< 1 Nyakati 5 >

1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Also the sones of Ruben, the firste gendrid sone of Israel; for he was the first gendrid sone of Israel, but whanne he hadde defoulid the bed of his fadir, the dignitye of his firste gendryng was youun to the sones of Joseph, the sone of Israel; and Ruben was not arettid in to the firste gendrid sone.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Forsothe Judas, that was the strongeste among hise britheren, prynces weren gaderid of his generacioun; forsothe the `riyt of firste gendryng was arettid to Joseph.
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Therfor the sones of Ruben, the firste gendrid sone of Israel, weren Enoch, and Phallu, Esrom, and Charmy.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
The sones of Johel weren Samaie; his sone, Gog; his sone, Semey;
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
his sone, Mycha; his sone, Rema; his sone, Baal;
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
his sone, Bera; whom Theglatphalassar, kyng of Assyriens, ledde prisoner; and he was prince in the lynage of Ruben.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Sotheli hise britheren, and al the kynrede, whanne thei weren noumbrid bi her meynees, hadden princes Jehiel, and Zacharie.
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Forsothe Bala, the sone of Achaz, sone of Sama, sone of Johel, he dwellide in Aroer til to Nebo and Beelmoon;
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
and he dwellide ayens the eest coost, til to the ende of deseert, `and to the flood Eufrates. And he hadde in possessioun myche noumbre of beestis in the lond of Galaad.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Forsothe in the daies of Saul the sones of Ruben fouyten ayens Agarenus, and killide hem; and dwelliden for hem in the tabernaclis of hem, in al the coost that biholdith to the eest of Galaad.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Sotheli the sones of Gad euene ayens hem dwelliden in the lond of Basan til to Selca;
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Johel was in the bygynnyng, and Saphan was the secounde; also Janahi and Saphan weren in Basan.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
Also her britheren bi the housis of her kynredis, Mychael, and Mosollam, and Sebe, and Jore, and Jachan, and Zie, and Heber, seuene.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
These weren the sones of Abiahel, the sone of Vry, sone of Jaro, sone of Galaad, sone of Mychael, sone of Esesi, sone of Jeddo, sone of Buz.
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Also the britheren of the sone of Abdiel, sone of Gumy, was prince of the hows in hise meynees.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
And thei dwelliden in Galaad, and in Basan, and in the townes therof, in alle the subarbis of Arnon, til to the endis.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Alle these weren noumbrid in the daies of Joathan, kyng of Juda, and in the daies of Jeroboam, kyng of Israel.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
The sones of Ruben, and of Gad, and of half the lynage of Manasses, weren men werriours, berynge scheeldis and swerdis, and beendynge bouwe, and tauyt to batels, foure and fourti thousynde seuene hundrid and sixti,
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
and thei yeden forth to batel, and fouyten ayens Agarenus. Forsothe Ethureis, and Napheis,
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
and Nadab, yauen help to hem; and Agarenus, and alle men that weren with hem, weren bitakun in to the hondis of Ruben, and Gad, and Manasses; for thei clepiden inwardli the Lord, while thei fouyten, and the Lord herde hem, for thei `hadden bileuyd in to him.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
And thei token alle thingis whiche Agarenus hadden in possessioun, fifti thousynde of camels, and twei hundrid and fifty thousynde of scheep, twei thousynde of assis, and an hundrid thousynde persoones of men;
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
for many men weren woundid and felden doun; for it was the batel of the Lord. And thei dwelliden for Agarenus til to the conquest.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Also the sones of the half lynage of Manasses hadden in possessioun the lond, fro the endis of Basan til to Baal Hermon, and Sanyr, and the hil of Hermon; for it was a greet noumbre.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
And these weren the princes of the hows of her kynrede; Epher, and Jesi, and Heliel, and Esryel, and Jeremye, and Odoie, and Jedihel, strongeste men and myyti, and nemyd duykis in her meynees.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Forsothe thei forsoken the God of her fadris, and diden fornycacioun after the goddis of puplis of the lond, whiche the Lord took awei bifor hem.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
And the Lord God of Israel reiside the spirit of Phul, kyng of Assiriens, and the spirit of Theglatphalasser, kyng of Assur; and he translatide Ruben, and Gad, and the half lynage of Manasses, and brouyte hem in to Ale, and Abor, and Aram, and in to the ryuer of Gozam, til to this dai.

< 1 Nyakati 5 >