< 1 Nyakati 29 >

1 Ndipo Mfalme Daudi akaliambia kusanyiko lote: “Mwanangu Solomoni, yeye ambaye Mungu amemchagua, ni kijana mdogo na asiye na uzoefu. Kazi hii ni kubwa, kwa sababu Hekalu hili la fahari si kwa ajili ya mwanadamu bali ni kwa ajili ya Bwana.
Et le roi David dit à toute l'Église: Mon fils Salomon, en qui le Seigneur s'est complu, est jeune et délicat, et l'œuvre est grande, car elle n'est point pour l'homme, mais pour le Seigneur Dieu.
2 Kwa uwezo wangu wote nimetenga mali kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu: dhahabu kwa kazi za dhahabu, fedha kwa ajili ya fedha, shaba kwa kazi za shaba, chuma kwa kazi za chuma na miti kwa kazi za miti, vivyo hivyo vito vya shohamu kwa ajili ya kutia kwenye vijalizo, almasi, mawe ya rangi mbalimbali, aina zote za vito vya thamani na marmar; yote haya kwa wingi mno.
Autant que je l'ai pu, j'ai préparé pour le temple de mon Dieu: de l'or, de l'argent, de l'airain, du fer, des bois, des pierres d'onyx, quantité de pierres chères et variées, toutes sortes de pierres précieuses, et beaucoup de marbre.
3 Zaidi ya hayo, kwa kujitolea kwangu kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, sasa ninatoa hazina zangu mwenyewe za dhahabu na fedha kwa ajili ya Hekalu la Mungu wangu, zaidi ya mali niliyotoa kwa ajili ya Hekalu hili takatifu:
De plus, comme je mets ma joie en la demeure de mon Dieu, j'ai conservé l'or et l'argent que je me suis procuré pour moi-même; je le donne entièrement au temple de mon Dieu, outre ce que j'ai amassé pour la maison des choses saintes, savoir:
4 talanta 3,000 za dhahabu (dhahabu ya Ofiri) na talanta 7,000 za fedha safi iliyosafishwa, kwa ajili ya kufunika kuta za Hekalu,
Trois mille talents d'or d'Ophir, et sept mille talents d'argent pur, pour que l'on en recouvre les murs du lieu saint.
5 kwa kazi ya dhahabu na kazi ya fedha na kwa kazi yote itakayofanywa na mafundi. Basi, ni nani anayependa kujitoa kwa Bwana leo?”
Il y aura ce qu'il faut à la main de l'artisan. Mais est-il quelqu'un qui désire aujourd'hui remplir ses mains pour le Seigneur?
6 Ndipo viongozi wa jamaa, maafisa wa kabila za Israeli, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, pamoja na maafisa waliokuwa wasimamizi wa kazi za mfalme wakatoa kwa hiari yao.
Et les princes des familles le désirèrent, les princes des fils d'Israël ainsi que les commandants de mille hommes, et les centeniers, et les intendants des travaux, et les architectes du roi.
7 Wakatoa kwa ajili ya kazi ya Hekalu la Mungu talanta 5,000 na darkoni 10,000 za dhahabu, talanta 10,000 za fedha, talanta 18,000 za shaba na talanta 100,000 za chuma.
Et ils donnèrent pour les travaux du temple du Seigneur: cinq mille talents et dix mille sicles d'or; dix mille talents d'argent; dix-huit mille talents d'airain et cent mille talents de fer.
8 Kila mmoja aliyekuwa na vito vya thamani akavitoa katika hazina ya Hekalu la Bwana chini ya uangalizi wa Yehieli Mgershoni.
Et celui chez qui il se trouva quelque pierre précieuse, la donna pour le trésor du temple par les mains de Dehiel, de la famille de Gerson.
9 Watu wakafurahi kwa sababu ya itikio la hiari la viongozi wao, kwa kuwa walikuwa wametoa kwa hiari na kwa moyo wote kwa Bwana. Mfalme Daudi pia akafurahi sana.
