< 1 Nyakati 9 >
1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
And all Israel was numbered: and the sum of them was written in the book of the kings of Israel, and Juda: and they were carried away to Babylon for their transgression.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Now the first that dwelt in their possessions, and in their cities, were the Israelites, and the priests, and the Levites, and the Nathineans.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
And in Jerusalem dwelt of the children of Juda, and of the children of Benjamin, and of the children of Ephraim, and of Manasses.
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Othei the son of Ammiud, the son of Amri, the son of Omrai, the son of Bonni, of the sons of Phares the son of Juda.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
And of Siloni: Asaia the firstborn, and his sons.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
And of the sons of Zara: Jehuel, and their brethren, six hundred and ninety.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
And of the sons of Benjamin: Sale the son of Mosollam, the son of Oduia, the son of Asana:
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
And Jobania the son of Jeroham: and Ela the son of Ozi, the son of Mochori: and Mosallam the son of Saphatias, the son of Rahuel, the son of Jebania:
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
And their brethren by their families, nine hundred and fifty-six. All these were heads of their families, by the houses of their fathers.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
And of the priests: Jedaia, Joiarib, and Jachin:
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
And Azarias the son of Helcias, the son of Mosollam, the son of Sadoc, the son of Maraioth, the son of Achitob, high priest of the house of God.
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
And Adaias the son of Jeroham, the son of Phassur, the son of Melchias, and Maasai the son of Adiel, the son of Jezra, the son of Mosollam, the son of Mosollamith, the son of Emmer.
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
And their brethren heads in their families a thousand seven hundred and threescore, very strong and able men for the work of the ministry in the house of God.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
And of the Levites: Semeia the son of Hassub the son of Ezricam, the son of Hasebia of the sons of Merari.
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
And Bacbacar the carpenter, and Galal, and Mathania the son of Micha, the son of Zechri the son of Asaph:
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
And Obdia the son of Semeia, the son of Galal, the son of Idithum: and Barachia the son of Asa, the son of Elcana, who dwelt in the suburbs of Netophati.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
And the porters were Sellum, and Accub, and Telmon, and Ahiman: and their brother Sellum was the prince,
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
Until that time, in the king’s gate eastward, the sons of Levi waited by their turns.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
But Sellum the son of Core, the son of Abiasaph, the son of Core, with his brethren and his father’s house, the Corites were over the works of the service, keepers of the gates of the tabernacle: and their families in turns were keepers of the entrance of the camp of the Lord.
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
And Phinees the son of Eleazar, was their prince before the Lord,
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
And Zacharias the son of Mosollamia, was porter of the gate of the tabernacle of the testimony:
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
All these that were chosen to be porters at the gates, were two hundred and twelve: and they mere registered in their proper towns: whom David and Samuel the seer appointed in their trust.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
As well them as their sons, to keep the gates of the house of the Lord, and the tabernacle by their turns.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
In four quarters were the porters: that is to say, toward the east, and west, and north, and south.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
And their brethren dwelt in villages, and came upon their sabbath days from time to time.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
To these four Levites were committed the whole number of the porters, and they were over the chambers, and treasures, of the house of the Lord.
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
And they abode in their watches round about the temple of the Lord: that when it was time, they might open the gates in the morning.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
And some of their stock had the charge of the vessels for the ministry: for the vessels were both brought in and carried out by number.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
Some of them also had the instruments of the sanctuary committed unto them, and the charge of the fine flour, and wine, and oil, and frankincense, and spices.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
And the sons of the priests made the ointments of the spices.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
And Mathathias a Levite, the firstborn of Sellum the Corite, was overseer of such things as were fried in the fryingpan.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
And some of the sons of Caath their brethren, were over the leaves of proposition, to prepare always new for every sabbath.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
These are the chief of the singing men of the families of the Levites, who dwelt in the chambers, by the temple, that they might serve continually day and night in their ministry.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
The heads of the Levites, princes in their families, abode in Jerusalem.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
And in Gabaon dwelt Jehiel the father of Gabaon, and the name of hill wife was Maacha:
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
His firstborn son Abdon, and Sur, and Cis, and Baal, and Ner, and Nadab,
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
Gedor also, and Ahio, and Zacharias, and Macelloth.
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
And Macelloth beget Samaan: these dwelt over against their brethren in Jerusalem, with their brethren.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
Now Ner beget Cia: and Cis begot Saul: and Saul beget Jonathan and Melchisua, and Abinadab, and Esbaal.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
And the son of Jonathan, was Meribbaal: and Meribbaal beget Micha.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
And the sons of Micha, were Phithon, and Melech, and Tharaa, and Ahaz.
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
And Ahaz beget Jara, and Jara beget Alamath, and Azmoth, and Zamri. And Zamri beget Mesa.
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
And Mesa beget Banaa: whose son Raphaia beget Elasa: of whom was born Asel.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
And heel had six sons whose names are, Ezricam, Bochru, Ismahel, Saria, Obdia, Hanan: these are the sons of Asel.