< 1 Nyakati 7 >
1 Wana wa Isakari walikuwa: Tola, Pua, Yashubu na Shimroni; wote ni wanne.
And to [the] sons of Issachar Tola and Puah (Jashub *Q(K)*) and Shimron four.
2 Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yahmai, Ibsamu na Shemueli waliokuwa viongozi wa jamaa zao. Wakati wa utawala wa Mfalme Daudi, wazao wa Tola walioorodheshwa kama wapiganaji katika ukoo wao walikuwa watu 22,600.
And [the] sons of Tola Uzzi and Rephaiah and Jeriel and Jahmai and Jibsam and Samuel chiefs of [the] house of ancestors their of Tola mighty [men] of strength to generations their number their in [the] days of David [was] twenty and two thousand and six hundred.
3 Mwana wa Uzi alikuwa: Izrahia. Wana wa Izrahia walikuwa: Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia. Wote hawa watano walikuwa wakuu wao.
And [the] sons of Uzzi Izrahiah and [the] sons Izrahiah Michael and Obadiah and Joel Isshiah five chiefs all of them.
4 Kulingana na ukoo wa jamaa zao, walikuwa na watu hodari wa vita wapatao 36,000, kwa sababu walikuwa na wanawake na watoto wengi.
And with them to generations their of [the] house of ancestors their troops of war of warfare thirty and six thousand for they had many wives and sons.
5 Jamaa ya watu waliokuwa wapiganaji hodari kutoka koo zote za Isakari, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, jumla yao walikuwa 87,000.
And relatives their to all [the] clans of Issachar mighty [men] of strength [was] eighty and seven thousand recording genealogy they of everyone.
6 Wana watatu wa Benyamini walikuwa: Bela, Bekeri na Yediaeli.
Benjamin Bela and Beker and Jediael three.
7 Wana wa Bela walikuwa: Esboni, Uzi, Uzieli, Yeremothi na Iri; walikuwa viongozi wa jamaa zao; wote ni watano. Watu wapiganaji walioorodheshwa katika ukoo wao walikuwa 22,034.
And [the] sons of Bela Ezbon and Uzzi and Uzziel and Jerimoth and Iri five chiefs of a house of ancestors mighty [men] of strength and recording genealogy they [was] twenty and two thousand and thirty and four.
8 Wana wa Bekeri walikuwa: Zemira, Yoashi, Eliezeri, Elioenai, Omri, Yeremothi, Abiya, Anathothi na Alemethi. Hawa wote walikuwa wana wa Bekeri.
And [the] sons of Beker Zemirah and Joash and Eliezer and Elioenai and Omri and Jeremoth and Abijah and Anathoth and Alemeth all these [were] [the] sons of Beker.
9 Orodha ya ukoo wao iliyoandikwa viongozi wa jamaa zao walikuwa wapiganaji 20,200.
And recording genealogy they to generations their chiefs of [the] house of ancestors their mighty [men] of strength [was] twenty thousand and two hundred.
10 Mwana wa Yediaeli alikuwa: Bilhani. Wana wa Bilhani walikuwa: Yeushi, Benyamini, Ehudi, Kenaana, Zethani, Tarshishi na Ahishahari.
And [the] sons of Jediael Bilhan and [the] sons of Bilhan (Jeush *Q(K)*) and Benjamin and Ehud and Kenaanah and Zethan and Tarshish and Ahishahar.
11 Hawa wana wote wa Yediaeli walikuwa viongozi wa jamaa zao. Kulikuwako wanaume wapiganaji 17,200 waliokuwa tayari kwenda vitani.
All these [were] [the] sons of Jediael to [the] chiefs of the fathers mighty [men] of strength seven-teen thousand and two hundred [those who] went forth of war for battle.
12 Washupimu na Wahupimu walikuwa wazao wa Iri. Wahushimu walikuwa wazao wa Aheri.
And Shuppim and Huppim [were] [the] sons of Ir Hushim [were] [the] sons of Aher.
13 Wana wa Naftali walikuwa: Yahzieli, Guni, Yeseri na Shalumu; hao walikuwa wazao wa Bilha.
[the] sons of Naphtali Jahziel and Guni and Jezer and Shallum [the] sons of Bilhah.
14 Wana wa Manase walikuwa: Asirieli alikuwa mzao wake kutokana na suria wake wa Kiaramu. Huyu suria akamzaa Makiri baba wa Gileadi.
[the] sons of Manasseh Asriel whom she bore concubine his Aramean she bore Makir [the] father of Gilead.
15 Makiri akatwaa mke kutoka miongoni mwa Wahupimu na Washupimu. Jina la dada yake aliitwa Maaka. Mwana wa pili wa Makiri aliitwa Selofehadi, ambaye alikuwa na wasichana tu.
And Makir he took a wife for Huppim and for Shuppim and [the] name of sister his [was] Maacah and [the] name of the second [son] [was] Zelophehad and they belonged to Zelophehad daughters.
16 Maaka mkewe Makiri akamzaa mwana aliyemwita Pereshi. Jina la nduguye lilikuwa Shereshi. Wana wa Pereshi walikuwa Ulamu na Rakemu.
And she bore Maacah [the] wife of Makir a son and she called name his Peresh and [the] name of brother his Sheresh and sons his [were] Ulam and Rekem.
17 Mwana wa Ulamu alikuwa: Bedani. Hawa ndio waliokuwa wana wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase.
And [the] sons of Ulam Bedan these [were] [the] descendants of Gilead [the] son of Makir [the] son of Manasseh.
