< 1 Nyakati 9 >
1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
And all Israel have reckoned themselves by genealogy, and lo, they are written on the book of the kings of Israel and Judah — they were removed to Babylon for their trespass.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
And the first inhabitants, who [are] in their possession, in their cities, of Israel, [are] the priests, the Levites, and the Nethinim.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
And in Jerusalem dwelt of the sons of Judah, and of the sons of Benjamin, and of the sons of Ephraim and Manasseh:
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Uthai son of Ammihud, son of Omri, son of Imri, son of Bani, of the sons of Pharez, son of Judah.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
And of the Shilonite: Asaiah the first-born, and his sons.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
And of the sons of Zerah: Jeuel, and their brethren, six hundred and ninety.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
And of the sons of Benjamin: Sallu son of Meshullam, son of Hodaviah, son of Hassenuah,
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
and Ibneiah son of Jeroham, and Elah son of Uzzi, son of Michri, and Meshullam son of Shephatiah, son of Reuel, son of Ibnijah.
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
And their brethren, according to their generations, [are] nine hundred and fifty and six. All these [are] men, heads of fathers, according to the house of their fathers.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
And of the priests: Jedaiah, and Jehoiarib, and Jachin,
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
and Azariah son of Hilkiah, son of Meshullam, son of Zadok, son of Meraioth, son of Ahitub, leader in the house of God;
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
and Adaiah son of Jeroham, son of Pashhur, son of Malchijah, and Maasai son of Adiel, son of Jahzerah, son of Meshullam, son of Meshillemith, son of Immer.
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
And their brethren, heads to the house of their fathers, a thousand and seven hundred and sixty, mighty in valour, [are] for the work of the service of the house of God.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
And of the Levites: Shemaiah son of Hashshub, son of Azrikam, son of Hashabiah, of the sons of Merari;
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
and Bakbakkar, Heresh, and Galal, and Mattaniah son of Micah, son of Zichri, son of Asaph;
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
and Obadiah son of Shemariah, son of Galal, son of Jeduthun, and Berechiah, son of Asa, son of Elkanah, who is dwelling in the villages of the Netophathite.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
And the gatekeepers [are] Shallum, and Akkub, and Talmon, and Ahiman, and their brethren — Shallum [is] the head;
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
and hitherto they [are] at the gate of the king eastward; they [are] the gatekeepers for the companies of the sons of Levi.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
And Shallum son of Kore, son of Ebiasaph, son of Korah, and his brethren, of the house of his father, the Korahites, [are] over the work of the service, keepers of the thresholds of the tent, and their fathers [are] over the camp of Jehovah, keepers of the entrance;
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
and Phinehas son of Eleazar hath been leader over them formerly; Jehovah [is] with him.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Zechariah son of Meshelemiah [is] gatekeeper at the opening of the tent of meeting.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
All of those who are chosen for gatekeepers at the thresholds [are] two hundred and twelve; they [are] in their villages, by their genealogy; they whom David and Samuel the seer appointed in their office.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
And they and their sons [are] over the gates of the house of Jehovah, even of the house of the tent, by watches.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
At four sides are the gatekeepers, east, west, north, and south.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
And their brethren in their villages [are] to come in for seven days from time to time with these.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
For in office [are] the four chiefs of the gatekeepers, they are Levites, and they have been over the chambers, and over the treasuries of the house of God,
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
and round about the house of God they lodge, for on them [is] the watch, and they [are] over the opening, even morning by morning.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
And [some] of them [are] over the vessels of service, for by number they bring them in, and by number they take them out.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
And [some] of them are appointed over the vessels, even over all the vessels of the sanctuary, and over the fine flour, and the wine, and the oil, and the frankincense, and the spices.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
And [some] of the sons of the priests are mixing the mixture for spices.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
And Mattithiah, of the Levites (he [is] the first-born to Shallum the Korahite), [is] in office over the work of the pans.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
And of the sons of the Kohathite, [some] of their brethren [are] over the bread of the arrangement, to prepare [it] sabbath by sabbath.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
And these who sing, heads of fathers of the Levites, in the chambers, [are] free, for by day and by night [they are] over them in the work.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
These heads of the fathers of the Levites throughout their generations [are] heads. These have dwelt in Jerusalem.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
And in Gibeon dwelt hath the father of Gibeon, Jehiel, and the name of his wife [is] Maachah;
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
and his son, the first-born, [is] Abdon, and Zur, and Kish, and Baal, and Ner, and Nadab,
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
and Gedor, and Ahio, and Zechariah, and Mikloth.
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
And Mikloth begat Shimeam, and they also, over-against their brethren, have dwelt in Jerusalem with their brethren.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
And Ner begat Kish, and Kish begat Saul, and Saul begat Jonathan, and Malchi-Shua, and Abinadab, and Esh-Baal.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
And a son of Jonathan [is] Merib-Baal, and Merib-Baal begat Micah.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
And sons of Micah: Pithon, and Melech, and Tahrea,
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
and Ahaz — he begat Jaarah, and Jaarah begat Alemeth, and Azmaveth, and Zimri, and Zimri begat Moza,
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
and Moza begat Binea, and Rephaiah [is] his son. Eleasah his son, Azel his son.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
And to Azel [are] six sons, and these their names: Azrikam, Bocheru, and Ishmael, and Sheariah, and Obadiah, and Hanan: these [are] sons of Azel.