< 1 Nyakati 7 >
1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
Des fils d'Issachar: Tola, Puah, Jashub et Shimron, quatre.
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
Fils de Tola: Uzzi, Rephaja, Jeriel, Jahmaï, Ibsam et Shemuel, chefs des maisons de leurs pères, de Tola; hommes vaillants dans leurs générations. Leur nombre, du temps de David, était de vingt-deux mille six cents.
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
Fils d'Uzzi: Jizrachia. Fils de Jizrachiah: Micaël, Abdias, Joël et Jischja, au nombre de cinq; tous étaient des chefs.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
Avec eux, selon leurs générations, selon les maisons de leurs pères, il y avait des troupes pour la guerre, au nombre de trente-six mille; car ils avaient beaucoup de femmes et de fils.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
Leurs frères, parmi toutes les familles d'Issacar, hommes vaillants, tous enregistrés selon leur généalogie, étaient quatre-vingt-sept mille.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
Fils de Benjamin: Bela, Becher et Jediael, trois.
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
Fils de Béla: Ezbon, Uzzi, Uzziel, Jerimoth et Iri, cinq; chefs de maisons paternelles, vaillants hommes; ils étaient au nombre de vingt-deux mille trente-quatre par généalogie.
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
Fils de Becher: Zemirah, Joas, Eliezer, Eliœnai, Omri, Jeremoth, Abijah, Anathoth et Alemeth. Tous ceux-là étaient les fils de Bécher.
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
Ils furent classés par généalogie, selon leurs générations, chefs des maisons de leurs pères, vaillants hommes, au nombre de vingt mille deux cents.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
Fils de Jediaël: Bilhan. Fils de Bilhan: Jeush, Benjamin, Ehud, Chenaana, Zethan, Tarsis et Ahishahar.
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
Tous ceux-là étaient fils de Jediaël, selon les chefs de famille de leurs pères, hommes vaillants, au nombre de dix-sept mille deux cents, aptes à aller à l'armée pour la guerre.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
Il en était de même de Shuppim, de Huppim, des fils de Ir, de Hushim et des fils de Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
Fils de Nephtali: Jahziel, Guni, Jezer, Shallum, et les fils de Bilha.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
Fils de Manassé: Asriel, qu'a porté sa concubine l'Aramitesse. Elle enfanta Makir, père de Galaad.
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
Machir prit une femme de Huppim et de Shuppim, dont la sœur s'appelait Maaca. Le nom de la seconde était Zelophehad; et Zelophehad eut des filles.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
Maaca, femme de Makir, enfanta un fils, qu'elle appela Peresh. Le nom de son frère était Sheresh; ses fils étaient Ulam et Rakem.
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
Fils d'Ulam: Bedan. Ce sont là les fils de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé.
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
Sa sœur Hammolecheth enfanta Ishhod, Abiezer et Mahla.
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
Les fils de Shemida furent: Ahian, Sichem, Likhi et Aniam.
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
Fils d'Ephraïm: Shuthelah, Bered, son fils, Tahath, son fils, Eleada, son fils, Tahath, son fils,
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
Zabad, son fils, Shuthelah, son fils, Ezer et Elead, que les hommes de Gath, nés dans le pays, tuèrent, parce qu'ils étaient descendus pour prendre leurs troupeaux.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
Ephraïm, leur père, fut longtemps dans le deuil, et ses frères vinrent le consoler.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
Il alla vers sa femme; elle conçut et enfanta un fils, qu'il appela Beriah, parce qu'il y avait du trouble dans sa maison.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
Sa fille était Schéérah, qui bâtit Beth Horon le bas et le haut, et Uzzen Schéérah.
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
Il eut pour fils Repha, pour fils Resheph, pour fils Telah, pour fils Tahan, pour fils
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Ladan, pour fils Ammihud, pour fils Elishama, pour fils
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Nun, pour fils et Josué, pour fils.
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
Leurs possessions et leurs établissements étaient Béthel et ses villes, à l'orient Naaran, à l'occident Guézer et ses villes, Sichem et ses villes, jusqu'à Azza et ses villes,
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
et, sur le territoire des fils de Manassé, Beth-Shean et ses villes, Taanac et ses villes, Meguiddo et ses villes, Dor et ses villes. Les enfants de Joseph, fils d'Israël, habitèrent dans ces localités.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
Fils d'Asher: Imnah, Ishvah, Ishvi et Beriah. Sérah était leur sœur.
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
Fils de Beria: Héber et Malkiel, qui fut le père de Birzaith.
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
Héber engendra Japhlet, Shomer, Hotham et Shua, leur sœur.
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
Fils de Japhlet: Pasach, Bimhal et Ashvath. Ce sont les fils de Japhlet.
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
Fils de Shemer: Ahi, Rohga, Jehubba et Aram.
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
Fils de Helem, son frère: Zopha, Imna, Shelesh et Amal.
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
Fils de Zopha: Sua, Harnépher, Schual, Beri, Imrah,
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bezer, Hod, Shamma, Schilsha, Ithran et Beera.
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
Fils de Jéther: Jephunné, Pispa et Ara.
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
Fils d'Ulla: Arach, Hanniel et Rizia.
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
Tous ceux-là étaient les fils d'Aser, chefs des maisons paternelles, hommes de choix et vaillants, chefs des princes. Le nombre de ceux qui étaient inscrits sur les listes généalogiques pour servir à la guerre était de vingt-six mille hommes.