< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
בני לוי גרשון קהת ומררי
2 Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
ובני קהת--עמרם יצהר וחברון ועזיאל
3 Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
ובני עמרם אהרן ומשה ומרים ובני אהרן--נדב ואביהוא אלעזר ואיתמר
4 Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
אלעזר הוליד את פינחס פינחס הליד את אבישוע
5 Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
ואבישוע הוליד את בקי ובקי הוליד את עזי
6 Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
ועזי הוליד את זרחיה וזרחיה הוליד את מריות
7 Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
מריות הוליד את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב
8 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את אחימעץ
9 Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
ואחימעץ הוליד את עזריה ועזריה הוליד את יוחנן
10 Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
ויוחנן הוליד את עזריה הוא אשר כהן בבית אשר בנה שלמה בירושלם
11 Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
ויולד עזריה את אמריה ואמריה הוליד את אחיטוב
12 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
ואחיטוב הוליד את צדוק וצדוק הוליד את שלום
13 Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
ושלום הוליד את חלקיה וחלקיה הוליד את עזריה
14 Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
ועזריה הוליד את שריה ושריה הוליד את יהוצדק
15 Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
ויהוצדק הלך--בהגלות יהוה את יהודה וירושלם ביד נבכדנאצר
16 Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
בני לוי גרשם קהת ומררי
17 Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
ואלה שמות בני גרשום לבני ושמעי
18 Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
ובני קהת--עמרם ויצהר וחברון ועזיאל
19 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
בני מררי מחלי ומשי ואלה משפחות הלוי לאבתיהם
20 Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
לגרשום--לבני בנו יחת בנו זמה בנו
21 Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
יואח בנו עדו בנו זרח בנו יאתרי בנו
22 Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
בני קהת--עמינדב בנו קרח בנו אסיר בנו
23 Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
אלקנה בנו ואביסף בנו ואסיר בנו
24 Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
תחת בנו אוריאל בנו עזיה בנו ושאול בנו
25 Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
ובני אלקנה--עמשי ואחימות
26 Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
אלקנה--בנו (בני) אלקנה צופי בנו ונחת בנו
27 Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
אליאב בנו ירחם בנו אלקנה בנו
28 Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
ובני שמואל הבכר ושני ואביה
29 Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
בני מררי מחלי לבני בנו שמעי בנו עזה בנו
30 Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
שמעא בנו חגיה בנו עשיה בנו
31 Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
ואלה אשר העמיד דויד על ידי שיר--בית יהוה ממנוח הארון
32 Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
ויהיו משרתים לפני משכן אהל מועד בשיר עד בנות שלמה את בית יהוה בירושלם ויעמדו כמשפטם על עבודתם
33 Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
ואלה העמדים ובניהם מבני הקהתי--הימן המשורר בן יואל בן שמואל
34 mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
בן אלקנה בן ירחם בן אליאל בן תוח
35 mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
בן ציף (צוף) בן אלקנה בן מחת בן עמשי
36 mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
בן אלקנה בן יואל בן עזריה בן צפניה
37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
בן תחת בן אסיר בן אביסף בן קרח
38 mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
בן יצהר בן קהת בן לוי בן ישראל
39 na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
ואחיו אסף העמד על ימינו--אסף בן ברכיהו בן שמעא
40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
בן מיכאל בן בעשיה בן מלכיה
41 mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
בן אתני בן זרח בן עדיה
42 mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
בן איתן בן זמה בן שמעי
43 mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
בן יחת בן גרשם בן לוי
44 Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