Et le peuple eut une grande joie à cause de ce zèle, car chacun eut ce zèle pour Dieu de plein cœur. Et le roi David fut comblé de joie.
10 Daudi akamhimidi Bwana mbele ya kusanyiko lote, akisema: “Uhimidiwe wewe, Ee Bwana, Mungu wa Israeli baba yetu, tangu milele hata milele.
Et le roi David bénit le Seigneur devant toute l'Église, disant: Béni soyez-vous, Seigneur Dieu d'Israël, ô notre Père, dans tous les siècles des siècles!
11 Ukuu na uweza, ni vyako, Ee Bwana, na utukufu na enzi na uzuri, kwa kuwa kila kilichoko mbinguni na duniani ni chako wewe. Ee Bwana, ufalme ni wako; umetukuzwa kuwa mkuu juu ya yote.
A vous, Seigneur, la magnificence, la force, la gloire, la victoire et la puissance; car vous êtes le maître de toutes les choses qui sont sur la terre et dans les cieux. Tous les rois des nations sont troublés devant vous.
12 Utajiri na heshima vyatoka kwako; wewe ndiwe utawalaye vitu vyote. Mikononi mwako kuna nguvu na uweza ili kuinua na kuwapa wote nguvu,
De vous viennent gloire et richesse; vous régnez sur toutes choses, ô Seigneur, prince de toutes les dominations; la force et le pouvoir résident en vos mains, et il dépend de vous, ô Tout-Puissant, de grandir et de fortifier toutes choses.
13 Sasa, Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu Jina lako tukufu.
Et maintenant, Seigneur, nous vous rendons hommage, nous louons votre nom et votre gloire.
14 “Lakini mimi ni nani, nao watu wangu ni nani, hata tuweze kukutolea kwa ukarimu namna hii? Vitu vyote vyatoka kwako, nasi tumekutolea tu vile vitokavyo mkononi mwako.
Et qui suis-je, moi, et qui est mon peuple, pour que nous ayons pu vous faire ces offrandes avec tant de zèle? Tout est à vous, et nous vous avons donné de ce qui vous appartient.
15 Sisi ni wageni na wapitaji machoni pako, kama walivyokuwa baba zetu wote. Siku zetu duniani ni kama kivuli, bila tumaini.
Car nous sommes des passagers devant vous, et Nous passons comme tous nos pères; nos jours sur la terre sont comme l'ombre, et rien n'a de la durée.
16 Ee Bwana Mungu wetu, kwa wingi wote huu ambao tumekutolea kwa kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina lako Takatifu, vimetoka mkononi mwako, navyo vyote ni mali yako.
Seigneur notre Dieu, toutes les richesses que j'ai préparées pour bâtir un temple à votre saint nom, viennent de vous; tout cela vous appartient.
17 Ninajua, Mungu wangu, kwamba wewe huujaribu moyo na unapendezwa na unyofu. Vitu hivi vyote nimetoa kwa hiari na kwa moyo mnyofu. Nami sasa nimeona kwa furaha jinsi watu wako walioko hapa kwa hiari yao walivyokutolea wewe.
Et j'ai reconnu, ô mon Dieu, que c'est vous qui sondez les cœurs et que vous aimez la justice; et je vous ai fait mes offrandes dans la simplicité de mon cœur, et je viens de voir ici avec joie ce peuple mettre tant de zèle à vous faire ses offrandes.
18 Ee Bwana, Mungu wa baba zetu Abrahamu, Isaki na Israeli, weka shauku hii ndani ya mioyo ya watu wako daima na uifanye mioyo yao iwe na uaminifu kwako.
Seigneur Dieu d'Abraham, d'Isaac et d'Israël nos pères, faites que votre peuple conserve toujours en son cœur le même amour, et dirigez son cœur vers vous.
19 Nawe umpe mwanangu Solomoni kujitolea kwako kwa moyo wote ili kuzishika amri zako, masharti yako, maagizo yako na kufanya kila kitu ili kujenga Hekalu hili la fahari ambalo kwa ajili yake nimetoa.”
