< 1 Nyakati 5 >
1 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli (yeye alikuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa kuwa alikinajisi kitanda cha baba yake, haki zake za mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu mwana wa Israeli. Hivyo hakuorodheshwa kwenye orodha ya ukoo wao kulingana na haki yake ya kuzaliwa.
Israel caming Reuben koca ah amah te caming ni. Tedae a napa kah rhaenghmuen te a poeih pah dongah a caminghamsum te Israel capa Joseph koca taengla a paek. Te dongah caminghamsum kah a khuui la om voel pawh.
2 Na ingawa Yuda alikuwa na nguvu zaidi ya ndugu zake wote, na mtawala alitoka kwake, haki za mzaliwa wa kwanza zilikuwa za Yosefu.)
Judah khaw a manuca lakli ah tah len tih amah lamloh rhaengsang cakhaw caminghamsum tah Joseph taengah ni a om.
3 Wana wa Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli walikuwa: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi.
Israel caming Reuben koca ah Enok, Pallu, Khetsron neh Karmee.
4 Wazao wa Yoeli walikuwa: Shemaya mwanawe, Gogu mwanawe; Shimei mwanawe,
Joel koca ah, a capa Shemaiah, Shemaiah capa Gog, Gog capa Shimei.
5 Mika mwanawe, Reaya mwanawe, Baali mwanawe,
Shimei capa Maikah, Mikah capa Reaiah, Reaiah capa Baal.
6 na Beera mwanawe, ambaye Tiglath-Pileseri mfalme wa Ashuru alimchukua kwenda uhamishoni. Beera alikuwa kiongozi wa Wareubeni.
Baal capa Beerah. Anih te Reuben kah a khoboei la om dae Assyria manghai Tiglathpileser loh a poelyoe.
7 Jamaa zao kulingana na koo zao, walioorodheshwa kwa kufuata koo zao kama ifuatavyo: Yeieli aliyekuwa mkuu wao, Zekaria,
A manuca khaw amah koca ah tah a khuui la ana om van. Amih rhuirhong khuikah a lu la Jeiel, Zekhariah,
8 Bela mwana wa Azazi, mwana wa Shema, mwana wa Yoeli. Hao waliishi katika eneo kuanzia Aroeri mpaka Nebo na Baal-Meoni.
Azaz capa Bala, Shema capa Azaz, Joel capa Shema loh Aroer neh Nebo Baalmeon duela kho a sak.
9 Kwa upande wa mashariki walienea hadi pembeni mwa jangwa linaloenea mpaka kwenye Mto Frati, kwa sababu mifugo yao ilikuwa imeongezeka huko Gileadi.
Amih kah boiva he Gilead khohmuen ah a ping pah dongah khocuk ah Perath tuiva lamloh khosoek hmoi hil kho a sak.
10 Wakati wa utawala wa Mfalme Sauli, walipigana vita dhidi ya Wahagari, wakaanguka kwa mikono yao, kisha wakaishi katika mahema ya Wahagari katika eneo lote la mashariki ya Gileadi.
Saul tue vaengah tah Hagri taengah caemtloek a saii tih amih kut ah cungku uh. Te vaengah amih kah dap ah Gilead khocuk imdan pum ah kho a sak uh.
11 Wagadi waliishi jirani nao katika nchi ya Bashani, mpaka Saleka.
Amih hmatoeng te Gad koca rhoek tih Bashan khohmuen ah Salkhah duela kho a sak uh.
12 Yoeli ndiye alikuwa mkuu wao, Shafamu wa pili, na wakafuata Yanai na Shafati, huko Bashani.
Bashan ah a lu la Joel tih a hnukthoi ah Shapham, Janai neh Shaphat om.
13 Ndugu zao kulingana na koo zao walikuwa saba: Mikaeli, Meshulamu, Sheba, Yorai, Yakani, Zia na Eberi.
A napa imkhui ah a manuca rhoek tah Michael, Meshullam, Sheba, Jorai, Jakhan, Zia, Eber neh parhih louh.
14 Hawa walikuwa ndio wana wa Abihaili mwana wa Huri, mwana wa Yaroa, mwana wa Gileadi, mwana wa Mikaeli, mwana wa Yeshishai, mwana wa Yahdo, mwana wa Buzi.
Abihail koca rhoek he Huri koca, Jaorah koca, Gilead koca, Michael koca, Jeshishai capa, Jahdo koca, Buz koca la om.
15 Ahi mwana wa Abdieli, mwana wa Guni, alikuwa ndiye kiongozi wa jamaa yao.
Guni koca Abdiel capa Ahi he a napa imkhui ah a lu la om.
