< 1 Nyakati 5 >
1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Also, there were the sons of Reuben, the firstborn of Israel. For indeed, he was his firstborn, but when he had violated the bed of his father, his right as firstborn was given to the sons of Joseph, the son of Israel, and he was not reputed as firstborn.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Moreover, Judah, who was strongest among his brothers, from his stock leaders sprung up, but the right of firstborn was reputed to Joseph.
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
So then, the sons of Reuben, the firstborn of Israel, were Hanoch and Pallu, Hezron and Carmi.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
The sons of Joel: Shemaiah his son, Gog his son, Shimei his son,
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Micah his son, Reaiah his son, Baal his son,
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Beerah his son, whom Tilgath-pilneser, the king of the Assyrians, led away captive, and he was a leader in the tribe of Reuben.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
Now his brothers and all his kindred, when they were being numbered according to their families, had as leaders Jeiel and Zechariah.
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Now Bela, the son of Azaz, the son of Shema, the son of Joel, lived in Aroer, as far as Nebo and Baalmeon.
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
And he lived toward the eastern region, as far as the entrance to the wilderness and the river Euphrates. For indeed, they possessed a great number of cattle in the land of Gilead.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Then, in the days of Saul, they battled against the Hagarites and put them to death. And they lived in place of them, in their dwellings, throughout the entire region that looks to the east of Gilead.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Truly, the sons of Gad lived in the opposite region from them, in the land of Bashan, as far as Salecah:
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Joel the head, and Shapham the second, then Janai and Shaphat, in Bashan.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
Truly, their brothers, according to the houses of their kindred, were: Michael, and Meshullam, and Sheba, and Jorai, and Jacan, and Zia, and Eber, seven.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
These were the sons of Abihail, the son of Huri, the son of Jaroah, the son of Gilead, the son of Michael, the son of Jeshishai, the son of Jahdo, the son of Buz,
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
along with their brothers, the sons of Abdiel, the son of Guni, the leader of the house, in their families,
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
And they lived in Gilead, and in Bashan and its towns, and in all the suburbs of Sharon, as far as the borders.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
All these were numbered in the days of Jotham, the king of Judah, and in the days of Jeroboam, the king of Israel:
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
the sons of Reuben, and of Gad, and the one half tribe of Manasseh, men of war, carrying shields and swords, and bending the bow, and trained for battle, forty-four thousand and seven hundred sixty, advancing to the fight.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
They struggled against the Hagarites, yet truly the Jetureans, and Naphish, and Nodab offered assistance to them.
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
And the Hagarites were delivered into their hands, and all who were with them. For they called upon God while they did battle. And he heeded them, because they had trusted in him.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
And they seized all that they possessed, of camels fifty thousand, and of sheep two hundred fifty thousand, and of donkeys two thousand, and of men one hundred thousand lives.
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
And many fell down wounded. For it was a war of the Lord. And they lived in place of them, until the transmigration.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Also, the sons of the one half tribe of Manasseh possessed the land, from the parts of Bashan as far as Baal, Hermon, and Sanir, and Mount Hermon. For certainly, their number was immense.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
And these were leaders of the house of their kindred: Epher, and Ishi, and Eliel, and Azriel, and Jeremiah, and Hodaviah, and Jahdiel, very valiant and powerful men, and renowned leaders in their families.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
But they abandoned the God of their fathers, and they fornicated after the gods of the peoples of the land, whom God took away before them.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
And so the God of Israel stirred up the spirit of Pul, the king of the Assyrians, and the spirit of Tilgath-pilneser, the king of Assur. And he took away Reuben, and Gad, and the one half tribe of Manasseh. And he led them to Halah, and to Habor, and to Hara, and to the river of Gozan, even to this day.