< 1 Nyakati 7 >

1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
Or les fils d’Issachar furent: Thola et Phua, Jasub et Siméron; quatre.
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
Les fils de Thola: Ozi, Raphaïa, Jériel, Jémaï, Jebsem et Samuel, princes dans les maisons de leurs familles. C’est de la race de Thola que, dans les jours de David, furent dénombrés des hommes très braves, au nombre de vingt-deux mille six cents.
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
Les fils d’Ozi: Izrahia, duquel naquirent Michaël, Obadia, Johel et Jésia, tous cinq princes.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
Et il y avait avec eux, dans leurs familles et leurs peuples, prêts au combat, des hommes très braves, au nombre de trente-six mille, car ils eurent beaucoup de femmes et d’enfants.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
Leurs frères aussi, dans toute la parenté d’Issachar, étaient très vigoureux pour combattre; il y en eut quatre-vingt-sept mille de dénombrés.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
Les fils de Benjamin furent Béla, Béchor et Jadihel; trois,
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
Les fils de Béla: Esbon, Ozi, Oziel, Jérimoth et Uraï; cinq princes de familles, et très vigoureux pour combattre: or leur nombre fut de vingt-deux mille et trente-quatre;
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
Les fils de Béchor: Zamira, Joas, Eliézer, Elioénaï, Amri, Jérimoth, Abia, Anathoth et Almath: tous ceux-là furent fils de Béchor.
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
Or on en dénombra, selon leurs familles, comme princes dans leur parenté, très braves pour les combats, vingt mille et deux cents.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
De plus, les fils de Jadihel: Balan; et les fils de Balan: Jéhus, Benjamin, Aod, Chanana, Zéthan, Tharsis et Ahisahar,
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
Tous ceux-là furent fils de Jadihel, princes dans leur parenté, hommes très braves, au nombre de dix-sept mille et deux cents, marchant aux combats.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
Sépham aussi et Hapham furent les fils de Hir; et Hasim, les fils d’Aher;
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
Mais les fils de Nephthali: Jasiel, Guni, Jéser et Sellum, fils de Bala.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
Or le fils de Manassé fut Esriel; et sa femme du second rang, la Syrienne, enfanta Machir, père de Galaad.
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
Et Machir prit des femmes pour ses fils Happhim et Saphan; et il eut une sœur du nom de Maacha; mais le nom du second fut Salphaad; et il naquit à Salphaad des filles.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
Et Maacha, femme de Machir, enfanta un fils qu’elle appela du nom de Pharès: or le nom du frère de Pharès fut Sarès, et les fils de Sarès: Ulam et Récen.
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
Mais le fils d’Ulam fut Badan; ceux-là sont les fils de Galaad, fils de Machir, fils de Manassé.
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
Sa sœur. Reine, enfanta Homme-beau, et Abiézer et Mohola.
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
Et les fils de Sémida étaient Ahir, Séchem, Léci et Aniam;
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Mais les fils d’Ephraïm: Suthala, Bared, son fils, Thahath, son fils, Elada, son fils, Thahath, son fils, le fils de celui-ci, Zabad,
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
Elle fils de celui-ci, Suthala, et le fils de celui-ci, Ezer, ainsi qu’Elad; mais les hommes indigènes de Geth les tuèrent, parce qu’ils étaient descendus pour envahir leurs possessions.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
C’est pourquoi Ephraïm, leur père, les pleura pendant un grand nombre de jours; et ses frères vinrent pour le consoler.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
Et il s’approcha de sa femme, qui conçut et eut un fils, et qui l’appela du nom de Béria, parce qu’il était né au milieu des maux de sa maison.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
Mais sa fille fut Sara, qui bâtit Béthoron la Basse et la Haute, et Ozensara.
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
Il eut encore pour fils, Rapha, Réseph, et Thalé, duquel naquit Thaan,
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Qui engendra Laadan; et le fils de celui-ci fut Ammiud, qui engendra Elizama,
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Duquel est né Nun, qui eut pour fils Josué.
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
Leur possession et leur habitation furent Béthel avec ses filles, Noran, contre l’orient, et contre le côté occidental. Gazer et ses filles, comme aussi Sichem avec ses filles, jusqu’à Aza avec ses filles.
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
Leur possession fut aussi, près des fils de Manassé, Bethsan et ses filles, Thanach et ses filles, Mageddo et ses filles, Dor et ses filles: c’est en ces lieux qu’habitèrent les fils de Joseph, fils d’Israël.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
Les fils d’Aser furent Jemna, Jésua, Jessui et Baria, et Sara était leur sœur;
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
Mais les fils de Bari: Heber et Melchiel: c’est lui qui est père de Barsaïth.
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
Or Héber engendra Jephlat, Somer et Hotham, et Suaa, leur sœur.
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
Les fils de Jéphlat furent Phosech, Chamaal et Asoth; ce sont là les fils de Jéphlat.
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
Mais les fils de Somer: Ahi, Roaga, Haba et Aram.
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
Et les fils d’Hélem, son frère: Supha, Jemna, Sellès et Amal.
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
Les fils de Supha: Sué, Harnapher, Sual, Béri et Jamra,
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bosor, Hod, Samma, Salusa, Jéthran et Béra.
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
Les fils de Jéther: Jéphoné, Phaspha et Ara.
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
Et les fils d’Olla: Arée, Haniel et Résia.
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
Tous ceux-là sont les fils d’Aser, et les princes des familles, chefs distingués et les plus braves des chefs: le nombre de ceux d’un âge propre à la guerre était de vingt-six mille.

< 1 Nyakati 7 >