< 1 Nyakati 9 >

1 Waisraeli wote waliorodheshwa katika koo zilizoandikwa kwenye kitabu cha wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda walichukuliwa mateka kwenda Babeli kwa sababu ya kukosa uaminifu kwa Mungu.
A tak všickni Izraelští sečteni byli, a aj, zapsáni jsou v knize králů Izraelských a Judských, a přeneseni jsou do Babylona pro přestoupení své.
2 Basi watu wa kwanza kurudi kukaa kwenye milki zao katika miji yao walikuwa baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi na watumishi wa Hekalu.
Ti pak, kteříž bydlili prvé v vládařství svém v městech svých, totiž Izraelští, kněží, Levítové a Netinejští,
3 Wale waliotoka Yuda, Benyamini, Efraimu na Manase ambao waliishi Yerusalemu walikuwa:
Bydlili v Jeruzalémě, z synů Judových, z synů Beniaminových, ano i z synů Efraimových a Manassesových:
4 Uthai mwana wa Amihudi, mwana wa Omri, mwana wa Imri, mwana wa Bani, wa wana wa Peresi, mwana wa Yuda.
Uttai syn Amiuda, syna Amri, syna Imri, syna Bani, z synů Fáresových, syna Judova.
5 Wazao wa Washiloni waliorudi ni: Asaya mzaliwa wa kwanza na wanawe.
A z čeledi Silonovy: Azaiáš prvorozený a synové jeho.
6 Kwa wana wa Zera: Yeueli. Watu wa Yuda jumla yao walikuwa watu 690.
A z synů Zerachových: Jehuel, a příbuzných jejich šest set a devadesát.
7 Kwa Benyamini walikuwa: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Hodavia, mwana wa Hasenua;
Z synů pak Beniaminových: Sallu syn Mesullama, syna Hodavia, syna Hasenuova,
8 Ibneya mwana wa Yerohamu, Ela mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya.
A Ibneiáš syn Jerochamův, Ela syn Uzi, syna Michri, a Mesullam syn Sefatiáše, syna Rehuelova, syna Ibniášova.
9 Watu kutoka Benyamini kama walivyoorodheshwa katika koo zao jumla yao ni 956. Watu hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao.
Bratří také jejich po pokoleních jejich, devět set padesáte a šest; všickni ti muži knížata čeledí po domích otců svých.
10 Wa jamaa za makuhani walikuwa: Yedaya, Yehoyaribu na Yakini;
Z kněží také Jedaiáš, Jehoiarib a Jachin,
11 Azaria mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu aliyekuwa afisa kiongozi wa nyumba ya Mungu.
Azariáš syn Helkiáše, syna Mesullamova, syna Sádochova, syna Meraiotova, syna Achitobova, kníže v domě Božím.
12 Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya; Maasai, mwana wa Adieli, mwana wa Yahzera, mwana wa Meshulamu, mwana wa Meshilemithi, mwana wa Imeri.
A Adaiáš syn Jerochama, syna Paschurova, syna Malchiášova, a Masai syn Adiele, syna Jachzery, syna Mesullamova, syna Mesillemitova, syna Immerova.
13 Makuhani waliokuwa viongozi wa jamaa zao walikuwa 1,760. Walikuwa watu wenye uwezo, waliowajibika kuhudumu katika nyumba ya Mungu.
A bratří jejich knížata po domích otců svých, tisíc sedm set a šedesát mužů udatných v práci přisluhování domu Božího.
14 Jamaa za Walawi walikuwa: Shemaya, mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, wa wana wa Merari.
A z Levítů: Semaiáš syn Chasuba, syna Azrikamova, syna Chasabiášova, z synů Merari.
15 Bakbakari, Hereshi, Galali na Matania mwana wa Mika, mwana wa Zikri, mwana wa Asafu.
A Bakbakar Cheres, a Galal, a Mataniáš syn Míchy, syna Zichri, syna Azafova.
