemption,
31 Hivyo, kama ilivyoandikwa: “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
that, according as it has been written: “He who is glorying—let him glory in the LORD.”