< 1 Nyakati 5 >

1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Fils de Ruben, premier-né d'Israël (car il était le premier-né; mais pour avoir souillé le lit de son père, son droit d'aînesse fut donné aux fils de Joseph, fils d'Israël, non toutefois pour être enregistré dans les généalogies, selon le droit d'aînesse.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Car Juda fut puissant parmi ses frères, et de lui est issu un prince; mais le droit d'aînesse est à Joseph).
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Fils de Ruben, premier-né d'Israël: Hénoc, Pallu, Hetsron et Carmi.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
Fils de Joël: Shémaja, son fils, Gog, son fils, Shimeï, son fils,
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Mica, son fils, Réaja, son fils, Baal, son fils,
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Béera, son fils, que Thilgath-Pilnéser, roi d'Assyrie, emmena captif. C'était un prince des Rubénites.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Ses frères, d'après leurs familles, au registre généalogique, selon leur naissance, étaient: le premier Jéïel; Zacharie;
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Béla, fils d'Azaz, fils de Shéma, fils de Joël. Béla habitait à Aroër, et jusqu'à Nébo et Baal-Méon;
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
A l'orient, il habitait jusqu'à l'entrée du désert, depuis le fleuve de l'Euphrate, car leurs troupeaux étaient nombreux au pays de Galaad.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Du temps de Saül, ils firent la guerre aux Hagaréniens, qui tombèrent entre leurs mains; et ils habitèrent dans leurs tentes, sur tout le côté oriental de Galaad.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Les enfants de Gad habitèrent vis-à-vis d'eux dans le pays de Bassan, jusqu'à Salca.
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Joël, le premier, Shapham, le second, Janaï et Shaphat en Bassan.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
Leurs frères, selon la maison de leurs pères: Micaël, Meshullam, Shéba, Joraï, Jaecan, Zia et Éber, sept.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
Ceux-ci sont les enfants d'Abichaïl, fils de Huri, fils de Jaroach, fils de Galaad, fils de Micaël, fils de Jeshishaï, fils de Jachdo, fils de Buz.
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Achi, fils d'Abdiel, fils de Guni, était le chef de la maison de leurs pères.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
Ils habitaient en Galaad, en Bassan, et dans les villes de leur ressort, et dans toutes les banlieues de Saron, jusqu'à leurs frontières.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Ils furent tous enregistrés dans les généalogies du temps de Jotham, roi de Juda, et du temps de Jéroboam, roi d'Israël.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
Les enfants de Ruben, les Gadites et la demi-tribu de Manassé, d'entre les vaillants hommes portant le bouclier et l'épée, tirant de l'arc, et instruits pour la guerre, étaient au nombre de quarante-quatre mille sept cent soixante, sortant en armée.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
Ils firent la guerre aux Hagaréniens, à Jétur, à Naphish et à Nodab.
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
Ils eurent du secours contre eux, et les Hagaréniens, et tous ceux qui étaient avec eux, furent livrés entre leurs mains; car, dans la bataille, ils crièrent à Dieu, et il les exauça, parce qu'ils avaient mis leur espérance en lui;
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
Et ils prirent leurs troupeaux: cinquante mille chameaux, deux cent cinquante mille brebis, deux mille ânes, et cent mille personnes.
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
Car il en tomba morts un grand nombre, parce que la bataille venait de Dieu; et ils habitèrent à leur place jusqu'à la déportation.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Les enfants de la demi-tribu de Manassé habitèrent dans le pays, depuis Bassan jusqu'à Baal-Hermon et à Sénir, et à la montagne de Hermon; ils étaient nombreux.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
Et voici les chefs des maisons de leurs pères: Épher, Jishéï, Éliel, Azriel, Jérémie, Hodavia et Jachdiel, vaillants hommes, gens de renom, chefs des maisons de leurs pères.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Mais ils péchèrent contre le Dieu de leurs pères, et ils se prostituèrent après les dieux des peuples du pays, que l'Éternel avait détruits devant eux.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
Et le Dieu d'Israël excita l'esprit de Pul, roi d'Assyrie, et l'esprit de Thilgath-Pilnéser, roi d'Assyrie, qui transporta les Rubénites, les Gadites et la demi-tribu de Manassé, et les emmena à Chalach, à Chabor, à Hara, et au fleuve de Gozan, où ils sont demeurés jusqu'à ce jour.

< 1 Nyakati 5 >