16 Obadia mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni. Berekia mwana wa Asa, mwana wa Elikana, ambao waliishi katika vijiji vya Wanetofathi.
A Abdiáš syn Semaiáše, syna Galalova, syna Jedutunova, a Berechiáš syn Asy, syna Elkánova, kterýž přebýval ve vsech Netofatských.
17 Mabawabu katika Hekalu la Bwana waliorudi walikuwa: Shalumu, Akubu, Talmoni, Ahimani na ndugu zao. Shalumu alikuwa mlinzi wao mkuu.
Též vrátní: Sallum a Akkub, a Talmon, Achiman, i bratří jejich, z nichž byl Sallum kníže.
18 Walikuwa wamewekwa katika lango la mfalme lililokuwa upande wa mashariki, mpaka wakati huu. Hawa walikuwa mabawabu wa kutoka kwenye kambi ya Walawi.
Kterýž až po dnes v bráně královské stával k východu, onino pak vrátnými byli po houfích synů Léví.
19 Shalumu mwana wa Kore, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora, pamoja na mabawabu wenzake kutoka jamaa yake ya Kora waliwajibika kulinda malango ya Hema, kama vile baba zao walivyokuwa wamewajibika kulinda ingilio la Maskani ya Bwana.
Ale Sallum syn Chóre, syna Abiazafova, syna Chóre, a bratří jeho z domu otce jeho, Chorejští, nad pracemi přisluhování, ostříhali prahů při stánku, tak jako otcové jejich nad vojskem Hospodinovým, kteříž ostříhali vcházení.
20 Hapo zamani Finehasi mwana wa Eleazari alikuwa kiongozi wa mabawabu, naye Bwana alikuwa pamoja naye:
Nad kterýmiž Fínes syn Eleazarův byl někdy knížetem, a Hospodin byl s ním.
21 Zekaria mwana wa Meshelemia alikuwa bawabu katika ingilio la Hema la Kukutania.
Zachariáš pak syn Meselemiášův vrátným byl u dveří stánku úmluvy.
22 Jumla ya waliochaguliwa kuwa mabawabu katika sakafu za kupuria nafaka walikuwa watu 212. Waliandikishwa kwa koo zao kwenye vijiji vyao. Mabawabu hawa waliwekwa katika nafasi zao za kuaminiwa na Daudi pamoja na mwonaji Samweli.
Všickni ti voleni za vrátné k veřejím, osob dvě stě a dvanáct. Ti ve vsech svých vyčteni jsou, kteréž nařídil David a Samuel vidoucí, pro jejich věrnost,
23 Wao na wazao wao walikuwa viongozi wa kulinda malango ya nyumba ya Bwana, nyumba iliyoitwa Hema.
Aby oni i synové jejich byli při branách domu Hospodinova, v domě stánku po strážích.
24 Mabawabu walikuwa pande zote nne: mashariki, magharibi, kaskazini na kusini.
Po čtyřech stranách byli vrátní, k východu, k západu, k půlnoci a ku poledni.
25 Ndugu zao katika vijiji vyao walikuwa wakija mara kwa mara na kuwasaidia katika kazi zao kwa vipindi mbalimbali vya siku saba.
A bratří jejich, po vsech svých bydlící, aby každého sedmého dne časy svými přicházeli s nimi.
26 Lakini mabawabu wanne wakuu, waliokuwa Walawi, walikabidhiwa wajibu kwa ajili ya vyumba na hazina katika nyumba ya Mungu.
Nebo Levítové byli pod spravou těch čtyř předních vrátných, a byli nad komorami a nad poklady domu Božího,
27 Walikesha mahali walipowekwa kuizunguka nyumba ya Mungu, kwa sababu iliwapasa kuilinda. Pia walitunza funguo kwa ajili ya kufungua mlango kila siku asubuhi.
A aby vůkol domu Božího ponocovali; nebo jim poručena stráž, a otvírati každý den ráno.
