< 1 Nyakati 6 >

1 Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
Les fils de Lévi furent Gerson, Caath et Mérari;
2 Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Les fils de Caath, Amram, Isaar, Hébron et Oziel;
3 Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Les fils d’Amram, Aaron, Moïse et Marie; les fils d’Aaron Nadab et Abiu, Eléazar et Ithamar.
4 Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
Eléazar engendra Phinéès, et Phinéès engendra Abisué.
5 Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
Abisué engendra Bocci, et Bocci engendra Ozi.
6 Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
Ozi engendra Zaraïas, et Zaraïas engendra Méraïoth.
7 Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
Méraïoth engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
8 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Achimaas.
9 Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
Achimaas engendra Azarias, Azarias engendra Johanan.
10 Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
Johanan engendra Azarias: ce fut lui qui remplit les fonctions du sacerdoce dans la maison que bâtit Salomon à Jérusalem.
11 Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
Or Azarias engendra Amarias, et Amarias engendra Achitob.
12 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
Achitob engendra Sadoc, et Sadoc engendra Sellum.
13 Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
Sellum engendra Helcias, et Helcias engendra Azarias.
14 Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
Azarias engendra Saraïas, et Saraïas engendra Josédec.
15 Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
Or Josédec sortit du pays, quand le Seigneur déporta Juda et Jérusalem par l’entremise de Nabuchodonosor.
16 Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
Les fils de Lévi furent donc Gerson, Caath et Mérari;
17 Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
Les fils de Gerson, Lobni et Séméi;
18 Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Les fils de Caath, Amram, Isaar, Hébron et Oziel;
19 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
Les fils de Mérari, Moholi et Musi. Mais voici la parenté des enfants de Lévi, selon leurs familles:
20 Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
Gerson, dont le fils, Lobni, dont le fils, Jahath, dont le fils, Zamma,
21 Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
Dont le fils, Joab, dont le fils, Addo, dont le fils, Zara, dont le fils, Jethraï;
22 Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
Les fils de Caath: Aminadab, son fils, dont le fils, Coré, dont le fils Asir,
23 Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
Dont le fils, Elcana, dont le fils, Abiasaph, dont le fils, Asir,
24 Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
Dont le fils, Thahath, dont le fils, Uriel, dont le fils, Ozias, dont le fils, Saül.
25 Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
Les fils d’Elcana: Amasaï, Achimoth,
26 Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
Et Elcana; les fils d’Elcana: Sophaï, son fils, dont le fils, Nahath,
27 Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
Dont le fils, Eliab, dont le fils, Jéroham, dont le fils, Elcana.
28 Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
Les fils de Samuel: le premier-né, Vasseni, et Abia;
29 Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
Mais les fils de Mérari, Moholi, dont le fils, Lobni, dont le fils, Séméi, dont le fils, Oza,
30 Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
Dont le fils, Sammaa, dont le fils, Haggia, dont le fils, Asaïa.
31 Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
Voilà ceux que David établit sur les chantres de la maison du Seigneur, depuis que l’arche eut été placée.
32 Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
Et ils servaient devant le tabernacle de témoignage, chantant, jusqu’à ce que Salomon eût bâti la maison du Seigneur dans Jérusalem; mais ils exerçaient ce ministère suivant leur rang.
33 Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
Or voici ceux qui servaient avec leurs fils d’entre les fils de Caath: Héman, le chantre, fils de Johel, fils de Samuel,
34 mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
Fils d’Elcana, fils de Jéroham, fils d’Eliel, fils de Thohu,
35 mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
Fils de Suph, fils d’Elcana, fils de Mahath, fils d’Amasa,
36 mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
Fils d’Elcana, fils de Joël, fils d’Azarias, fils de Sophonias,
37 mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
Fils de Thahath, fils d’Asir, fils d’Abiasaph, fils de Coré,
38 mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
Fils d’Isaar, fils de Caath, fils de Lévi, fils d’Israël.
39 na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
Et son frère Asaph, qui se tenait à sa droite; Asaph, fils de Barachias, fils de Samaa,
40 mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
Fils de Michaël, fils de Basaïas, fils de Melchias,
41 mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
Fils d’Athanaï, fils de Zara, fils d’Adaïa,
42 mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
Fils d’Ethan, fils de Zamma, fils de Séméi,
43 mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
Fils de Jeth, fils de Gerson, fils de Lévi;
44 Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
Mais les fils de Mérari, leurs frères, qui se tenaient à la gauche, étaient: Ethan, fils de Cusi, fils d’Abdi, fils de Maloch,
45 mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
Fils d’Hasabias, fils d’Amasias, fils d’Helcias,
46 mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
Fils d’Amasaï, fils de Boni, fils de Somer,
47 mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
Fils de Moholi, fils de Musi, fils de Mérari, fils de Lévi.
48 Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
Les Lévites, leurs frères, étaient aussi désignés pour tout le service du tabernacle de la maison du Seigneur.
