< 1 Nyakati 4 >

1 Wana wa Yuda walikuwa: Peresi, Hesroni, Karmi, Huri na Shobali.
Judovi sinovi: Parec, Hecrón, Karmí, Hur in Šobál.
2 Reaya mwana wa Shobali akamzaa Yahathi, Yahathi akawazaa Ahumai na Lahadi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Wasorathi.
Reajá, sin Šobála, je zaplodil Jahata. Jahat je zaplodil Ahumája in Lahada. To so družine Corčanov.
3 Hawa ndio waliokuwa wana wa Etamu: Yezreeli, Ishma na Idbashi. Dada yao aliitwa Haselelponi.
Ti so bili od očeta Etáma: Jezreél, Jišmá in Jidbáš in ime njihove sestre je bilo Haclelpóni;
4 Penueli akamzaa Gedori, naye Ezeri akamzaa Husha. Hawa walikuwa wazao wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi, na baba yake Bethlehemu.
Penuél, oče Gedórja in Ecer, oče Hušája. To so sinovi Hura, Efrátinega prvorojenca, očeta Betlehema.
5 Ashuri baba yake Tekoa alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.
Ašhúr, oče Tekóe, je imel dve ženi, Helo in Naáro.
6 Hawa walikuwa wazao wa Naara: Ahuzamu, Heferi, Temeni na Haahashtari.
Naára mu je rodila Ahuzáma, Heferja, Timníja in Ahaštaríja. Ti so bili Naárini sinovi.
7 Wana wa Hela walikuwa: Serethi, Sohari, Ethnani,
Sinovi Hele so bili Ceret, Cohar in Etnán.
8 na Kosi ambaye aliwazaa Anubi, Sobeba na jamaa zote za Aharheli mwana wa Harumu.
Koc je zaplodil Anúba in Cobebá in družine Harúmovega sina Aharhéla.
9 Yabesi aliheshimiwa kuliko ndugu zake. Mama yake alimwita Yabesi, akisema, “Nilimzaa kwa huzuni.”
Jabéc je bil bolj častitljiv kakor njegovi bratje in njegova mati je njegovo ime imenovala Jabéc, rekoč: »Ker sem ga rodila z bridkostjo.«
10 Yabesi akamlilia Mungu wa Israeli akisema, “Ee Mungu, laiti ungenibariki kweli kweli na kuipanua mipaka yangu! Mkono wako na uwe pamoja nami, uniepushe na uovu ili nisidhurike!” Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.
Jabéc je klical k Izraelovemu Bogu, rekoč: »Oh da bi me ti resnično blagoslovil in povečal moj kraj in da bi bila tvoja roka lahko z menoj in da bi me varoval pred zlom, da me ta ne bi žalostil!« In Bog mu je zagotovil to, kar je zahteval.
11 Kelubu, nduguye Shuha, akamzaa Mehiri, naye Mehiri akamzaa Eshtoni.
Kelúb, brat Šuaha, je zaplodil Mehírja, ki je bil oče Eštóna.
12 Eshtoni akawazaa Beth-Rafa, Pasea na Tehina. Tehina alikuwa baba wa Iri-Nahashi. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Reka.
Eštón je zaplodil Betrafá, Paséaha in Tehiná, očeta Ir Naháša. To so možje iz Rehe.
13 Wana wa Kenazi walikuwa: Othnieli na Seraya. Wana wa Othnieli walikuwa: Hathathi na Meonathai.
Kenázova sinova: Otniél in Serajá. Otniélovi sinovi: Hatát.
14 Meonathai akamzaa Ofra. Seraya akamzaa Yoabu, baba wa Ge-Harashimu. Liliitwa hivyo kwa sababu watu walioishi humo walikuwa mafundi.
Meonotáj je zaplodil Ofrá. Serajá je zaplodil Joába, očeta doline Ge Haraším, kajti bili so rokodelci.
15 Kalebu mwana wa Yefune alikuwa na wana watatu: Iru, Ela na Naamu. Naye mwana wa Ela alikuwa: Kenazi.
Sinovi Jefunéjevega sina Kaléba: Iru, Elá in Náam. Elájevi sinovi: celo Kenáz.
