< 1 Nyakati 28 >
1 Daudi akawaita maafisa wote wa Israeli wakusanyike huko Yerusalemu: yaani, maafisa walio juu ya makabila, majemadari wa vikosi katika utumishi wa mfalme, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, maafisa wanaosimamia mali zote na mifugo ya mfalme na wanawe, wakiwemo maafisa wa jumba la kifalme, mashujaa na askari wote walio hodari.
David je zbral vse Izraelove prince, prince rodov in poveljnike skupin, ki so služili kralju po skupini in poveljnike nad tisočimi, poveljnike nad stotimi in oskrbnike nad vsem imetjem in posestjo kralja in njegovih sinov, s častniki in z mogočnimi možmi in z vsemi hrabrimi možmi v Jeruzalem.
2 Mfalme Daudi akainuka na kusema: “Nisikilizeni ndugu zangu nanyi watu wangu. Nilikuwa na nia ya kujenga nyumba ili iwe mahali pa kukaa Sanduku la Agano la Bwana kwa ajili ya kuwa mahali pa kuwekea miguu ya Mungu wetu, nami nikafanya maandalizi ya kuijenga.
Potem je kralj David stopil na svoja stopala in rekel: »Poslušajte me, moji bratje in moje ljudstvo: › Kar se mene tiče, sem imel v svojem srcu, da zgradim hišo počitka za skrinjo Gospodove zaveze in za pručko našega Boga in sem pripravil za gradnjo,
3 Lakini Mungu akaniambia, ‘Wewe hutajenga nyumba kwa Jina langu, kwa sababu wewe umepigana vita na umemwaga damu.’
toda Bog mi je rekel: ›Ne boš gradil hiše mojemu imenu, ker si bil bojevnik in si prelival kri.‹
4 “Hata hivyo, Bwana, Mungu wa Israeli, alinichagua mimi kutoka jamaa yangu yote niwe mfalme juu ya Israeli milele. Alimchagua Yuda kuwa kiongozi na kutoka nyumba ya Yuda akaichagua jamaa yangu na kutoka wana wa baba yangu ikampendeza kunifanya niwe mfalme juu ya Israeli yote.
Vendar je Gospod, Izraelov Bog, mene izbral pred vso hišo mojega očeta, da bi bil na veke kralj nad Izraelom, kajti Juda je izbral, da bi bil vladar; in od Judove hiše, hišo mojega očeta; in med sinovi mojega očeta sem mu bil všeč, da me je postavil za kralja nad vsem Izraelom,
5 Miongoni mwa wanangu wote, naye Bwana amenipa wengi, amemchagua Solomoni mwanangu ili kukikalia kiti cha enzi cha ufalme wa Bwana juu ya Israeli.
in izmed vseh mojih sinov (kajti Gospod mi je dal mnogo sinov), je izbral mojega sina Salomona, da sedi na prestolu Gospodovega kraljestva nad Izraelom.
6 Aliniambia, ‘Solomoni mwanao ndiye atakayejenga nyumba yangu na nyua zangu, kwa maana nimemchagua yeye kuwa mwanangu, nami nitakuwa baba yake.
Rekel mi je: ›Tvoj sin Salomon bo zgradil mojo hišo in moje dvore, kajti izbral sem ga, da bo moj sin in jaz bom njegov oče.
7 Nitaufanya imara ufalme wake milele kama akiendelea kuzishika amri zangu na sheria zangu, kama afanyavyo hivi leo.’
Poleg tega bom na veke utrdil njegovo kraljestvo, če bo stalno izpolnjeval moje zapovedi in moje sodbe, kakor ta dan.‹
8 “Hivyo basi ninawaagiza mbele za Israeli yote na kusanyiko hili la Bwana naye Mungu wetu akiwa anasikia: Kuweni na bidii kuzifuata amri za Bwana Mungu wenu, ili mpate kumiliki nchi hii nzuri na kuwaachia wana wenu kuwa urithi milele.
Zdaj se torej pred očmi vsega Izraela, Gospodove skupnosti in v občinstvu našega Boga, držite in iščite vse zapovedi Gospoda, svojega Boga, da boste lahko posedli to dobro deželo in jo pustili za dediščino svojim otrokom za seboj na veke.
9 “Nawe Solomoni mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa kujitoa kwa moyo wote na kwa nia ya kumkubali, kwa maana Bwana huuchunguza kila moyo na kujua kila kusudi la kila fikira. Ukimtafuta, ataonekana kwako; bali kama ukimwacha, yeye atakukataa milele.
Ti pa, moj sin Salomon, spoznaj Boga svojega očeta in mu služi s popolnim srcem in z voljnim umom, kajti Gospod preiskuje vsa srca in razume vse miselne zamisli. Če ga boš iskal, ga boš našel, toda če ga zapustiš, te bo on zavrgel na veke.
10 Angalia basi, kwa maana Bwana amekuchagua wewe ili ujenge Hekalu kuwa mahali patakatifu. Uwe hodari ukafanye kazi hiyo.”
Pazi torej, kajti Gospod te je izbral, da zgradiš hišo za svetišče. Bodi močan in to stôri.‹«
11 Ndipo Daudi akampa Solomoni mwanawe kielelezo kwa ajili ya ukumbi wa Hekalu, nyumba zake, vyumba vyake vya hazina, ghorofa zake, vyumba vyake vya ndani na mahali pa kufanyia upatanisho.