18 Dada yake aliyeitwa Hamolekethi aliwazaa Ish-Hodi, Abiezeri na Mahla.
And sister his Hammoleketh she bore Ishhod and Abiezer and Mahlah.
19 Wana wa Shemida walikuwa: Ahiani, Shekemu, Liki na Aniamu.
And they were [the] sons of Shemida Ahian and Shechem and Likhi and Aniam.
20 Wana wa Efraimu walikuwa: Shuthela, ambaye alimzaa Beredi, Beredi akamzaa Tahathi, Tahathi akazaa Eleada, Eleada akamzaa Tahathi,
And [the] descendants of Ephraim Shuthelah and Bered son his and Tahath son his and Eleadah son his and Tahath son his.
21 Tahathi akamzaa Zabadi, na Zabadi akamzaa Shuthela. Ezeri na Eleadi waliuawa na wenyeji wa Gathi walipokuwa wamekwenda huko kuwanyangʼanya mifugo yao.
And Zabad son his and Shuthelah son his and Ezer and Elead and they killed them [the] men of Gath who were born in the land for they went down to take livestock their.
22 Baba yao Efraimu akawaombolezea kwa siku nyingi, na jamaa zake wakaja kumfariji.
And he mourned Ephraim father their days many and they came brothers his to comfort him.
23 Kisha akakutana kimwili na mke wake tena, naye akachukua mimba, akamzalia mwana. Akamwita Beria, kwa sababu ya misiba iliyoipata nyumba yake.
And he went into wife his and she conceived and she bore a son and he called name his Beriah for in distress it was in house his.
24 Beria alikuwa na binti jina lake Sheera. Huyu ndiye aliijenga miji ya Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, pamoja na Uzen-Sheera.
And daughter his [was] Sheerah and she built Beth Horon lower and upper and Uzzen Sheerah.
25 Beria akamzaa pia Refa, naye Refa akamzaa Reshefu, Reshefu akamzaa Tela, Tela akamzaa Tahani,
And Rephah son his and Resheph (son his *X*) and Telah son his and Tahan son his.
26 Tahani akamzaa Ladani, Ladani akamzaa Amihudi, Amihudi akamzaa Elishama,
Ladan son his Ammihud son his Elishama son his.
27 Elishama akamzaa Nuni, Nuni akamzaa Yoshua.
Nun son his Joshua son his.
28 Nchi zao na makazi yao yalijumuisha Betheli na vijiji vilivyouzunguka, Naarani ilikuwa upande wa mashariki, Gezeri pamoja na vijiji vyake upande wa magharibi, pia Shekemu na vijiji vyake hadi kufikia Aya na vijiji vyake.
And possession their and dwelling places their [were] Beth-el and daughters its and to the east Naaran and to the west Gezer and daughters its and Shechem and daughters its to Ayyah and daughters its.
29 Katika mipaka ya Manase walikuwepo Beth-Shani, Taanaki, Megido na Dori pamoja na vijiji vyake. Wana wa Yosefu mwana wa Israeli waliishi katika miji hii.
And on [the] hands of [the] descendants of Manasseh Beth Shan and daughters its Taanach and daughters its Megiddo and daughters its Dor and daughters its in these they dwelt [the] descendants of Joseph [the] son of Israel.
30 Wana wa Asheri walikuwa: Imna, Ishva, Ishvi na Beria. Dada yao alikuwa Sera.
[the] sons of Asher Imnah and Ishvah and Ishvi and Beriah and Serah [was] sister their.
31 Wana wa Beria walikuwa: Heberi na Malkieli, aliyekuwa baba yake Birzaithi.
And [the] sons of Beriah Heber and Malkiel he [was] [the] father (Birzaith. *Q(K)*)
32 Heberi akawazaa Yafleti, Shomeri na Hothamu, na Shua dada yao.
And Heber he fathered Japhlet and Shomer and Hotham and Shua sister their.
33 Wana wa Yafleti walikuwa: Pasaki, Bimhali na Ashvathi. Hawa walikuwa wana wa Yafleti.
And [the] sons of Japhlet Pasach and Bimhal and Ashvath these [were] [the] sons of Japhlet.
34 Wana wa Shemeri walikuwa: Ahi, Roga, Yehuba na Aramu.
And [the] sons of Shemer Ahi (and Rohgah and Hubbah *Q(K)*) and Aram.
35 Wana wa Helemu ndugu yake walikuwa: Sofa, Imna, Sheleshi na Amali.
And [the] son of Helem brother his Zophah and Imna and Shelesh and Amal.
36 Wana wa Sofa walikuwa: Sua, Harneferi, Shuali, Beri, Imra,
[the] sons of Zophah Suah and Harnepher and Shual and Beri and Imrah.
37 Bezeri, Hodu, Shama, Shilsha, Ithrani na Beera.
Bezer and Hod and Shamma and Shilshah and Ithran and Beera.
38 Wana wa Yetheri walikuwa: Yefune, Pispa na Ara.
And [the] sons of Jether Jephunneh and Pispah and Ara.
39 Wana wa Ula walikuwa: Ara, Hanieli na Risia.
And [the] sons of Ulla Arah and Hanniel and Rizia.
40 Hawa wote ndio waliokuwa wazao wa Asheri, viongozi wa jamaa zao, watu bora, mashujaa walio hodari na viongozi maarufu. Idadi ya watu waliokuwa tayari kwa vita, kama ilivyoorodheshwa katika ukoo wao, walikuwa 26,000.
All these [were] [the] descendants of Asher [the] chiefs of [the] house of the ancestors chosen mighty [men] of strength [the] chiefs of the leaders and recording genealogy they in the army in battle number their [was] men twenty and six thousand.