16 Wagadi waliishi Gileadi, huko Bashani pamoja na vijiji vilivyoizunguka, pia katika nchi yote ya malisho ya Sharoni kote walikoenea.
Te dongah Gilead ah khaw, Bashan ah khaw a vang khui neh Sharon khocaak pum ah a hmoi duela kho a sak uh.
17 Yote haya yaliwekwa katika kumbukumbu za ukoo wao wakati wa utawala wa Yothamu, mfalme wa Yuda na Yeroboamu mfalme wa Israeli.
Amih boeih te Judah manghai Jotham tue ah khaw, Israel manghai Jeroboam tue ah khaw a khuui a thuep coeng.
18 Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase walikuwa na watu mashujaa 44,760 waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya vita: watu wenye nguvu, hodari wa kutumia ngao na upanga, mashujaa wa kutumia upinde, waliokuwa tayari kwa ajili ya kazi hiyo.
Reuben koca, Gad koca, photling neh cunghang aka muk, lii aka oei, caemtloek neh aka phaep uh tih caempuei la aka pawk, Manasseh koca rhakthuem lamkah hlang, tatthai capa he thawng sawmli thawng li ya rhih sawmrhuk lo.
19 Walipigana vita dhidi ya Wahagari, Yeturi, Nafishi na Nodabu.
Te vaengah Hagri, Jetur, Naphish neh Nodab taengah caemtloek la thoo uh.
20 Walisaidiwa katika kupigana nao, Mungu akawatia Wahagari pamoja na wote walioungana nao mikononi mwao, kwa sababu walimlilia Mungu wakati wa vita. Alijibu maombi yao, kwa sababu walimtegemea.
Caemtloek vaengah khaw Pathen taengah pang uh tih amah dongah a pangtung uh dongah amih ham khaw a rhoi pah. Te dongah amih te a bom tih Hagri neh a taengkah boeih te amih kut ah a paek.
21 Walitwaa mifugo ya Wahagari: ngamia 50,000, kondoo 250,000, punda 2,000. Pia wakateka watu 100,000,
Amih kah boiva te a sol uh tih a kalauk thawng sawmnga, boiva thawng yahnih thawng sawmnga, laak thawng hnih, hlang kah hinglu thawng yakhat lo.
22 na wengine wengi waliuawa kwa sababu vita vilikuwa ni vya Mungu. Nao waliendelea kuikalia nchi hiyo mpaka wakati wa uhamisho.
Pathen taeng lamkah caemtloek la a om dongah a rhok la muep cungku uh. Te dongah a vangsawn khohnin hil tah amih yueng la kho a sak uh.
23 Idadi ya nusu ya kabila la Manase walikuwa wengi sana, Wakakaa kuanzia Bashani hadi Baal-Hermoni, yaani mpaka Seniri na mlima Hermoni.
Manasseh koca hlangvang ca rhoek khaw khohmuen ah Bashan lamloh Baalhermon hil kho a sak uh. Senir neh Hermon tlang ah khaw amih te ping uh.
24 Hawa ndio waliokuwa viongozi wa jamaa za kabila hilo: Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia na Yahdieli. Walikuwa askari shujaa watu maarufu, viongozi wa jamaa zao.
A napa rhoek kah imkhui kah a lu he tah, Epher, Ishi, Eliel, Azriel, Jeremiah, Hodaviah, Jahdiel. He tah a napa rhoek imkhui kah a lu la aka om hlang neh tatthai hlangrhalh hlang kah a ming ni.
25 Lakini hawakuwa waaminifu kwa Mungu wa baba zao, nao wakafanya ukahaba kwa miungu ya mataifa, ambayo Mungu alikuwa ameyaangamiza mbele yao.
Tedae a napa rhoek kah Pathen taengah boe a koek uh tih Pathen loh amih mikhmuh lamkah a mitmoeng sak khohmuen pilnam kah pathen roek taengla cukhalh uh.
26 Kwa hiyo Mungu wa Israeli akaiamsha roho ya Pulu, mfalme wa Ashuru (ambaye pia alijulikana kama Tiglath-Pileseri), ambaye aliwachukua Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase kwenda uhamishoni. Akawapeleka huko Hala, Habori, Hara na mto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.
Te dongah Israel Pathen loh Assyria manghai Pul kah mueihla neh Assyria manghai Tiglathpileser kah mueihla te a haeng pah. Te vaengah amih, Reuben neh Gad, Manasseh koca hlangvang te a poelyoe. Te phoeiah amih te Halah, Habor, Hara neh tahae khohnin hil Gozan tuiva la a khuen.