16 Wana wa Yahaleleli walikuwa: Zifu, Zifa, Tiria na Asareli.
Jehalelélovi sinovi: Zif, Zifá, Tirjá in Asarél.
17 Wana wa Ezra walikuwa: Yetheri, Meredi, Eferi na Yaloni. Mmojawapo wa wake zake Meredi aliwazaa: Miriamu, Shamai na Ishba aliyekuwa baba yake Eshtemoa.
Sinovi Ezra so bili: Jeter, Mered, Efer in Jalón. In ona je rodila Mirjáma, Šamája in Jišbáha, očeta Eštemóa.
18 Meredi alikuwa na mke mwingine Myahudi ambaye aliwazaa: Yeredi baba wa Gedori, Heberi baba wa Soko na Yekuthieli baba wa Zanoa. Hawa walikuwa watoto wa Bithia binti Farao, ambaye Meredi alikuwa amemwoa.
Njegova žena Jehudija je rodila Jereda, Gedórjevega očeta in Heberja, Sohójevega očeta in Jekutiéla, Zanóahovega očeta. Vsi ti so sinovi faraonove hčere Bitije, ki jo vzel Mered.
19 Wana wa mke wa Hodia aliyekuwa dada yake Nahamu walikuwa: baba yake Keila, Mgarmi na Eshtemoa, Mmaakathi.
Sinova njegove žene Hodijáje, Nahamove sestre, Keílin oče Garmít in Maahčán Eštemóa.
20 Wana wa Shimoni walikuwa: Amnoni, Rina, Ben-Hanani na Tiloni. Wazao wa Ishi walikuwa: Zohethi na Ben-Zohethi.
Šimónovi sinovi so bili Amnón, Riná, Ben-Hanán in Tilón. Jišíjeva sinova sta bila Zohét in Ben Zohét.
21 Wana wa Shela, mwana wa Yuda, walikuwa: Eri baba yake Leka, Laada baba yake Maresha na jamaa za wafumaji nguo za kitani safi waliokuwa wakiishi huko Beth-Ashbea,
Sinovi Judovega sina Šelája so bili Er, Lehájev oče in Ladá, Marešájev oče in družine iz hiše tistih, ki so izdelovali tanko laneno platno, iz hiše Ašbéa;
22 Yokimu, watu walioishi Kozeba, Yoashi na Sarafi waliotawala huko Moabu na Yashubi-Lehemu. (Taarifa hizi ni za zamani sana.)
in Jokím, možje iz Kozébe, Joáš in Saráf, ki so imeli gospostvo v Moábu in Jashubi–lehemu. In to so starodavne stvari.
23 Hawa walikuwa wafinyanzi walioishi Netaimu na Gedera; waliishi huko wakimtumikia mfalme.
Ti so bili lončarji in tisti, ki so prebivali med sadikami in ograjami. Tam so zaradi svojega dela prebivali s kraljem.
24 Wazao wa Simeoni walikuwa: Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera na Shauli.
Simeonovi sinovi so bili Nemuél, Jamín, Jaríb, Zerah in Šaúl;
25 Mwana wa Shauli alikuwa Shalumu, Shalumu akamzaa Mibsamu, na Mibsamu akamzaa Mishma.
njegov sin Šalúm, njegov sin Mibsám, njegov sin Mišmá.
26 Wazao wa Mishma walikuwa: Hamueli aliyemzaa Zakuri, Zakuri akamzaa Shimei.
Mišmájevi sinovi: njegov sin Hamuél, njegov sin Zakúr in njegov sin Šimí.
27 Shimei alikuwa na wana kumi na sita, na binti sita, lakini ndugu zake hawakuwa na watoto wengi, hivyo ukoo wao wote haukuwa na watu wengi kama ukoo wa Yuda.
Šimí je imel šestnajst sinov in šest hčera, toda njegovi bratje niso imeli veliko otrok niti se vse njihove družine niso množile, kakor Judovi otroci.