Potem je David svojemu sinu Salomonu dal vzorec preddverja, njegovih hiš, njegovih zakladnic, njegovih gornjih sob, njegovih notranjih dvoran in kraja sedeža milosti,
12 Akampa vielelezo vya yote Roho alikuwa ameviweka moyoni mwake kwa ajili ya kumbi za Hekalu la Bwana na vyumba vyote vilivyolizunguka, kwa ajili ya hazina za Hekalu la Mungu na kwa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
vzorec vsega, kar je imel po duhu glede dvorov Gospodove hiše in vseh sob naokoli, zakladnic Božje hiše in zakladnic posvečenih stvari.
13 Mfalme pia akampa Solomoni maelekezo kwa ajili ya migawanyo ya huduma za makuhani na Walawi, pia kwa ajili ya kazi zote za huduma katika Hekalu la Bwana. Akampa pia maelezo kuhusu vifaa vyote vya kutumika katika huduma ya Hekalu.
Tudi za skupine duhovnikov in Lévijevcev in za vse delo službe Gospodove hiše in za vse posode službe v Gospodovi hiši.
14 Akamwagizia uzito wa dhahabu kwa ajili ya vitu vyote vya dhahabu vya kutumika katika huduma mbalimbali, uzito wa fedha kwa ajili ya vitu vyote vya fedha vya kutumika katika huduma mbalimbali.
Dal je zlata po teži za stvari iz zlata, za vse priprave vseh vrst službe; tudi srebra za vse priprave iz srebra po teži, za vse priprave vsake vrste službe.
15 Uzito wa dhahabu kwa ajili ya vinara vya dhahabu na taa zake, kukiwa na uzito kwa ajili ya kila kinara na taa zake, pamoja na uzito wa fedha kwa ajili ya kila kinara cha fedha na taa zake, kulingana na matumizi ya kila kinara;
Celo težo za svečnike iz zlata in za njihove svetilke iz zlata po teži za vsak svečnik in za njihove svetilke. In za svečnike iz srebra po teži, tako za svečnik in tudi za njihove svetilke, glede na uporabo vsakega svečnika.
16 uzito wa dhahabu kwa ajili ya meza ya mikate iliyowekwa wakfu, uzito wa fedha kwa ajili ya meza ya fedha;
Po teži je dal zlata za mize hlebov navzočnosti za vsako mizo in podobno zlata za mize iz srebra.
17 uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya nyuma, mabakuli ya kunyunyizia na vikombe, masinia; uzito wa dhahabu kwa ajili ya kila bakuli la dhahabu; uzito wa fedha kwa ajili ya kila bakuli la fedha;
Tudi čistega zlata za kavlje za meso, skledice in čaše. Za zlate umivalnike je dal zlata po teži za vsak umivalnik; in podobno srebra, po teži za vsak umivalnik iz srebra;
18 na uzito wa dhahabu safi kwa ajili ya madhabahu ya kufukizia uvumba. Pia alimpa kielelezo kwa ajili ya gari, yaani, wale makerubi wa dhahabu waliokunjua mbawa zao na kuweka kivuli juu ya Sanduku la Agano la Bwana.
Za kadilni oltar prečiščeno zlato po teži in zlata za vzorec bojnega voza kerubov, ki razprostirata svoje peruti in pokrivata skrinjo Gospodove zaveze.
19 Daudi akasema, “Hii yote, ninayo kwa maandishi kutoka mkononi mwa Bwana ulio juu yangu, naye amenipa ufahamu kwa ajili ya habari zote za kielelezo hiki.”
»Vse to, « je rekel David, »mi je Gospod dal razumeti v pisanju po svoji roki nad menoj, torej vsa dela tega vzorca.«
20 Daudi pia akamwambia Solomoni mwanawe, “Uwe hodari na moyo mkuu, ukafanye kazi hii. Usiogope wala usifadhaike, kwa maana Bwana aliye Mungu, Mungu wangu yu pamoja nawe. Hatakuacha wala hatakupungukia mpaka kazi hii yote kwa ajili ya utumishi wa Hekalu la Bwana itakapokamilika.
David je rekel svojemu sinu Salomonu: »Bodi močan in odločnega poguma in stôri to. Ne boj se niti ne bodi zaprepaden, kajti Gospod Bog, celó moj Bog, bo s teboj. Ne bo te razočaral niti te ne bo zapustil, dokler ne dokončaš vsega dela za službo Gospodove hiše.
21 Migawanyo ya makuhani na Walawi iko tayari kwa ajili ya kazi yote katika Hekalu la Mungu, naye kila mtu mwenye moyo wa kupenda mwenye ustadi katika aina yoyote ya ufundi atakusaidia katika kazi yote. Maafisa na watu wote watatii kila agizo lako.”
Glej, skupine duhovnikov in Lévijevcev, celo oni bodo s teboj za vso službo Božje hiše, in tam bo s teboj za vse vrste rokodelstva vsak voljan vešč mož, za vse vrste del. Tudi princi in vse ljudstvo bo popolno ob tvoji zapovedi.«