< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
Esta es la lista de los israelitas, los jefes de casas paternas, jefes de millares y centenas, con sus oficiales que servían al rey en todos los asuntos de las divisiones. Ellos entraban y salían cada mes durante todo el año. Cada división era de 24.000.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
El comandante de la primera división para el primer mes era Jasobeam, hijo de Zabdiel. En su división había 24.000.
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
Él era de los hijos de Fares y el comandante de todos los jefes del ejército el primer mes.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante de la división para el segundo mes era Dodai ahohíta. Miclot era el jefe principal en esta división, en la cual también había 24.000.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
El comandante de la tercera división para el tercer mes era Benaía, hijo del sumo sacerdote Joiada. Su división tenía 24.000.
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
Este es aquel Benaía que fue héroe entre los 30. Era jefe de los 30. En su división estaba Amisabad su hijo.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el cuarto mes era Asael, hermano de Joab, y después de él su hijo Zebadías. En su división había 24.000.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el quinto mes era el jefe Samhut izraíta. En su división había 24.000.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el sexto mes era Ira, hijo de Iques, de Tecoa. En su división había 24.000.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el séptimo mes era Heles pelonita, de los hijos de Efraín. En su división había 24.000.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el octavo mes era Sibecai husatita, de los zeraítas. En su división había 24.000.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el noveno mes era Abiezer anatotita, de los benjamitas. En su división había 24.000.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el décimo mes era Maharai netofatita, de los zeraítas. En su división había 24.000.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el mes undécimo era Benaía piratonita, de los hijos de Efraín. En su división había 24.000.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El comandante para el mes duodécimo era Heldai netofatita, de Otoniel. En su división había 24.000.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
Asimismo el caudillo de los rubenitas, Eliezer, hijo de Zicri, comandaba las tribus de Israel. De los simeonitas, Sefatías, hijo de Maaca.
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
De los levitas, Hasabías, hijo de Quemuel. De los de Aarón, Sadoc.
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
De Judá, Elihú, uno de los hermanos de David. De los de Isacar, Omri, hijo de Micael.
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
De los de Zabulón, Ismaías, hijo de Abdías. De los de Neftalí, Jerimot, hijo de Azriel.
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
De los hijos de Efraín, Oseas, hijo de Azazías. De la media tribu de Manasés, Joel, hijo de Pedaías.
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
De la otra media tribu de Manasés, en Galaad, Iddo, hijo de Zacarías. De los de Benjamín, Jaasiel, hijo de Abner.
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
De Dan, Azareel, hijo de Jeroham. Tales eran los jefes de las tribus de Israel.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
Pero David no tomó el censo de los que eran menores de 20 años, por cuanto Yavé dijo que Él multiplicaría a Israel como las estrellas del cielo.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Joab, hijo de Sarvia, comenzó a contar, pero no acabó, pues por eso hubo una explosión de ira contra Israel. Así el número no fue colocado en el registro de las crónicas del rey David.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Azmavet, hijo de Adiel, estaba a cargo de los tesoros del rey; Jonatán, hijo de Uzías, de los almacenes en el campo, las ciudades, aldeas y torres;
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
Ezri, hijo de Quelub, de los que trabajaban en la labranza de las tierras;
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
Simei ramadita, de las viñas; y Zabdi sifmita, del fruto de las viñas para las bodegas del vino.
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
Baal-hanán gederita [estaba a cargo] de los olivares e higuerales de la Sefela; de los almacenes del aceite, Joás;
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
del ganado que pastaba en Sarón, Sitrai saronita; del ganado que estaba en los valles, Safat, hijo de Adlai;
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
de los camellos, Obil ismaelita; de las asnas, Jehedías meronotita,
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
y de las ovejas, Jaziz agareno. Todos éstos eran administradores de la hacienda particular del rey David.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Jonatán, tío de David, varón prudente, era consejero y escriba, y Jehiel, hijo de Hacmoni, estaba con los hijos del rey.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
También Ahitofel era consejero del rey. Husai arquita era el amigo del rey.
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
Después de Ahitofel seguían Joiada, hijo de Benaía, y Abiatar. Joab era el general del ejército del rey.

< 1 Nyakati 27 >