Et donnez à mon fils Salomon un bon cœur pour exécuter vos commandements, pour être attentif à vos ordres et à vos témoignages, et pour conduire jusqu'à la fin la construction de votre temple.
20 Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote, “Mhimidini Bwana Mungu wenu.” Hivyo wote wakamhimidi Bwana, Mungu wa baba zao. Wakasujudu na kuanguka kifudifudi mbele za Bwana na mfalme.
Et David dit à toute l'Église: Bénissez le Seigneur notre Dieu. Et toute l'Église bénit le Seigneur Dieu de leurs pères; ils plièrent les genoux et ils adorèrent le Seigneur et le roi.
21 Siku ya pili yake wakamtolea Bwana dhabihu na sadaka za kuteketezwa: mafahali 1,000, kondoo dume 1,000 na wana-kondoo dume 1,000, pamoja na sadaka za kinywaji na sadaka nyingine nyingi sana kwa ajili ya Israeli.
Et David sacrifia au Seigneur; il offrit en holocauste à Dieu, dès le matin du jour suivant: mille bœufs, mille béliers, mille agneaux; il fit leurs libations, et il distribua des victimes en abondance à tout Israël.
22 Wakala na kunywa kwa furaha kubwa mbele za Bwana siku ile. Wakamtawaza Solomoni mwana wa Daudi mara ya pili kuwa mfalme, wakamtia mafuta kwa ajili ya Bwana ili awe mfalme na Sadoki kuwa kuhani.
Et ils mangèrent, et ils burent avec joie devant le Seigneur toute la journée, et, pour la seconde fois, ils proclamèrent roi Salomon, fils de David; ils le sacrèrent roi devant le Seigneur, et ils sacrèrent Sadoc comme pontife.
23 Solomoni akaketi kwenye kiti cha enzi cha Bwana kuwa mfalme mahali pa Daudi baba yake. Akafanikiwa sana na Israeli wote wakamtii.
Et Salomon s'assit sur le trône de David son père; il fut honoré, et tout Israël lui obéit.
24 Maafisa wote na mashujaa, pamoja na wana wote wa Daudi, wakaahidi kumtii Mfalme Solomoni.
Les princes, les vaillants, et tous les fils du roi David son père, se soumirent à sa puissance.
25 Bwana akamtukuza sana Solomoni mbele ya Israeli wote na kumvika fahari ya kifalme ambayo hakuna mfalme yeyote wa Israeli kabla yake aliwahi kuwa nayo.
Et le Seigneur éleva Salomon au-dessus de tout Israël, il lui donna plus de gloire qu'à nul des rois qui l'avaient devancé.
26 Daudi mwana wa Yese alikuwa mfalme wa Israeli yote.
Or, David, fils de Jessé, avait régné sur Israël
27 Alitawala Israeli kwa miaka arobaini: huko Hebroni alitawala miaka saba, na katika Yerusalemu akatawala miaka thelathini na mitatu.
Quarante ans: sept à Hébron, trente-trois à Jérusalem.
28 Daudi akafa akiwa mzee mwenye umri mwema, akiwa ameshiba siku, utajiri na heshima. Naye Solomoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
Et il finit en une heureuse vieillesse, plein de jours, de richesses et de gloire, et son fils Salomon régna à sa place.
29 Kuhusu matukio ya utawala wa Mfalme Daudi, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kumbukumbu za mwonaji Samweli, na kumbukumbu za nabii Nathani na kumbukumbu za mwonaji Gadi,
Le reste des discours du roi David, ses premières et ses dernières paroles, sont écrits parmi les Récits de Samuel le voyant, de Nathan le prophète, et de Gad le voyant,
30 pamoja na habari zote za utawala wake, nguvu zake na matukio yaliyompata yeye, na Israeli, na falme za nchi nyingine zote.
Concernant tout son règne, ses guerres et les événements arrivés tant à lui qu'à Israël, et en tous les royaumes de la terre.

< 1 Nyakati 29 >