ובני מררי אחיהם על השמאול--איתן בן קישי בן עבדי בן מלוך
45 mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
בן חשביה בן אמציה בן חלקיה
46 mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
בן אמצי בן בני בן שמר
47 mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
בן מחלי בן מושי בן מררי בן לוי
48 Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
ואחיהם הלוים נתונים--לכל עבודת משכן בית האלהים
49 Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
ואהרן ובניו מקטירים על מזבח העולה ועל מזבח הקטרת לכל מלאכת קדש הקדשים ולכפר על ישראל ככל אשר צוה משה עבד האלהים
50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
ואלה בני אהרן--אלעזר בנו פינחס בנו אבישוע בנו
51 Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
בקי בנו עזי בנו זרחיה בנו
52 Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
מריות בנו אמריה בנו אחיטוב בנו
53 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
צדוק בנו אחימעץ בנו
54 Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
ואלה מושבותם לטירותם בגבולם--לבני אהרן למשפחת הקהתי כי להם היה הגורל
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
ויתנו להם את חברון בארץ יהודה ואת מגרשיה סביבתיה
56 Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
ואת שדה העיר ואת חצריה--נתנו לכלב בן יפנה
57 Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
ולבני אהרן נתנו את ערי המקלט--את חברון ואת לבנה ואת מגרשיה ואת יתר ואת אשתמע ואת מגרשיה
58 Hileni, Debiri,
ואת חילז ואת מגרשיה את דביר ואת מגרשיה
59 Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת עשן ואת מגרשיה ואת בית שמש ואת מגרשיה
60 Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
וממטה בנימן את גבע ואת מגרשיה ואת עלמת ואת מגרשיה ואת ענתות ואת מגרשיה כל עריהם שלש עשרה עיר במשפחותיהם
61 Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
ולבני קהת הנותרים ממשפחת המטה ממחצית מטה חצי מנשה בגורל--ערים עשר
62 Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
ולבני גרשום למשפחותם ממטה יששכר וממטה אשר וממטה נפתלי וממטה מנשה בבשן--ערים שלש עשרה
63 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
לבני מררי למשפחותם ממטה ראובן וממטה גד וממטה זבלון בגורל--ערים שתים עשרה
64 Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
ויתנו בני ישראל ללוים את הערים ואת מגרשיהם
65 Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
ויתנו בגורל ממטה בני יהודה וממטה בני שמעון וממטה בני בנימן--את הערים האלה אשר יקראו אתהם בשמות
66 Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
וממשפחות בני קהת--ויהי ערי גבולם ממטה אפרים
67 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
ויתנו להם את ערי המקלט את שכם ואת מגרשיה--בהר אפרים ואת גזר ואת מגרשיה
68 Yokmeamu, Beth-Horoni,
ואת יקמעם ואת מגרשיה ואת בית חורון ואת מגרשיה
69 Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת אילון ואת מגרשיה ואת גת רמון ואת מגרשיה
70 Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממחצית מטה מנשה את ענר ואת מגרשיה ואת בלעם ואת מגרשיה--למשפחת לבני קהת הנותרים
71 Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
לבני גרשום--ממשפחת חצי מטה מנשה את גולן בבשן ואת מגרשיה ואת עשתרות ואת מגרשיה
72 Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
וממטה יששכר את קדש ואת מגרשיה את דברת ואת מגרשיה
73 Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת ראמות ואת מגרשיה ואת ענם ואת מגרשיה
74 Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
וממטה אשר את משל ואת מגרשיה ואת עבדון ואת מגרשיה
75 Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת חוקק ואת מגרשיה ואת רחב ואת מגרשיה
76 Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
וממטה נפתלי את קדש בגליל ואת מגרשיה ואת חמון ואת מגרשיה ואת קריתים ואת מגרשיה
77 Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
לבני מררי הנותרים--ממטה זבלון את רמונו ואת מגרשיה את תבור ואת מגרשיה
78 Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
ומעבר לירדן ירחו למזרח הירדן--ממטה ראובן את בצר במדבר ואת מגרשיה ואת יהצה ואת מגרשיה
79 Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת קדמות ואת מגרשיה ואת מיפעת ואת מגרשיה
80 Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
וממטה גד--את ראמות בגלעד ואת מגרשיה ואת מחנים ואת מגרשיה
81 Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.
ואת חשבון ואת מגרשיה ואת יעזיר ואת מגרשיה

< 1 Nyakati 6 >