< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
Сынове же Израилевы но числу своему, началницы отечеств, тысящницы и сотницы и книгочии служащии царю, и на всякое слово царево по разделением, и на всякое слово входящаго и исходящаго, месяц от месяца, во вся месяцы лета разделение едино, двадесять четыре тысящы.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
И над первым разделением в первый месяц бысть Извоаз сын Завдиилов, в разделении его двадесять четыре тысящы:
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
от сынов Фаресовых, началник всем князем воинства месяца перваго.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
И над разделением месяца втораго Додай Екхотский и над разделением его, и Макеллоф вождь, и в разделении его двадесять четыре тысящи, князи силы.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
Третий месяца третияго Ванеа сын Иодаев, иже священник началный, и в разделении его двадесять четыре тысящы:
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
сей Ванеа крепчайший между тридесятми, и над тридесятми: и над разделением его Завад сын его.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Четвертый месяца четвертаго Асаил брат Иоавль, и Завадиа сын его и братия, и в полце его двадесять четыре тысящы.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Пятый пятаго месяца началник Самаоф сын Иезраев, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Шестый месяца шестаго Одуиа сын Еккисов Фекуитянин, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Седмый месяца седмаго Хеллис иже от Фалуса, от сынов Ефремлих, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Осмый месяца осмаго Совохай Усафитянин, от колена Зараина, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Девятый месяца девятаго Авиезер, иже от Анафофа, от земли Вениамини, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Десятый месяца десятаго Меирай, иже от Нетофафита, от колена Зараина, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Первыйнадесять месяца первагонадесять Ванаиа, иже от Фарафона, от сынов Ефремлих и в полце его двадесять и четыре тысящы.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Вторыйнадесять месяца вторагонадесять Холдиа, иже от Нетофафита, от колена Гофониилева, и в полце его двадесять и четыре тысящы.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
И над племены Израилевыми, Рувиму вождь Елиезер, сын Зехриев: Симеону Сафатиа, сын Мааха:
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
Левию Асавиа, сын Камуилев: Аарону Садок:
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
Иуде Елиав от братий Давидовых: Иссахару Амри, сын Михаилов:
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
Завулону Самаиа, сын Авдиев: Неффалиму Иеримоф, сын Озииль:
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
Ефрему Осий, сын Озазиев: полуплемени Манассиину Иоиль, сын Фадеев:
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
полуплемени Манассиину сущему в земли Галаадстей Иаддай сын Завадиин: сыном Вениаминим Иасиил, сын Авениров:
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
Дану Азариил, сын Иорамов. Сии быша началницы племеном Израилевым.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
Не хоте же Давид счести их от двадесятилетнаго и нижае: зане рече Господь умножити Израиля, яко звезды небесныя.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Иоав же сын Саруиев нача сочитати люди, и не соверши: сего ради бысть гнев Божий на Израиля: и не внесеся сочисление в книгу словес царя Давида.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Над сокровищи же царскими бысть Асмоф сын Одиилев: и над сокровищи, иже на нивах и в селех, и в весех и в столпех, Ионафан сын Озиев:
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
и над земледелатели землю делающими Ездрай сын Хелувов:
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
и над селы Семей Армафейский: и над сокровищами виноградными Замвдиа сын Сефамиев:
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
над маслинами же и над черничием, иже бяху на полях, Валанан Гедоритянин: над сокровищи елеа Иоас:
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
над скоты же, иже пасяхуся в Сароне, Сатрай Саронитянин: и над волы, иже во юдолех, Софат сын Адаин:
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
над велблюды же Увиа Исмаилтянин: над ослы же Иадиа, иже от Марафона:
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
и над овцами Иоас Агаритин. Вси тии началницы имений Давида царя.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Ионафан же дядя Давидов (бысть) советник, муж мудр и книжен сый: и Иеиль сын Ахаманиев бе с сынами царевыми.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
Ахитофел советник царев, и Хусиа первейший друг царев,
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
и по (нем) Ахитофеле бысть (близ)) Иодай сын Ванеин и Авиафар: и Иоав началный воевода царев.

< 1 Nyakati 27 >