28 Baadhi yao walikuwa viongozi wa kutunza vifaa vilivyotumika katika huduma ndani ya Hekalu; walivihesabu kila vilipoingizwa ndani na kila vilipotolewa.
Z těch také ustaveni nad nádobami přisluhování; nebo v počtu vnášeli je, a v jistém počtu též vynášeli.
29 Wengine walipangiwa kutunza mapambo na vifaa vingine vya patakatifu, pamoja na unga, divai, mafuta, uvumba na vikolezo.
Z nichž opět někteří postaveni byli nad nádobami jinými a nade všemi nádobami posvátnými, a nad bělí, vínem, olejem, kadidlem a vonnými věcmi.
30 Lakini baadhi ya makuhani walifanya kazi ya kuchanganya vikolezo.
Někteří také synové kněžští strojili masti z těch vonných věcí.
31 Mlawi aliyeitwa Matithia, mwana mzaliwa wa kwanza wa Shalumu, wa ukoo wa Kora, alikabidhiwa wajibu kwa ajili ya kuoka mikate ya sadaka.
Matatiáš pak z Levítů, prvorozený Salluma Choritského, správcí byl těch věcí, kteréž se na pánvi smažily.
32 Baadhi ya ndugu zao wa ukoo wa Kohathi walikuwa viongozi wa kuandaa mikate ya Wonyesho kwa ajili ya kila Sabato, mikate iliyokuwa inawekwa mezani.
A z synů Kahat, z bratří jejich, byli ustanoveni nad chlebem předložení, aby jej připravovali na každou sobotu.
33 Wale waliokuwa waimbaji, viongozi wa jamaa za Walawi, waliishi katika vyumba vya Hekalu, nao hawakufanya shughuli nyingine yoyote kwa sababu iliwapasa kuwajibika kwa kazi hiyo usiku na mchana.
Z těch také byli zpěváci, přednější z čeledí otcovských mezi Levíty bydlíce, nejsouce zaměstknaní něčím jiným; nebo ve dne i v noci k své povinnosti státi musili.
34 Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa za Walawi, wakuu kama walivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu.
Ti jsou přední z čeledí otcovských mezi Levíty v čeledech svých, a ti přední jsouce, bydlili v Jeruzalémě.
35 Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka,
V Gabaon pak bydlili, otec Gabaonitských Jehiel, a jméno manželky jeho Maacha.
36 mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu,
Syn pak jeho prvorozený Abdon, Zur, Cis, Bál, Ner a Nádab.
37 Gedori, Ahio, Zekaria na Miklothi.
Ale Gedor, Achio, Zachariáš a Miklot,
38 Miklothi akamzaa Shimeamu. Wao pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu.
(Miklot pak zplodil Simam), ti také naproti bratřím svým bydlili v Jeruzalémě s bratřími svými.
39 Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli. Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali.
Ner pak zplodil Cisa, a Cis zplodil Saule, Saul pak zplodil Jonatu, Melchisua, Abinadaba a Ezbále.
40 Yonathani akamzaa Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika.
Syn pak Jonatův Meribbál, a Meribbál zplodil Mícha.
41 Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea, na Ahazi.
Synové pak Míchovi: Piton, Melech, Tarea.
42 Ahazi akamzaa Yara, Yara akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa.
Achaz pak zplodil Járu, Jára pak zplodil Alemeta, Azmaveta a Zimri. Zimri pak zplodil Mozu.
43 Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Refaya, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli.
Moza pak zplodil Bina. Refaiáš syn jeho, Elasa syn jeho, Azel syn jeho.
44 Aseli alikuwa na wana sita, na haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Aseli.
Azel pak měl šest synů, jichžto tato jsou jména: Azrikam, Bochru, Izmael, Seariáš, Abdiáš a Chanan. Ti jsou synové Azelovi.

< 1 Nyakati 9 >