< 1 Nyakati 5 >
1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Synowie Rubena, pierworodnego Izraela. Był on pierworodnym, ale ponieważ zbezcześcił łoże swego ojca, jego pierworództwo zostało dane synom Józefa, syna Izraela. Nie spisano więc rodowodu według pierworództwa.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Juda bowiem był najpotężniejszy wśród swoich braci i od niego pochodził władca, lecz pierworództwo [należało] do Józefa.
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Synami Rubena, pierworodnego Izraela, [byli]: Henoch, Pallu, Chesron i Karmi.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
Synowie Joela: jego syn Szemajasz, jego syn Gog, jego syn Szimei;
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Jego syn Micheasz, jego syn Reajasz, jego syn Baal;
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Jego syn Beera, którego Tiglat-Pileser, król Asyrii, wziął do niewoli. On był księciem Rubenitów.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Jego braćmi według swoich rodzin, gdy spisywano rodowody ich pokoleń, [byli] naczelnicy: Jejel, Zachariasz;
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
I Bela, syn Azaza, syna Szemy, syna Joela, który zamieszkiwał w Aroerze aż po Nebo i Baal-Meon.
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
A na wschodzie zamieszkiwał aż do wejścia na pustkowie od rzeki Eufrat. Ich stada bowiem pomnożyły się w ziemi Gilead.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Za czasów Saula prowadzili wojnę z Hagrytami, którzy zostali przez nich pokonani. Zamieszkali więc w ich namiotach w całej wschodniej [części] Gileadu.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
A synowie Gada mieszkali naprzeciw nich w ziemi Baszanu, aż [do] Salka.
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Joel [był] zwierzchnikiem, potem Szafam, następnie Janaj i Szafat w Baszanie.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
A ich braćmi według domów swoich ojców [byli]: Mikael, Meszullam, Szeba, Joraj, Jakan, Zija i Eber – siedmiu.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
Ci są synami Abichaila, syna Churiego, syna Jaroacha, syna Gileada, syna Mikaela, syna Jesziszaja, syna Jachdo, syna Buza;
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Achi, syn Abdiela, syna Guniego – głowa domu ich ojców.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
I mieszkali w Gileadzie, w Baszanie, w jego miasteczkach i na wszystkich pastwiskach Szaronu aż po ich krańce.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Wszyscy oni spisani zostali według rodowodów za czasów Jotama, króla Judy, i za czasów Jeroboama, króla Izraela.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
Synów Rubena i Gada oraz połowy pokolenia Manassesa, dzielnych wojowników zdolnych do noszenia tarczy i miecza i do strzelania z łuku i wyćwiczonych w boju, było czterdzieści cztery tysiące siedmiuset sześćdziesięciu wyruszających do bitwy.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
Oni prowadzili wojnę z Hagrytami, z Jeturem, z Nafiszem i Nodabem;
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
I otrzymali pomoc przeciwko nim. Wydano więc w ich ręce Hagrytów wraz ze wszystkimi, którzy z nimi byli. Podczas walki bowiem wołali do Boga, a [on] ich wysłuchał, bo pokładali w nim ufność.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
I zabrali z ich stad: pięćdziesiąt tysięcy wielbłądów, dwieście pięćdziesiąt tysięcy owiec, dwa tysiące osłów, a ludzi – sto tysięcy.
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
Wielu bowiem poległo, gdyż wojna ta [wyszła] od Boga. I mieszkali na ich miejscu aż do uprowadzenia do niewoli.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Ale synowie połowy pokolenia Manassesa mieszkali w tej ziemi i rozmnożyli się od Baszanu aż do Baal-Chermon i Seniru, i do góry Hermon.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
A oto [są] naczelnicy domów ich ojców: Efer, Jiszi, Eliel, Azriel, Jeremiasz, Hodawiasz i Jachdiel, dzielni wojownicy, ludzie sławni, naczelnicy domu swoich ojców.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Lecz zgrzeszyli przeciw Bogu swoich ojców i cudzołożyli, idąc za bogami narodów [tej] ziemi, które Bóg zniszczył przed nimi.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
Wtedy Bóg Izraela pobudził ducha Pula, króla Asyrii, i ducha Tiglat-Pilesera, króla Asyrii, i uprowadził Rubenitów i Gadytów oraz połowę pokolenia Manassesa i zaprowadził ich do Chalach, do Chabor, do Hara i do rzeki Gozan; [są tam] aż do dziś.