49 Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
Mais Aaron et ses fils offraient ce qui se brûle sur l’autel de l’holocauste et sur l’autel du parfum, pour toute l’œuvre du Saint des Saints, et afin qu’ils priassent pour Israël, selon tout ce qu’avait ordonné Moïse, serviteur de Dieu.
50 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
Or ceux-ci sont les fils d’Aaron: Eléazar, son fils, dont le fils, Phinéès, dont le fils, Abisué,
51 Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
Dont le fils, Bocci, dont le fils, Ozi, dont le fils, Zaraïas,
52 Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
Dont le fils, Méraïoth, dont le fils, Amarias, dont le fils, Achitob,
53 Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
Dont le fils, Sadoc, dont le fils Achimaas.
54 Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
Et voici leurs habitations dans les bourgs et les environs, c’est-à-dire les habitations des enfants d’Aaron, selon les familles des Caathites; car c’est à eux qu’elles étaient échues par le sort.
55 Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
On leur donna donc Hébron, dans la terre de Juda, et ses faubourgs tout autour;
56 Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
Mais les campagnes de la ville et les villages, on les donna à Caleb, fils de Jéphoné.
57 Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
Quant aux fils d’Aaron, on leur donna les villes de refuge, Hébron, et Lobna et ses faubourgs;
58 Hileni, Debiri,
Jéther aussi et Esthémo, avec leurs faubourgs; et même Hélon et Dabir, avec leurs faubourgs,
59 Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
Et encore Asan et Bethsémès, et leurs faubourgs;
60 Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
Et de la tribu de Benjamin, Gabée et ses faubourgs, Almath avec ses faubourgs, comme aussi Anathoth avec ses faubourgs; en tout, treize villes, selon leurs familles.
61 Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
Mais aux enfants de Caath, qui restaient de sa famille, on donna en possession, sur la demi-tribu de Manassé, dix villes;
62 Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
Et aux enfants de Gersom, selon leurs familles, sur la tribu d’Issachar, sur la tribu d’Aser, sur la tribu de Nephthali, et sur la tribu de Manassé, en Basan, treize villes.
63 Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
Quant aux enfants de Mérari, on leur donna par le sort, selon leurs familles, sur la tribu de Ruben, sur la tribu de Gad, et sur la tribu de Zabulon, douze villes.
64 Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
Ainsi les enfants d’Israël donnèrent aux Lévites ces villes et leurs faubourgs;
65 Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
Et ils donnèrent par le sort sur la tribu des enfants de Juda, et sur la tribu des enfants de Siméon, et sur la tribu des enfants de Benjamin, ces mêmes villes qu’ils appelèrent de leurs noms,
66 Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
Et pour ceux qui étaient de la famille des enfants de Caath, il y eut des villes dans leur territoire de la tribu d’Ephraïm.
67 Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
Ils leur donnèrent donc j des villes de refuge, Sichem avec ses faubourgs, dans la montagne d’Ephraïm, et Gazer avec ses faubourgs;
68 Yokmeamu, Beth-Horoni,
Jecmaam aussi avec ses faubourgs, et Béthoron également;
69 Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
En outre, Hélon avec ses faubourgs, et Gethremmon de la même manière.
70 Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Mais sur la demi-tribu de Manassé, Aner et ses faubourgs, et Baalam et ses faubourgs, furent donnés, savoir, à ceux qui restaient de la famille de Caath.
71 Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
Et aux enfants de Gersom, sur la famille de la demi-tribu de Manassé, ce fut Gaulon en Basan et ses faubourgs, et Astharoth avec ses faubourgs,
72 Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
Sur la tribu d’Issachar, Cédés et ses faubourgs, et Dabéreth avec ses faubourgs;
73 Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
Ramoth aussi et ses faubourgs, et Anem avec ses faubourgs;
74 Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
Mais sur la tribu d’Aser, Masal avec ses faubourgs, et Abdon également;
75 Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
Hucac aussi et ses faubourgs, et Rohob avec ses faubourgs;
76 Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
Mais sur la tribu de Nephthali, Cédés en Galilée et ses faubourgs, Hamon avec ses faubourgs, et Cariathaïm et ses faubourgs.
77 Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
De plus, aux enfants de Mérari, qui restaient encore, furent donnés, sur la tribu de Zabulon, Remmono et ses faubourgs, et Thabor avec ses faubourgs;
78 Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
Au delà du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho, contre l’orient du Jourdain, ce fut sur la tribu de Ruben: Bosor, dans le désert, avec ses faubourgs, et Jassa avec ses faubourgs;
79 Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
Cadémoth aussi et ses faubourgs, et Méphaat avec ses faubourgs;
80 Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
De même que sur la tribu de Gad, Ramoth en Galaad et ses faubourgs, et Manaïm avec ses faubourgs;
81 Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.
Et de plus, Hésébon avec ses faubourgs, et Jézer avec ses faubourgs.

< 1 Nyakati 6 >