28 Waliishi Beer-Sheba, Molada, Hasar-Shuali,
Prebivali so pri Beeršébi, Moládi, Hacár Šuálu,
29 Bilha, Esemu, Toladi,
pri Bilhi, pri Ecemu, pri Toladu,
30 Bethueli, Horma, Siklagi,
pri Betuélu, pri Hormi, pri Ciklágu,
31 Beth-Markabothi, Hasar-Susimu, Beth-Biri na Shaaraimu. Hii ilikuwa miji yao mpaka wakati wa utawala wa Daudi.
pri Bet Markabótu, pri Hacár Susímu, pri Bet Biríju in pri Šaarájimu. To so bila njihova mesta do Davidovega kraljevanja.
32 Vijiji vilivyoizunguka vilikuwa Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni na Ashani; jumla miji mitano:
Njihove vasi so bile Etám, Ajin, Rimón, Tohen in Ašán, pet mest
33 pamoja na vijiji vyote kuizunguka hii miji hadi huko Baali. Haya yalikuwa makao yao, nao waliweka kumbukumbu ya ukoo wao.
in vse njihove vasi, ki so bile naokoli istih mest, do Báala. To so bila njihova prebivališča in njihov rodovnik.
34 Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia,
Mešobáb, Jamléh, Amacjájev sin Jošá,
35 Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia, mwana wa Seraya, mwana wa Asieli.
Joél, Jehú, sin Jošibjája, sin Serajája, sin Asiéla,
36 Pia Elioenai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya,
Eljoenáj, Jaakóba, Ješohája, Asajá, Adiél, Jesimiél, Benajá,
37 Ziza mwana wa Shifi, mwana wa Aloni, mwana wa Yedaya, mwana wa Shimri, mwana wa Shemaya.
Zizá, sin Šifíja, sinú Alóna, sinú Jedajája, sinú Šimríja, sinú Šemajája;
38 Watu hawa walioorodheshwa hapa juu kwa majina walikuwa viongozi wa koo zao. Jamaa zao ziliongezeka sana,
ti, omenjeni po svojih imenih, so bili princi v svojih družinah in hiše njihovih očetov so se silno povečale.
39 wakaenea mpaka kwenye viunga vya Gedori kuelekea mashariki mwa bonde wakitafuta malisho kwa ajili ya mifugo yao.
Šli so k vhodu Gedórja, celó do vzhodne strani doline, da poiščejo pašnik za svoje trope.
40 Huko walipata malisho mengi mazuri, nayo nchi ilikuwa na nafasi kubwa, yenye amani na utulivu. Baadhi ya Wahamu waliishi huko zamani.
Našli so obilen in dober pašnik in dežela je bila prostrana, tiha in mirna, kajti tisti iz Hama so tam prebivali od davnine.
41 Watu walioorodheshwa majina walikuja katika nchi hiyo wakati wa Hezekia mfalme wa Yuda. Akawashambulia Wahamu katika makao yao pamoja na Wameuni ambao walikuwako huko nao wakawaangamiza kabisa, kama ilivyo dhahiri hadi leo. Kisha wakafanya makazi yao huko kwa sababu kulikuwa na malisho mazuri kwa ajili ya mifugo yao.
In tisti, zapisani po imenu, so prišli v dneh Judovega kralja Ezekíja in udarili njihove šotore in prebivališča, ki so bila najdena tam in jih popolnoma uničili do današnjega dne in prebivali so namesto njih, ker je bil tam pašnik za njihove trope.
42 Watu wa kabila la wa Simeoni wapatao mia tano, wakiongozwa na Pelatia, Nearia, Refaya na Uzieli wana wa Ishi, wakavamia nchi ya vilima ya Seiri.
Nekateri izmed njih, celo izmed Simeonovih sinov, petsto mož, so odšli na gorovje Seír, za svoje poveljnike pa so imeli Pelatjája, Nearjá, Refajá, Uziéla, Jišíjeve sinove.
43 Wakawaua Waamaleki waliobaki, waliokuwa wamenusurika, nao wanaishi huko hadi leo.
Udarili so preostanek Amalečanov, ki so pobegnili in tam prebivajo do današnjega dne.

< 1 Nyakati 4 >