< 1 Nyakati 9 >
1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
So all Israel was listed by their families; and, truly, they are recorded in the book of the kings of Israel. And Judah was taken away as prisoners to Babylon because of their sin.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Now the first to take up their heritage in their towns were: Israel, the priests, the Levites, and the Nethinim.
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
And in Jerusalem there were living some of the sons of Judah, and of Benjamin, and of Ephraim and Manasseh;
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Uthai, the son of Ammihud, the son of Omri, the son of Imri, the son of Bani, of the sons of Perez, the son of Judah.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
And of the Shilonites: Asaiah the oldest, and his sons.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
And of the sons of Zerah: Jeuel, and their brothers, six hundred and ninety.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
And of the sons of Benjamin: Sallu, the son of Meshullam, Judah, the son of Hassenuah,
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
And Ibneiah, the son of Jeroham, and Elah, the son of Uzzi, the son of Michri, and Meshullam, the son of Shephatiah, the son of Reuel, the son of Ibnijah;
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
And their brothers, in the list of their generations, nine hundred and fifty-six. All these men were heads of families, listed by the names of their fathers.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
And of the priests: Jedaiah and Jehoiarib and Jachin
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
And Azariah, the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, the ruler of the house of God;
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
And Adaiah, the son of Jeroham, the son of Pashhur, the son of Malchijah, and Maasai, the son of Adiel, the son of Jahzerah, the son of Meshullam, the son of Meshillemith, the son of Immer;
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
And their brothers, heads of their families, a thousand and seven hundred and sixty: able men, doing the work of the house of God.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
And of the Levites: Shemaiah, the son of Hasshub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, of the sons of Merari;
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
And Bakbakkar, Heresh, and Galal, and Mattaniah, the son of Mica, the son of Zichri, the son of Asaph;
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
And Obadiah, the son of Shemaiah, the son of Galal, the son of Jeduthun, and Berechiah, the son of Asa, the son of Elkanah, who were living in the small towns of the Netophathites.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
And the door-keepers: Shallum and Akkub and Talmon and Ahiman and their brothers: Shallum was the chief.
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
Up till then they had been at the king's door to the east. They were door-keepers for the tents of the sons of Levi.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
And Shallum, the son of Kore, the son of Ebiasaph, the son of Korah, and his brothers, of his family, the Korahites, were responsible for everything which had to be done in connection with the order of worship, keepers of the doors of the Tent; their fathers had had the care of the tents of the Lord, being keepers of the doorway.
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
In the past Phinehas, the son of Eleazar, had been ruler over them; may the Lord be with him!
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Zechariah, the son of Meshelemiah, was keeper of the door of the Tent of meeting.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
There were two hundred and twelve whose business it was to keep the doorway. These were listed by families in the country places where they were living, whom David and Samuel the seer put in their responsible positions.
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
So they and their sons had the care of the doors of the house of the Lord, the house of the Tent, as watchers.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
There were keepers of the doors on the four sides, to the east, west, north, and south.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
And their brothers, in the country places where they were living, were to come in every seven days to be with them from time to time.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
For the four chief door-keepers, who were Levites, had a special position, looking after the rooms and the store-houses of the house of God.
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
Their sleeping-rooms were round the house of God, for they had the care of it, and were responsible for opening it morning by morning.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
Certain of them had the care of the vessels used in worship, to keep an account of them when they came in and when they were taken out again.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
And some of them were responsible for the holy things and for the vessels of the holy place, and the meal and the wine and the oil and the perfume and the spices.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
And some of the sons of the priests were responsible for crushing the spices.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
And Mattithiah, one of the Levites, the oldest son of Shallum the Korahite, was responsible for cooking the flat cakes.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
And some of their brothers, sons of the Kohathites, were responsible for the holy bread which was put in order before the Lord, to get it ready every Sabbath.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
And these were those who had the ordering of the music and songs, heads of families of the Levites, who were living in the rooms, and were free from other work, for their work went on day and night.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
These were heads of families of the Levites in their generations, chief men; they were living at Jerusalem.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
And in Gibeon was living the father of Gibeon, Jeiel, whose wife's name was Maacah;
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
And Abdon his oldest son, and Zur and Kish and Baal and Ner and Nadab
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
And Gedor and Ahio and Zechariah and Mikloth
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
Mikloth was the father of Shimeam. They were living with their brothers in Jerusalem opposite their brothers.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
And Ner was the father of Kish; and Kish was the father of Saul; and Saul was the father of Jonathan and Malchi-shua and Abinadab and Eshbaal.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
And the son of Jonathan was Merib-baal; and Merib-baal was the father of Micah.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
And the sons of Micah: Pithon and Melech and Tahrea and Ahaz.
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
And Ahaz was the father of Jarah; and Jarah was the father of Alemeth and Azmaveth and Zimri; and Zimri was the father of Moza.
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
And Moza was the father of Binea; and Rephaiah was his son, Eleasah his son, Azel his son.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
And Azel had five sons, whose names are: Azrikam, his oldest son, and Ishmael and Sheariah and Obadiah and Hanan: these were the sons of Azel.