< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
A oto synowie Izraela według ich liczby: naczelnicy rodów, tysiącznicy, setnicy i urzędnicy, którzy służyli królowi we wszelkiej sprawie związanej z oddziałami przychodzącymi i odchodzącymi co miesiąc, przez wszystkie miesiące w roku. Każdy oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
2 Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
Nad oddziałem w miesiącu pierwszym [stał] Jaszobeam, syn Zabdiela, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
3 Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
On pochodził z synów Peresa, a [był] wodzem wszystkich dowódców wojska w miesiącu pierwszym.
4 Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Nad oddziałem w miesiącu drugim [stał] Dodaj, Achochita. [Po nim] dowódcą był Miklot, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
5 Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
Trzecim dowódcą wojska, na miesiąc trzeci, [był] Benajasz, syn Jehojady, naczelnego kapłana, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
6 Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
Ten to Benajasz [był] waleczny wśród trzydziestu i dowodził trzydziestoma, a jego syn Ammizabad należał do jego oddziału.
7 Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Czwartym dowódcą, na miesiąc czwarty, [był] Asahel, brat Joaba, a po nim jego syn Zebadiasz – jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
8 Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Piątym dowódcą, na piąty miesiąc, [był] Szamhut Jizrachita, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
9 Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Szóstym, na miesiąc szósty, [był] Ira, syn Ikkesza Tekoitczyka, a jego oddział [liczył] dwudziestu czterech.
10 Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Siódmym, na miesiąc siódmy, [był] Cheles Pelonita, z synów Efraima, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
11 Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Ósmym, na miesiąc ósmy, [był] Sibbekaj Chuszatyta, z Zerachitów, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
12 Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Dziewiątym, na miesiąc dziewiąty, [był] Abiezer Anatotczyk, z synów Beniamina, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
13 Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Dziesiątym, na miesiąc dziesiąty, [był] Maharaj Netofatyta, z Zerachitów, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
14 Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Jedenastym, na miesiąc jedenasty, [był] Benajasz Piratończyk, z synów Efraima, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
15 Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
Dwunastym, na miesiąc dwunasty, [był] Cheldaj Netofatyta, z Otniela, a jego oddział [liczył] dwadzieścia cztery tysiące.
16 Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
Ponadto nad pokoleniami Izraela [postawieni byli]: nad Rubenitami przełożonym [był] Eliezer, syn Zikriego; nad Symeonitami – Szefatiasz, syn Maaki;
17 kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
Nad Lewitami – Chaszabiasz, syn Kemuela, nad Aaronitami – Sadok;
18 kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
Nad Judą – Elihu, [jeden] z braci Dawida, nad Issacharytami – Omri, syn Mikaela;
19 kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
Nad Zebulonitami – Jiszmajasz, syn Obadiasza, nad Neftalitami – Jerimot, syn Azriela;
20 kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
Nad synami Efraima – Ozeasz, syn Azazjasza, nad połową pokolenia Manassesa – Joel, syn Pedajasza;
21 kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
Nad [drugą] połową [pokolenia] Manassesa w Gileadzie – Iddo, syn Zachariasza, nad Beniaminatami – Jaasiel, syn Abnera.
22 kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
Nad Danitami – Azareel, syn Jerochama. Ci [byli] książętami pokoleń Izraela.
23 Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
Dawid nie włączył jednak do spisu [nikogo], kto miał dwadzieścia lat lub mniej. PAN powiedział bowiem, że rozmnoży Izraela jak gwiazdy na niebie.
24 Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
Joab, syn Serui, zaczął [ich] liczyć, ale nie dokończył, gdyż za to spadł gniew na Izraela. Nie włączono więc tej liczby do spisu w kronikach króla Dawida.
25 Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
Nad skarbcami króla [postawiony był] Azmawet, syn Adiela; nad dochodami z pól, miast, wsi i zamków – Jonatan, syn Uzjasza;
26 Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
Nad rolnikami, [którzy] uprawiali ziemię, [stał] Ezri, syn Keluba.
27 Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
Nad winnicami – Szimei Ramatczyk; nad plonami winnic w piwnicach – Zabdi Szifmita.
28 Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
Nad drzewami oliwnymi i sykomorami, które [rosły] na równinach, [postawiony był] Baalchanan Gederczyk, a nad składami oliwy – Joasz.
29 Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
Nad bydłem pasącym się w Szaronie – Szitraj Szarończyk, nad bydłem zaś w dolinach – Szafat, syn Adlaja.
30 Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
Nad wielbłądami – Obil Izmaelita, nad oślicami – Jechdejasz Meronotyta.
31 Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
I nad owcami – Jaziz Hagryta. Ci wszyscy [byli] zarządcami dobytku króla Dawida.
32 Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
Jonatan, stryj Dawida, [był] doradcą, człowiekiem mądrym i uczonym. Jechiel, syn Chakmoniego, [był] z synami króla.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
Achitofel też [był] doradcą króla, a Chuszaj Arkita – przyjacielem króla.
34 Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.
Po Achitofelu [był] Jehojada, syn Benajasza, i Abiatar. Joab zaś [był] dowódcą wojska króla.

< 1 Nyakati 27 >