< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
Esta es una lista de los israelitas, de los jefes de familia, de los comandantes de millares y de los comandantes de centenas, y de sus oficiales que servían al rey en todo lo relacionado con las divisiones que estaban de servicio cada mes durante el año. Había 24.000 hombres en cada división.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
Al mando de la primera división para el primer mes, estaba Jashobeam, hijo de Zabdiel. Tenía 24.000 hombres en su división.
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
Era descendiente de Fares y estaba a cargo de todos los oficiales del ejército durante el primer mes.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Al mando de la división para el segundo mes estaba Dodai el ahohita. Miclot era su jefe de división. Tenía 24.000 hombres en su división.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
El tercer comandante del ejército para el tercer mes era Benaía, hijo del sacerdote Joiada. Era el jefe y había 24.000 hombres en su división.
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
Este era el mismo Benaía que era un gran guerrero entre los Treinta, y estaba a cargo de los Treinta. Su hijo Amizabad era el jefe de su división.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El cuarto, para el cuarto mes, era Asael, hermano de Joab. Su hijo Zebadías fue su sucesor. Tenía 24.000 hombres en su división.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El quinto, para el quinto mes, era el comandante del ejército Shamhuth el Izrahita. Tenía 24.000 hombres en su división.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El sexto, para el sexto mes, era Ira, hijo de Iqués de Tecoa. Tenía 24.000 hombres en su división.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El séptimo, para el séptimo mes, era Heles el pelonita de la tribu de Efraín. Tenía 24.000 hombres en su división.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El octavo, para el octavo mes, era Sibecai de Husa, de la tribu de Zera. Tenía 24.000 hombres en su división.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El noveno, para el noveno mes, era Abiezer, de Anatot, de la tribu de Benjamín. Tenía 24.000 hombres en su división.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El décimo, para el décimo mes, era Maharai de Netofa, de la tribu de Zera. Tenía 24.000 hombres en su división.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El undécimo, para el undécimo mes, era Benaía, de Piratón, de la tribu de Efraín. Tenía 24.000 hombres en su división.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
El duodécimo, para el duodécimo mes, era Heldai de Netofa, de la familia de Otoniel. Tenía 24.000 hombres en su división.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
Esta es la lista de los jefes para las tribus de Israel: para los rubenitas Eliezer, hijo de Zicri; para los simeonitas: Sefatías, hijo de Maaca;
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
para Leví: Hasabías, hijo de Quemuel; para Aarón: Sadoc;
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
para Judá: Eliú, hermano de David; por Isacar Omri, hijo de Miguel;
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
para Zabulón Ismaías, hijo de Abdías; por Neftalí: Jerimot, hijo de Azriel;
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
por los efraimitas: Oseas, hijo de Azazías; por la media tribu de Manasés Joel, hijo de Pedaías;
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
para la media tribu de Manasés en Galaad Iddo, hijo de Zacarías; por Benjamín: Jaasiel, hijo de Abner;
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
por Dan: Azarel, hijo de Jeroham. Estos fueron los oficiales para las tribus de Israel.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
David no censó a los hombres menores de veinte años porque el Señor había dicho que haría a Israel tan numeroso como las estrellas del cielo.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Joab, hijo de Sarvia, había comenzado el censo, pero no lo terminó. Israel fue castigado a causa de este censo, y los resultados no fueron registrados en la cuenta oficial del rey David.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Azmavet, hijo de Adiel, estaba a cargo de los almacenes del rey, mientras que Jonatán, hijo de Uzías, estaba a cargo de los del campo, las ciudades, las aldeas y las torres de vigilancia.
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
Ezri, hijo de Quelub, estaba a cargo de los campesinos que trabajaban la tierra.
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
Simei, el ramatita, estaba a cargo de las viñas. Zabdi el sifmita estaba a cargo del producto de las viñas para las bodegas.
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
Baal-Hanán el gederita estaba a cargo de los olivos y los sicómoros de las colinas. Joás estaba a cargo de los almacenes de aceite de oliva.
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
Sitrai de Sarón estaba a cargo del ganado en los pastos de Sarón. Safat, hijo de Adlai, estaba a cargo del ganado en los valles.
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
Obil el ismaelita estaba a cargo de los camellos. Jehedías de Meronot estaba a cargo de los asnos.
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
Jaziz el agareno estaba a cargo de las ovejas y las cabras. Todos estos eran funcionarios a cargo de lo que pertenecía al rey David.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Jonatán, tío de David, era un consejero, un hombre perspicaz y un escriba. Jehiel, hijo de Hacmoni, cuidaba de los hijos del rey.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
Ahitofel era el consejero del rey y Husai, el arquita, era el amigo del rey.
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
Después de Ahitofel vino Joiada, hijo de Benaía y de Abiatar. Joab era el comandante del ejército real.

< 1 Nyakati 27 >