< 1 Nyakati 7 >

1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
Dos filhos de Issachar: Tola, Puah, Jashub, e Shimron, quatro.
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
Dos filhos de Tola: Uzzi, Rephaiah, Jeriel, Jahmai, Ibsam e Shemuel, chefes das casas de seus pais, de Tola; poderosos homens de valor em suas gerações. O número deles nos dias de Davi era de vinte e dois mil e seiscentos.
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
O filho de Uzzi: Izrahiah. Os filhos de Izrahiah: Michael, Obadiah, Joel, e Isshiah, cinco; todos eles homens chefes.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
Com eles, por suas gerações, depois das casas de seus pais, estavam bandas do exército para a guerra, trinta e seis mil; pois tinham muitas esposas e filhos.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
Seus irmãos entre todas as famílias de Issachar, poderosos homens de valor, listados ao todo pela genealogia, eram oitenta e sete mil.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
Os filhos de Benjamin: Bela, Becher, e Jediael, três.
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
Os filhos de Bela: Ezbon, Uzzi, Uzziel, Jerimoth e Iri, cinco; chefes de casa dos pais, homens poderosos e de valor; e foram listados por genealogia vinte e dois mil e trinta e quatro.
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
Os filhos de Becher: Zemirah, Joash, Eliezer, Elioenai, Omri, Jeremoth, Abijah, Anathoth, e Alemeth. Todos estes foram os filhos de Becher.
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
Eles foram listados por genealogia, depois de suas gerações, chefes das casas de seus pais, homens poderosos de valor, vinte mil e duzentos.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
O filho de Jediael: Bilhan. Os filhos de Bilhan: Jeush, Benjamin, Ehud, Chenaanah, Zethan, Tarshish, e Ahishahar.
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
Todos estes foram filhos de Jediael, de acordo com os chefes de família de seus pais, poderosos homens de valor, dezessete mil e duzentos, que puderam sair para a guerra no exército.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
So eram Shuppim, Huppim, os filhos de Ir, Hushim, e os filhos de Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
Os filhos de Naftali: Jahziel, Guni, Jezer, Shallum, e os filhos de Bilhah.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
Os filhos de Manasseh: Asriel, a quem sua concubina, a Aramitess, aborreceu. Ela deu à luz Machir, o pai de Gilead.
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
Machir levou uma esposa de Huppim e Shuppim, cujo nome da irmã era Maacah. O nome da segunda era Zelophehad; e Zelophehad tinha filhas.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
Maacah, a esposa de Machir, teve um filho, e ela lhe deu o nome de Peresh. O nome de seu irmão era Sheresh; e seus filhos eram Ulam e Rakem.
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
Os filhos de Ulam: Bedan. Estes eram os filhos de Gilead, o filho de Machir, o filho de Manasseh.
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
Sua irmã Hammolecheth deu à luz Ishhod, Abiezer, e Mahlah.
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
Os filhos de Shemida eram Ahian, Shechem, Likhi, e Aniam.
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Os filhos de Efraim: Shuthelah, Bered seu filho, Tahath seu filho, Eleadah seu filho, Tahath seu filho,
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
Zabad seu filho, Shuthelah seu filho, Ezer, e Elead, que os homens de Gate que nasceram na terra mataram, porque desceram para levar seu gado.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
Ephraim seu pai chorou muitos dias, e seus irmãos vieram para confortá-lo.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
Ele foi até sua esposa, e ela concebeu e deu à luz um filho, e ele o chamou de Beriah, porque havia problemas com sua casa.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
Sua filha era Sheerah, que construiu Beth Horon, a inferior e a superior, e Uzzen Sheerah.
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
Rephah era seu filho, Resheph seu filho, Telah seu filho, Tahan seu filho,
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Ladan seu filho, Ammihud seu filho, Elishama seu filho,
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Nun seu filho, e Joshua seu filho.
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
Seus bens e assentamentos foram Betel e suas cidades, e Naaran ao leste, e Gezer ao oeste com suas cidades; Shechem também e suas cidades, para Azzah e suas cidades;
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
e pelas fronteiras das crianças de Manasseh, Beth Shean e suas cidades, Taanach e suas cidades, Megiddo e suas cidades, e Dor e suas cidades. Os filhos de José, o filho de Israel, viviam neles.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
Os filhos de Asher: Imnah, Ishvah, Ishvi, e Beriah. Serah era irmã deles.
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
Os filhos de Beriah: Heber e Malchiel, que foi o pai de Birzaith.
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
Heber tornou-se o pai de Japhlet, Shomer, Hotham e Shua, irmã deles.
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
Os filhos de Japhlet: Pasach, Bimhal, e Ashvath. Estes são os filhos de Japhlet.
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
Os filhos de Shemer: Ahi, Rohgah, Jehubbah, e Aram.
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
Os filhos de Helem, seu irmão: Zophah, Imna, Shelesh, e Amal.
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
Os filhos de Zophah: Suah, Harnepher, Shual, Beri, Imrah,
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bezer, Hod, Shamma, Shilshah, Ithran, e Beera.
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
Os filhos de Jether: Jephunneh, Pispa, e Ara.
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
Os filhos de Ulla: Arah, Hanniel, e Rizia.
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
Todos estes foram os filhos de Asher, chefes das casas dos pais, escolhidos e poderosos homens de valor, chefes dos príncipes. O número deles listados por genealogia para o serviço na guerra foi de vinte e seis mil homens.

< 1 Nyakati 7 >