< 1 Nyakati 5 >
1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Fils de Ruben, premier-né d’Israël. — Car il était le premier-né; mais, parce qu’il souilla la couche de son père, son droit d’aînesse fut donné aux fils de Joseph, fils d’Israël, non, toutefois, pour que Joseph fût inscrit dans les généalogie comme premier-né.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Car Judas fut puissant parmi ses frères, et de lui est issu un prince. Mais le droit d’aînesse est à Joseph. —
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Fils de Ruben, premier-né d’Israël: Enoch, Phallu, Esron et Charmi.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
Fils de Joël: Samia, son fils; Gog, son fils; Séméï, son fils;
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Micha, son fils; Réïa, son fils; Baal, son fils;
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Bééra, son fils, que Thelgathphalnasar, roi d’Assyrie, emmena captif: il fut un des princes des Rubénites. —
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Frères de Bééra, chacun selon sa famille, tels qu’ils sont inscrits dans les généalogies selon leurs générations: le chef, Jéhiel; Zacharie;
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Bala, fils d’Azaz, fils de Samma, fils de Joël. Bala habitait à Aroër, et jusqu’à Nébo et à Béel-Méon;
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
à l’orient, il habitait jusqu’à l’entrée du désert, qui va depuis le fleuve de l’Euphrate, car leurs troupeaux étaient nombreux dans le pays de Galaad.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Du temps de Saül, ils firent la guerre aux Agaréens, qui tombèrent entre leurs mains, et ils habitèrent dans leurs tentes, sur tout le côté oriental de Galaad.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Les fils de Gad habitaient vis-à-vis d’eux dans le pays de Basan, jusqu’à Selcha.
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
C’étaient: le chef, Joël; le second, Saphan, puis Janaï et Saphath, en Basan.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
Leurs frères, d’après leurs maisons patriarcales, étaient: Michaël, Mosollam, Sébé, Joraï, Jachan, Zié et Héber: sept.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
Ils étaient fils d’Abihaïl, fils de Huri, fils de Jara, fils de Galaad, fils de Michaël, fils de Jésési, fils de Jeddo, fils de Buz.
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Achi, fils d’Abdiel, fils de Guni, était chef de leurs maisons patriarcales.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
Ils habitaient en Galaad, en Basan, et dans les villes de leurs dépendances, et dans tous les pâturages de Saron jusqu’à leurs extrémités.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Tous ces fils de Gad furent enregistrés dans les généalogies du temps de Joatham, roi de Juda, et du temps de Jéroboam, roi d’Israël.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
Les fils de Ruben, les Gadites et la demi-tribu de Manassé avaient de vaillants hommes, portant le bouclier et l’épée, tirant de l’arc, et exercés à la guerre, au nombre de quarante quatre mille sept cent soixante, en état d’aller à l’armée.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
Ils firent la guerre aux Agaréens, à Jéthur, à Naphis et à Nodab.
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
Ils furent aidés contre eux, et les Agaréens et tous ceux qui étaient avec eux furent livrés entre leurs mains. Car ils avaient crié vers Dieu pendant le combat, et il les avait exaucés, parce qu’ils s’étaient confiés en lui.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
Ils enlevèrent leurs troupeaux, cinquante mille chameaux, deux cent cinquante mille brebis, deux mille ânes, et cent mille personnes,
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
car il était tombé beaucoup de morts, parce que la guerre était de Dieu. Et ils s’établirent à leur place jusqu’à la captivité.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Les fils de la demi-tribu de Manassé habitaient dans le pays depuis Basan jusqu’à Baal-Hermon et à Sanir, et à la montagne d’Hermon; ils étaient nombreux.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
Voici les chefs de leurs familles: Epher, Jési, Eliel, Ezriel, Jérémia, Odoïa et Jédiel, hommes forts et vaillants, hommes de renom, chefs de leurs maisons patriarcales.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Mais ils furent infidèles au Dieu de leurs pères, et ils se prostituèrent en servant les dieux des peuples du pays que Dieu avait détruits devant eux.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
Le Dieu d’Israël excita l’esprit de Phul, roi d’Assyrie, et l’esprit de Thelgathphalnasar, roi d’Assyrie; et Thelgathphalnasar emmena captifs les Rubénites, les Gadites et la demi-tribu de Manassé, et il les conduisit à Hala, à Habor, à Ara et au fleuve de Gozan, où ils sont demeurés jusqu’à ce jour.